Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 40.23
Bible en Swahili de l’est


La consolation d’Israël

Venue prochaine du Seigneur

1 Watulizeni mioyo, watulizeni mioyo, watu wangu, asema Mungu wenu.
Sophonie 3.14-3.17 Esaïe 51.12 2 Corinthiens 1.4 Jérémie 31.10-31.14 Esaïe 51.3
2 Semeni na moyo wa Yerusalemu, kauambieni kwa sauti kuu ya kwamba vita vyake vimekwisha, uovu wake umeachiliwa; kwa kuwa amepokea kwa mkono wa Bwana adhabu maradufu kwa dhambi zake zote.
Zacharie 9.12 Esaïe 61.7 Osée 2.14 Jérémie 16.18 Esaïe 43.25
3 Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu.
Marc 1.2-1.5 Jean 1.23 Malachie 3.1 Luc 1.16-1.17 Matthieu 3.1-3.3
4 Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa;
Luc 3.5 Ezéchiel 21.26 Esaïe 2.12-2.15 Esaïe 45.2 Job 40.11-40.13
5 Na utukufu wa Bwana utafunuliwa, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya.
Luc 3.6 Habakuk 2.14 2 Corinthiens 4.6 Esaïe 6.3 Esaïe 52.10
6 Sikiliza, ni sauti ya mtu asemaye, Lia! Nikasema, Nilie nini? Wote wenye mwili ni majani, Na wema wake wote ni kama ua la kondeni;
Job 14.2 Psaumes 103.15-103.16 Psaumes 102.11 Jacques 1.10-1.11 1 Pierre 1.24-1.25
7 Majani yakauka, ua lanyauka; Kwa sababu pumzi ya Bwana yapita juu yake. Yakini watu hawa ni majani.
Job 41.21
8 Majani yakauka, ua lanyauka; Bali neno la Mungu wetu litasimama milele.
Marc 13.31 Matthieu 24.35 1 Pierre 1.25 Matthieu 5.18 Esaïe 55.10-55.11
9 Wewe uuhubiriye Sayuni habari njema, Panda juu ya mlima mrefu; Wewe uuhubiriye Yerusalemu habari njema, Paza sauti kwa nguvu; Paza sauti yako, usiogope; Iambie miji ya Yuda, Tazameni, Mungu wenu.
Esaïe 12.2 Esaïe 25.9 Esaïe 52.7-52.8 Ephésiens 6.19 Esaïe 61.1
10 Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, Na ijara yake i mbele zake.
Apocalypse 22.12 Esaïe 62.11 Esaïe 9.6-9.7 Psaumes 110.6 Esaïe 49.4
11 Atalilisha kundi lake kama mchungaji, Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.
Michée 5.4 Ezéchiel 34.23 Ezéchiel 34.12-34.14 Psaumes 23.1-23.6 Ezéchiel 34.31
12 Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?
Proverbes 30.4 Hébreux 1.10-1.12 Psaumes 102.25-102.26 Job 38.4-38.11 Esaïe 48.13
13 Ni nani aliyemwongoza roho ya Bwana, na kumfundisha kwa kuwa mshauri wake?
1 Corinthiens 2.16 Romains 11.34 Job 21.22 Jean 1.13 Ephésiens 1.11
14 Alifanya shauri na nani, ni nani aliyemwelimisha na kumfunza njia ya hukumu, na kumfunza maarifa, na kumwonyesha njia ya fahamu?
Colossiens 2.3 Job 21.22 1 Corinthiens 12.4-12.6 Jacques 1.17
15 Tazama, mataifa ni kama tone la maji katika ndoo, huhesabiwa kuwa kama mavumbi membamba katika mizani; tazama, yeye huvinyanyua visiwa kama ni kitu kidogo sana.
Esaïe 40.22 Jérémie 10.10 Esaïe 59.18 Job 34.14-34.15 Esaïe 29.5
