Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 51.19
Bible en Swahili de l’est


Promesses de délivrance

1 Nisikilizeni, ninyi mnaoifuatia haki; ninyi mnaomtafuta Bwana; uangalieni mwamba ule ambao mlitolewa kwa kuchongwa, na tundu la shimo ambalo mlitolewa kwa kuchimbuliwa.
Esaïe 51.7 Psaumes 94.15 Hébreux 12.14 Genèse 17.15-17.17 Romains 9.30-9.32
2 Mwangalieni Ibrahimu, baba yenu, na Sara, aliyewazaa; kwa maana alipokuwa mmoja tu nalimwita, nikambariki, nikamfanya kuwa wengi.
Ezéchiel 33.24 Galates 3.9-3.14 Romains 4.16-4.24 Genèse 24.35 Genèse 22.17
3 Maana Bwana ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama bustani ya Edeni, na nyika yake kama bustani ya Bwana; furaha na kicheko zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba.
Esaïe 52.9 Joël 2.3 Genèse 13.10 Esaïe 49.13 Psaumes 85.8
4 Nisikilizeni mimi, enyi watu wangu; nisikieni, taifa langu; maana sheria itatoka kwangu, nami nitaistarehesha hukumu yangu iwe nuru ya mataifa.
Esaïe 42.6 Esaïe 2.3 Michée 4.2 Esaïe 49.6 Esaïe 26.2
5 Haki yangu i karibu, wokovu wangu umekuwa wazi, na mikono yangu itawahukumu kabila za watu; visiwa vitaningoja, navyo vitautumainia mkono wangu.
Esaïe 46.13 Esaïe 42.4 Esaïe 60.9 2 Corinthiens 5.10 Romains 15.9-15.12
6 Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na haki yangu haitatanguka.
Esaïe 34.4 Matthieu 24.35 Esaïe 40.26 2 Pierre 3.10-3.12 Apocalypse 6.12-6.14
7 Nisikilizeni, ninyi mjuao haki, watu ambao mioyoni mwenu mna sheria yangu; msiogope matukano ya watu, wala msifadhaike kwa sababu ya dhihaka zao.
Psaumes 37.31 Matthieu 5.11 Matthieu 10.28 Ezéchiel 2.6 Actes 5.41
8 Maana nondo itawala kama vazi, na funza atawala kama sufu; bali haki yangu itakuwa ya milele, na wokovu wangu hata vizazi vyote.
Esaïe 50.9 Esaïe 51.6 Esaïe 66.24 Job 4.19 Esaïe 45.17
9 Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana; Amka kama katika siku zile za kale, Katika vizazi vile vya zamani.
Psaumes 74.13-74.14 Esaïe 27.1 Esaïe 52.1 Esaïe 51.17 Job 26.12
10 Si wewe uliyemkata-kata Rahabu? Uliyemchoma yule joka? Si wewe uliyeikausha bahari, Na maji ya vilindi vikuu; Uliyevifanya vilindi kuwa njia, Ili wapite watu waliokombolewa?
Esaïe 50.2 Exode 14.21-14.22 Exode 15.13 Esaïe 43.16 Esaïe 63.11-63.12
11 Nao waliokombolewa na Bwana watarejea, Watafika Sayuni, wakiimba; Furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; Watapata shangwe na furaha; Huzuni na kuugua zitakimbia.
Esaïe 35.10 Apocalypse 7.17 Apocalypse 21.4 Esaïe 25.8 Esaïe 60.19-60.20
12 Mimi, naam, mimi, ndimi niwafarijiye; wewe u nani hata ukamwogopa mtu atakayekufa, na mwanadamu atakayefanywa kuwa kama majani?
1 Pierre 1.24 Psaumes 118.6 Esaïe 2.22 Esaïe 51.3 Jean 14.26-14.27
13 Ukamsahau Bwana, Muumba wako, yeye aliyezitanda mbingu, na kuiweka misingi ya dunia; nawe unaogopa daima mchana kutwa kwa sababu ya ghadhabu yake yeye aoneaye, hapo afanyapo tayari kuharibu; nayo i wapi ghadhabu yake aoneaye?
Psaumes 104.2 Esaïe 40.22 Esaïe 17.10 Job 9.8 Esaïe 45.12
14 Yeye aliyehamishwa na kufungwa atafunguliwa kwa haraka; wala hatakufa na kushuka shimoni, wala chakula chake hakitapunguka.
Zacharie 9.11 Esaïe 52.2 Esaïe 48.20 Actes 12.7-12.8 Esdras 1.5
15 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako, niichafuaye bahari, mawimbi yake yakavuma.
Jérémie 31.35 Psaumes 136.13 Psaumes 114.3-114.5 Esaïe 47.4 Psaumes 74.13
16 Bwana wa majeshi ndilo jina lake. Nami nimetia maneno yangu kinywani mwako, nami nimekusitiri katika kivuli cha mkono wangu, ili nizipande mbingu, na kuiweka misingi ya dunia, na kuuambia Sayuni, Ninyi ni watu wangu.
Esaïe 59.21 Deutéronome 18.18 Esaïe 49.2 Psaumes 75.3 Esaïe 66.22
17 Amka, amka, simama, Ee Yerusalemu, Wewe uliyenywea, mkononi mwa Bwana, Kikombe cha hasira yake; Bakuli la kikombe cha kulevya-levya Umelinywea na kulimaliza.
Esaïe 52.1 Job 21.20 Esaïe 51.9 Psaumes 60.3 Apocalypse 14.10
18 Hapana hata mmoja wa kumwongoza Miongoni mwa wana wote aliowazaa, Wala hapana hata mmoja wa kumshika mkono Miongoni mwa wana wote aliowalea.
Esaïe 49.21 Psaumes 88.18 Psaumes 142.4 Actes 13.11 Actes 9.8
19 Mambo haya mawili yamekupata; Ni nani awezaye kukusikitikia? Ukiwa na uharibifu, na njaa na upanga; Niwezeje kukutuliza?
Amos 7.2 Esaïe 47.9 Ezéchiel 14.21 Ecclésiaste 4.1 Job 2.11
20 Wana wako wamezimia, Wamelala penye pembe za njia kuu zote Kama kulungu wavuni; Wamejaa hasira ya Bwana, Lawama ya Mungu wako.
Lamentations 2.11-2.12 Esaïe 8.21 Esaïe 9.19-9.21 Deutéronome 14.5 Esaïe 40.30
21 Basi, kwa sababu ya hayo, ulisikilize neno hili, ewe uliyeteswa, na kulewa, lakini si kwa mvinyo;
Esaïe 54.11 Esaïe 29.9 Esaïe 51.17
22 Bwana, Bwana wako na Mungu wako, awateteaye watu wake, asema hivi, Tazama, nimeondoa mkononi mwako kikombe cha kulevya-levya, hilo bakuli la kikombe cha hasira yangu; hutakinywea tena;
Esaïe 51.17 Jérémie 50.34 Esaïe 49.25 Psaumes 35.1 Esaïe 62.8
23 nami nitakitia mikononi mwao wakutesao; waliokuambia nafsi yako, Inama, tupate kupita; nawe uliufanya mgongo wako kuwa kama nchi, na kama njia, kwa hao wapitao juu yake.
Zacharie 12.2 Josué 10.24 Proverbes 21.18 Apocalypse 17.18 Apocalypse 17.6-17.8

Cette Bible est dans le domaine public.