Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 6.3
Bible en Swahili de l’est


Péchés de Juda et annonce du jugement

1 Kimbieni mpate kuwa salama, enyi wana wa Benyamini; tokeni katika Yerusalemu, pigeni tarumbeta katika Tekoa, simamisheni ishara juu ya Beth-hakeremu; kwa maana mabaya yanachungulia toka kaskazini, na uharibifu mkuu.
Néhémie 3.14 2 Chroniques 11.6 Jérémie 6.22 Juges 1.21 2 Samuel 14.2
2 Binti Sayuni aliye mzuri, mwororo, nitamkatilia mbali.
Esaïe 1.8 Jérémie 4.31 Esaïe 3.16-3.17 Lamentations 2.1 Lamentations 2.13
3 Wachungaji na makundi yao ya kondoo watamjilia; watapiga hema zao karibu naye pande zote; watalisha kila mmoja mahali pake.
Luc 19.43 Jérémie 4.16-4.17 2 Rois 24.10-24.12 2 Rois 25.1-25.4 2 Rois 24.2
4 Takaseni vita juu yake; inukeni, na tupande juu wakati wa adhuhuri. Ole wetu, kwa kuwa mchana umeanza kupungua, vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
Jérémie 15.8 Joël 3.9 Sophonie 2.4 Cantique 2.17 Esaïe 5.26-5.30
5 Inukeni, na tupande juu wakati wa usiku, tukayaharibu majumba yake.
Jérémie 52.13 Esaïe 32.14 Amos 3.10-3.11 Amos 2.5 Jérémie 9.21
6 Maana Bwana wa majeshi asema hivi, Jikatieni miti, mfanyize boma juu ya Yerusalemu. Mji huu ni mji unaojiliwa; dhuluma tupu imo ndani yake.
Jérémie 32.24 Deutéronome 20.19-20.20
7 Kama vile kisima kitoavyo maji yake, ndivyo utoavyo uovu wake; jeuri na kuharibu kwasikiwa ndani yake; ugonjwa na jeraha zi mbele zangu daima.
Ezéchiel 7.23 Ezéchiel 7.11 Jérémie 20.8 Esaïe 57.20 Michée 3.1-3.3
8 Uadhibishwe, Ee Yerusalemu, nafsi yangu, isije ikafarakana nawe; nisije nikakufanya ukiwa, nchi isiyokaliwa na watu.
Osée 9.12 Ezéchiel 23.18 Jérémie 17.23 Jérémie 35.13-35.15 Psaumes 50.17
9 Bwana wa majeshi asema hivi, Wataokota mabaki ya Israeli kama mzabibu; rudisha mkono wako ndani ya vikapu, kama mchuma zabibu.
Jérémie 16.16 Abdias 1.5-1.6 Jérémie 49.9 Apocalypse 14.18 Jérémie 52.28-52.30
10 Niseme na nani na kushuhudia, wapate kusikia? Tazama, sikio lao halikutahiriwa, wala hawawezi kusikiliza; tazama, neno la Bwana limekuwa matukano kwao; hawalifurahii.
Actes 7.51 Jérémie 7.26 Exode 6.12 Esaïe 53.1 Hébreux 11.7
11 Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana; nimechoka kwa kujizuia; imwageni juu ya watoto walio njiani, na juu ya kusanyiko la vijana pia; maana hata mume atatwaliwa pamoja na mkewe, mzee pamoja na yeye aliyetimiza siku zake.
Jérémie 9.21 Jérémie 20.9 Michée 3.8 Job 32.18-32.19 Jérémie 18.21
12 Na nyumba zao zitakuwa mali za watu wengine, mashamba yao na wake zao pamoja; kwa kuwa nitaunyosha mkono wangu juu ya wenyeji wa nchi hii, asema Bwana.
Jérémie 8.10 Esaïe 5.25 Esaïe 9.12 Esaïe 9.17 Lamentations 5.3
13 Kwa maana, tangu aliye mdogo hata aliye mkubwa miongoni mwao, kila mmoja ni mtamanifu; na, tangu nabii hata kuhani, kila mmoja hutenda mambo ya udanganyifu.
Jérémie 23.11 Jérémie 8.10 Michée 3.11 Michée 3.2-3.3 Ezéchiel 22.25-22.28
14 Wameiponya jeraha ya watu wangu kwa juu juu tu, wakisema, Amani, Amani, wala hapana amani.
Ezéchiel 13.10 Jérémie 23.17 Jérémie 14.13 Jérémie 4.10 Lamentations 2.14
15 Je! Walitahayarika, walipokuwa wameunda machukizo? La, hawakutahayarika hata kidogo, wala hawakuweza kuona haya usoni; basi, wataanguka miongoni mwa hao waangukao; wakati nitakapowajilia wataangushwa chini, asema Bwana.
