Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 28.1
Bible en Swahili de l’est


Jérémie et Hanania

1 Ikawa, katika mwaka ule ule, mwanzo wa kutawala kwake Sedekia, mfalme wa Yuda, mwaka wa nne, mwezi wa tano, Hanania, mwana wa Azuri, nabii, wa Gibeoni, akasema nami ndani ya nyumba ya Bwana, mbele ya makuhani na watu wote, akisema,
Jérémie 27.1 Josué 9.3 Esaïe 9.15 Zacharie 13.2-13.4 Jérémie 36.12
2 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimeivunja nira ya mfalme wa Babeli.
Ezéchiel 13.5-13.16 Jérémie 27.2-27.12 Michée 3.11
3 Kabla haujatimia muda wa miaka miwili mizima, nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana, ambavyo Nebukadreza, mfalme wa Babeli, aliviondoa katika mahali hapa, akavichukua mpaka Babeli.
2 Rois 24.13 2 Chroniques 36.10 Daniel 1.2 Psaumes 90.10 Jérémie 27.16-27.22
4 Nami nitamrudisha hapa Yekonia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, pamoja na mateka wote wa Yuda, waliokwenda Babeli, asema Bwana; maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
Jérémie 22.24 Jérémie 24.1 Jérémie 28.2 Jérémie 52.31-52.34 2 Rois 25.27-25.30
5 Ndipo nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, mbele ya makuhani, na mbele ya watu wote waliosimama ndani ya nyumba ya Bwana,
Jérémie 28.1 Jérémie 7.2 Jérémie 19.14 Jérémie 26.2
6 naam, nabii Yeremia akasema, Amina, Bwana na atende hivi; Bwana ayatimize maneno yako uliyotabiri, kuvirudisha hapa vyombo vya nyumba ya Bwana na watu wote waliofungwa, toka Babeli, hata mahali hapa.
1 Rois 1.36 Psaumes 41.13 Jérémie 11.5 Psaumes 106.48 Jérémie 18.20
7 Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote,
1 Rois 22.28
8 Manabii waliokuwako kabla ya zamani zangu, na zamani zako, walitabiri juu ya nchi nyingi, na juu ya falme kubwa, habari ya vita, na ya mabaya, na ya tauni.
Amos 1.2 1 Rois 17.1 1 Samuel 2.27-2.32 1 Samuel 3.11-3.14 Deutéronome 31.16-31.17
9 Nabii atabiriye habari za amani, neno la nabii yule litakapotokea, ndipo nabii yule atakapojulikana, kuwa Bwana amemtuma kweli kweli.
Deutéronome 18.22 Jérémie 6.14 Ezéchiel 13.10-13.16 Jérémie 14.13 Jérémie 8.11
10 Ndipo nabii Hanania akaitwaa hiyo nira iliyokuwa juu ya shingo ya Yeremia, akaivunja.
Jérémie 27.2 Jérémie 28.2 Malachie 3.13 1 Rois 22.11 1 Rois 22.24-22.25
11 Naye Hanania akanena mbele ya watu wote, akisema, Bwana asema hivi, Hivyo ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kabla haujatimia muda wa miaka miwili mizima, na kuiondoa shingoni mwa mataifa yote. Basi nabii Yeremia akaenda zake.
1 Rois 22.11-22.12 1 Rois 13.18 2 Chroniques 18.22-18.23 Proverbes 14.7 Jérémie 23.17
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, baada ya Hanania, nabii, kuivunja ile nira iliyokuwa juu ya shingo ya Yeremia, kusema,
Jérémie 1.2 Jérémie 29.30 1 Chroniques 17.3 2 Rois 20.4 Daniel 9.2
13 Enenda ukamwambie Hanania, ukisema, Bwana asema hivi, Umezivunja nira za mti; lakini badala yake utafanya nira za chuma.
Psaumes 149.8 Lamentations 2.14 Jérémie 27.15
14 Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimetia nira ya chuma juu ya shingo ya mataifa haya yote, ili wamtumikie Nebukadreza, mfalme wa Babeli nao watamtumikia; nami nimempa wanyama wa nchi pia.
Deutéronome 28.48 Jérémie 27.6-27.7 Deutéronome 4.20 Apocalypse 17.12-17.13 Jérémie 25.9-25.26
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini unawatumainisha watu hawa maneno ya uongo.
Ezéchiel 13.22 Lamentations 2.14 Zacharie 13.3 Ezéchiel 13.2-13.3 Ezéchiel 22.28
16 Basi Bwana asema hivi, Tazama, nakutuma uende zako toka juu ya uso wa nchi; mwaka huu utakufa, kwa sababu umenena maneno ya uasi juu ya Bwana.
Jérémie 29.32 Genèse 7.4 1 Rois 13.34 Jérémie 20.6 Exode 32.12
17 Basi nabii Hanania akafa, mwaka uo huo, mwezi wa saba.
Zacharie 1.6 Esaïe 44.25-44.26

Cette Bible est dans le domaine public.