Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 48.12
Bible en Swahili de l’est


Anciennes et nouvelles prédictions

1 Sikieni haya, enyi watu wa nyumba ya Yakobo, mnaoitwa kwa jina la Israeli, mliotoka katika maji ya Yuda; mnaoapa kwa jina la Bwana, na kumtaja Mungu wa Israeli, lakini si kwa kweli, wala si kwa haki.
Psaumes 68.26 Jérémie 4.2 Deutéronome 33.28 Nombres 24.7 Esaïe 45.23
2 Maana hujiita wenyeji wa mji mtakatifu, hujitegemeza juu ya Mungu wa Israeli; Bwana wa majeshi ni jina lake.
Michée 3.11 Esaïe 10.20 Romains 2.17 Esaïe 52.1 Jérémie 21.2
3 Mimi nimehubiri mambo ya kale tangu zamani; naam, yalitoka katika kinywa changu, nikayadhihirisha; naliyatenda kwa ghafula, yakatokea.
Esaïe 41.22 Esaïe 42.9 Josué 21.45 Esaïe 43.9 Esaïe 44.7-44.8
4 Kwa sababu nalijua ya kuwa wewe u mkaidi, na shingo yako ni shingo ya chuma, na kipaji cha uso wako ni shaba;
Exode 32.9 Deutéronome 31.27 Actes 7.51 Zacharie 7.11-7.12 Exode 33.3
5 basi nimekuonyesha tangu zamani; kabla hayajatukia nalikuonyesha; usije ukasema, Sanamu yangu imetenda haya; sanamu yangu ya kuchonga, na sanamu yangu ya kuyeyusha, imeyaamuru.
Luc 1.70 Esaïe 48.3 Jérémie 44.15-44.18 Esaïe 42.8-42.9 Esaïe 44.7
6 Umesikia haya; tazama haya yote; nanyi, je! Hamtayahubiri? Nimekuonyesha mambo mapya tangu wakati huu, naam, mambo yaliyofichwa, usiyoyajua.
Esaïe 42.9 Esaïe 43.8-43.10 Esaïe 21.10 Apocalypse 4.1 Psaumes 40.9-40.10
7 Yameumbwa sasa, wala si tokea zamani; na kabla ya siku hii ya leo hukusikia habari yake; usije ukasema, Tazama, naliyajua.
8 Naam, hukusikia; naam, hukujua; naam, tokea zamani sikio lako halikuzibuka; maana nalijua ya kuwa wewe watenda kwa hila nyingi, nawe umeitwa mkosaji tangu kuzaliwa kwako;
Psaumes 58.3 Esaïe 42.19-42.20 Osée 6.7 Psaumes 139.1-139.4 Jérémie 3.7-3.11
9 kwa ajili ya jina langu nitaahirisha hasira yangu, na kwa ajili yako nitajizuia, ili nisifiwe, wala nisikukatilie mbali.
Psaumes 78.38 Esaïe 48.11 Néhémie 9.30-9.31 Psaumes 103.8-103.10 Ezéchiel 20.22
10 Tazama, nimekusafisha, lakini si kama fedha; nimekuchagua katika tanuru ya mateso.
Deutéronome 4.20 Jérémie 9.7 Proverbes 17.3 Ezéchiel 22.18-22.22 Job 23.10
11 Kwa ajili ya nafsi yangu, kwa ajili ya nafsi yangu, nitatenda haya; je! Litiwe unajisi jina langu? Wala sitampa mwingine utukufu wangu.
Esaïe 42.8 Ezéchiel 20.9 Deutéronome 32.26-32.27 Ezéchiel 20.44 Jérémie 14.7

Appel à écouter Dieu

12 Nisikilize mimi, Ee Yakobo; na Israeli, niliyekuita; mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho pia.
Esaïe 41.4 Apocalypse 22.13 Esaïe 55.3 Esaïe 46.3 Esaïe 49.1
13 Naam, mkono wangu umeuweka msingi wa dunia, na mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo husimama pamoja.
Esaïe 40.26 Hébreux 1.10-1.12 Exode 20.11 Psaumes 102.25 Esaïe 42.5
14 Kusanyikeni, ninyi nyote, mkasikie; ni nani miongoni mwao aliyehubiri haya? Bwana amempenda; atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli, na mkono wake utakuwa juu ya Wakaldayo.
Esaïe 43.9 Esaïe 13.17-13.18 Jérémie 50.21-50.29 Esaïe 45.20-45.21 Esaïe 46.10-46.11
15 Mimi, naam, mimi, nimenena; naam, nimemwita; nimemleta, naye ataifanikisha njia yake.
Esaïe 45.1-45.2 Josué 1.8 Ezéchiel 1.2 Psaumes 45.4
16 Nikaribieni, sikieni haya; tokea mwanzo sikunena kwa siri; tangu yalipokuwapo, mimi nipo; na sasa Bwana MUNGU amenituma, na roho yake.
Esaïe 45.19 Jean 18.20 Jean 20.21-20.22 Esaïe 61.1-61.3 Jean 3.34
17 Bwana, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.
Psaumes 32.8 Deutéronome 8.17-8.18 Job 22.21-22.22 Psaumes 25.12 Job 36.22
18 Laiti ungalisikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari;
Esaïe 66.12 Deutéronome 32.29 Psaumes 119.165 Deutéronome 5.29 Amos 5.24
19 Tena wazao wako wangalikuwa kama mchanga, na hao waliotoka katika tumbo lako kama chembe zake; jina lake lisingalikatika, wala kufutwa mbele zangu.
Esaïe 10.22 Genèse 22.17 Jérémie 33.22 Osée 1.10 Ruth 4.10
20 Haya, tokeni katika Babeli, Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo; Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya, Yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni, Bwana amemkomboa mtumishi wake, Yakobo.
Esaïe 52.9 Jérémie 50.8 Jérémie 51.45 Jérémie 51.6 Zacharie 2.6-2.7
21 Wala hawakuona kiu alipowaongoza jangwani; Alitoa maji katika mwamba kwa ajili yao; Pia akaupasua mwamba, maji yakatoka kwa nguvu.
Exode 17.6 Esaïe 30.25 Nombres 20.11 Psaumes 105.41 Psaumes 78.15
22 Hapana amani kwa wabaya, asema Bwana.
Esaïe 57.21 Job 15.20-15.24 Luc 19.42 Romains 3.17

Cette Bible est dans le domaine public.