Jérémie 8.12 Jérémie 3.3 Sophonie 3.5 Jérémie 5.29 Ezéchiel 7.6-7.9
16 Bwana asema hivi, Simameni katika njia kuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katika njia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu. Lakini walisema, Hatutaki kwenda katika njia hiyo.
Jérémie 18.15 Deutéronome 32.7 Malachie 4.4 Esaïe 30.21 Luc 16.29
17 Nami naliweka walinzi juu yenu, wakisema, Isikilizeni sauti ya tarumbeta; lakini walisema, Hatutaki kusikiliza.
Esaïe 58.1 Jérémie 25.4 Zacharie 7.11 Esaïe 21.11 Habakuk 2.1
18 Kwa sababu hiyo sikilizeni, enyi mataifa, mkajue, Ee kusanyiko, ni jambo gani litokealo kati yao.
Deutéronome 29.24-29.28 Esaïe 5.3 Jérémie 4.10 Jérémie 31.10 Michée 6.5
19 Sikia, Ee nchi; tazama, nitaleta mabaya juu ya watu hawa, naam, matunda ya mawazo yao, kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu; tena kwa habari ya sheria yangu, wameikataa.
Jérémie 8.9 Jérémie 22.29 Esaïe 1.2 Jean 3.19-3.21 Actes 8.22
20 Yafaa nini niletewe ubani kutoka Sheba, na uudi kutoka nchi iliyo mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa hazikubaliwi, wala dhabihu zenu haziniridhii.
Esaïe 1.11 Esaïe 60.6 Amos 5.21-5.22 Michée 6.6-6.8 Psaumes 40.6
21 Basi, kwa hiyo, Bwana asema hivi, Tazama, nitaweka makwazo mbele ya watu hawa, na baba na wana wao watajikwaa pamoja; jirani ya mtu na rafiki yake watapotea.
Esaïe 8.14 Ezéchiel 3.20 Jérémie 13.16 Esaïe 9.14-9.17 Jérémie 19.7-19.9
22 Bwana asema hivi, Tazama, watu wanakuja, wakitoka katika nchi ya kaskazini; na taifa kubwa litaamshwa, litokalo katika pande za mwisho wa dunia.
Jérémie 50.41-50.43 Jérémie 10.22 Jérémie 25.9 Jérémie 6.1 Jérémie 1.14-1.15
23 Washika upinde na mkuki; ni wakatili, hawana huruma; sauti yao huvuma kama bahari, nao wamepanda farasi zao; kila mmoja kama mtu wa vita amejipanga juu yako, Ee binti Sayuni.
Esaïe 13.18 Jérémie 50.42 Esaïe 19.4 Esaïe 5.26-5.30 Jérémie 30.14
24 Tumesikia habari zake; mikono yetu inalegea; dhiki imetushika, na utungu kama wa mwanamke wakati wa kuzaa kwake.
Jérémie 50.43 Jérémie 49.24 Jérémie 4.31 Esaïe 28.19 Jérémie 30.6
25 Msitoke kwenda mashambani, wala msitembee njiani, kwa maana upanga wa adui uko huko; hofu ziko pande zote.
Jérémie 49.29 Jérémie 20.10 Jérémie 14.18 Psaumes 31.13 Job 18.11
26 Ee binti wa watu wangu, ujivike nguo ya magunia, na kugaagaa katika majivu; fanya maombolezo, kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, maombolezo ya uchungu mwingi; maana mwenye kuteka nyara atakuja juu yetu ghafula.
Jérémie 4.8 Zacharie 12.10 Jérémie 13.17 Esaïe 22.12 Jérémie 12.12
27 Nimekuweka uwe mnara na ngome kati ya watu wangu; upate kuijua njia yao na kuijaribu.
Jérémie 1.18 Jérémie 15.20 Jérémie 9.7 Ezéchiel 20.4 Ezéchiel 3.8-3.10
28 Ni waasi kupita kiasi wote pia, waendao huko na huko wakisingizia, ni shaba na chuma hao, hutenda dhuluma wote pia.
Jérémie 9.4 Jérémie 5.23 Jérémie 18.18 Jérémie 20.10 Apocalypse 11.18
29 Mifuo inafukuta kwa nguvu; risasi tu inatoka katika moto huo; mfua fedha ameyeyusha bure tu; maana wabaya hawaondolewi mbali.
Malachie 3.2-3.3 Esaïe 49.4 Ezéchiel 24.13 1 Pierre 4.12 Zacharie 13.9
30 Watu watawaita taka za fedha, kwa sababu Bwana amewakataa.
Psaumes 119.119 Osée 9.17 Esaïe 1.22 Esaïe 1.25 Proverbes 25.4

Cette Bible est dans le domaine public.