16 Lebanoni nayo hautoshi kwa kuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa kafara.
Michée 6.6-6.7 Psaumes 40.6 Psaumes 50.9-50.12 Hébreux 10.5-10.10
17 Mataifa yote huwa kama si kitu mbele zake; huhesabiwa kwake kuwa duni ya si kitu, na ubatili.
Psaumes 62.9 Daniel 4.34-4.35 Job 25.6 Esaïe 29.7 2 Corinthiens 12.11
18 Basi, mtamlinganisha Mungu na nani? Au mtamfananisha na mfano wa namna gani?
Esaïe 46.5 Actes 17.29 1 Samuel 2.2 Esaïe 40.25 Exode 8.10
19 Sanamu fundi mmoja huiyeyusha, na mfua dhahabu huifunika dhahabu, huifulia mikufu ya fedha.
Psaumes 115.4-115.8 Habakuk 2.18-2.19 Jérémie 10.9 Esaïe 37.18-37.19 Psaumes 135.18
20 Yeye aliye maskini sana hata hawezi kutoa sadaka ya namna hii, huchagua mti usiooza, hujitafutia fundi mstadi wa kusimamisha sanamu ya kuchonga isiyoweza kutikisika.
Jérémie 10.3-10.4 Esaïe 46.7 1 Samuel 5.3-5.4 Esaïe 41.7 Esaïe 2.8-2.9
21 Je! Hamkujua? Hamkusikia? Hamkuambiwa tokea mwanzo? Hamkufahamu tangu kuwekwa misingi ya dunia?
Actes 14.17 Romains 1.28 Esaïe 51.13 Esaïe 44.20 Romains 3.1-3.2
22 Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa;
Psaumes 104.2 Nombres 13.33 Esaïe 42.5 Job 9.8 Psaumes 68.33
23 ndiye awatanguaye wakuu, na kuwabatilisha waamuzi wa dunia.
Job 12.21 Psaumes 107.40 Jérémie 25.18-25.27 Esaïe 24.21-24.22 Psaumes 76.12
24 Naam, hawakupandwa; hawakutiwa katika ardhi kama mbegu; naam, shina lao halikutia mizizi katika ardhi; tena awapuzia tu, wakanyauka, upepo wa kisulisuli wawaondoa kama mabua makavu.
Esaïe 41.16 Esaïe 17.13 Esaïe 14.21-14.22 Job 4.9 Zacharie 9.14
25 Mtanifananisha na nani, basi, nipate kuwa sawa naye? Asema yeye aliye Mtakatifu.
Esaïe 40.18 Deutéronome 4.33 Deutéronome 4.15-4.18 Deutéronome 5.8
26 Inueni macho yenu juu, mkaone; ni nani aliyeziumba hizi; aletaye nje jeshi lao kwa hesabu; aziita zote kwa majina; kwa ukuu wa uweza wake, na kwa kuwa yeye ni hodari kwa nguvu zake; hapana moja isiyokuwapo mahali pake.
Esaïe 51.6 Esaïe 48.13 Colossiens 1.16-1.17 Psaumes 89.11-89.13 Jérémie 32.17-32.19
27 Mbona unasema, Ee Yakobo, mbona unanena, Ee Israeli, Njia yangu imefichwa, Bwana asiione, na hukumu yangu imempita Mungu wangu asiiangalie?
Luc 18.7-18.8 Esaïe 49.4 Job 27.2 Esaïe 49.14
28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.
Psaumes 147.5 Romains 11.33-11.34 Actes 13.47 Jean 5.17 Genèse 21.33
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
Esaïe 41.10 Philippiens 4.13 2 Corinthiens 12.9-12.10 Jérémie 31.25 Psaumes 29.11
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
Esaïe 13.18 Amos 2.14 Psaumes 33.16 Ecclésiaste 9.11 Esaïe 9.17
31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
2 Corinthiens 4.16 Psaumes 103.5 Lamentations 3.25-3.26 2 Corinthiens 12.9-12.10 Psaumes 27.13-27.14

Cette Bible est dans le domaine public.