Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 33.24
Bible en Swahili de l’est


Délivrance de Jérusalem

1 Ole wako uharibuye ila hukuharibiwa, utendaye hila wala hukutendwa hila! Utakapokwisha kuharibu, utaharibiwa wewe; na utakapokwisha kutenda kwa hila, wao watakutenda hila wewe.
Esaïe 21.2 Matthieu 7.2 Jérémie 25.12-25.14 Esaïe 24.16 Esaïe 10.12
2 Ee Bwana, uturehemu; tumekungoja wewe; uwe wewe mkono wetu kila asubuhi,na wokovu wetu pia wakati wa taabu.
Esaïe 25.9 Esaïe 26.8 Esaïe 30.18-30.19 Lamentations 3.23 Psaumes 62.8
3 Kabila za watu wamekimbia wakisikia kelele za fujo; mataifa wametawanyika ulipojiinua nafsi yako.
Esaïe 17.12-17.14 Esaïe 59.16-59.18 Esaïe 10.32-10.34 Esaïe 37.11-37.18 Psaumes 46.6
4 Na mateka yako yatakumbwa kama wadudu wakumbavyo, wataruka juu yake kama arukavyo nzige.
Joël 2.9 Esaïe 33.23 2 Chroniques 20.25 Joël 2.25 2 Chroniques 14.13
5 Bwana ametukuka; kwa maana anakaa juu; amejaza Sayuni hukumu na haki.
Esaïe 2.17 Esaïe 54.11-54.14 Esaïe 4.2-4.4 Esaïe 32.15-32.18 Esaïe 1.26-1.27
6 Nyakati zako zitakuwa nyakati za kukaa imara; za wokovu tele na hekima na maarifa; kumcha Bwana ni hazina yake ya akiba.
Matthieu 6.33 Proverbes 24.3-24.7 Psaumes 112.1-112.3 Psaumes 27.1-27.2 Proverbes 28.15-28.16
7 Angalia, mashujaa wao wanalia nje, wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.
Esaïe 36.22 2 Rois 18.18 Esaïe 36.3 2 Rois 18.37-19.3
8 Njia kuu zimeachwa, msafiri amekoma; ameyavunja maagano, ameidharau miji, hamjali mtu.
Juges 5.6 Esaïe 10.9-10.11 2 Rois 18.13-18.17 1 Samuel 17.26 Esaïe 10.29-10.31
9 Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani.
Esaïe 35.2 Nahum 1.4 Esaïe 65.10 Jérémie 4.20-4.26 Esaïe 24.4-24.6
10 Basi, sasa nitasimama; asema Bwana; sasa nitajiinua, sasa nitajitukuza.
Psaumes 12.5 Sophonie 3.8 Esaïe 59.16-59.17 Esaïe 10.33 Esaïe 10.16
11 Ninyi mtachukua mimba ya makapi, mtazaa majani makavu; pumzi yenu ni moto utakaowateketeza wenyewe.
Psaumes 7.14 Esaïe 59.4 Jacques 1.15 Esaïe 31.8-31.9 Nahum 1.5-1.10
12 Nao mataifa watakuwa kama kuchoma chokaa, kama miiba iliyokatika, iteketezwayo motoni.
Esaïe 27.4 2 Samuel 23.6-23.7 Esaïe 9.18 Amos 2.1 Esaïe 10.17
13 Sikieni, ninyi mlio mbali, niliyoyatenda; na ninyi mlio karibu, kirini uweza wangu.
Psaumes 48.10 Esaïe 49.1 Ephésiens 2.11-2.18 Daniel 6.25-6.27 1 Samuel 17.46
14 Wenye dhambi walio katika Sayuni wanaogopa; tetemeko limewashika wasiomcha Mungu; Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
Hébreux 12.29 Deutéronome 5.24-5.25 Matthieu 18.8 Matthieu 25.41 Apocalypse 14.10
15 Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Psaumes 119.37 2 Pierre 2.14-2.16 Psaumes 106.3 Michée 7.3-7.4 Deutéronome 16.19
16 Huyu ndiye atakayekaa juu; majabali ni ngome yake; atapewa chakula chake; maji yake hayatakoma.
Luc 12.29-12.31 Esaïe 32.18 Psaumes 37.3 Psaumes 34.10 Habakuk 3.19
17 Macho yako yatamwona mfalme katika uzuri wake, yataona nchi iliyoenea sana.
Esaïe 6.5 Psaumes 31.8 2 Corinthiens 4.18 Psaumes 45.2 Jean 14.21
18 Moyo wako utatafakari hofu ile; Yuko wapi yeye aliyehesabu? Yuko wapi yeye aliyeupima ushuru? Yuko wapi yeye aliyeihesabu minara?
2 Rois 18.14 1 Corinthiens 1.20 Psaumes 31.7-31.8 Esaïe 38.9-38.22 Psaumes 71.20
19 Hutawaona watu wale wakali; watu wa maneno magumu usiyoweza kuyafahamu; wenye lugha ya kigeni usiyoweza kuelewa nayo.
Esaïe 28.11 Deutéronome 28.49-28.50 Jérémie 5.15 2 Rois 19.32 Ezéchiel 3.5-3.6
20 Angalia Sayuni, mji wa sikukuu zetu; macho yako yatauona Yerusalemu umekuwa kao la raha; hema isiyotanga-tanga; vigingi vyake havitang’olewa, wala kamba zake hazitakatika.
Psaumes 46.5 Esaïe 32.18 Esaïe 54.2 Ezéchiel 48.35 Deutéronome 12.5
21 Bali huko Bwana atakuwa pamoja nasi, mwenye adhama; mahali penye mito mipana na vijito, pasipopita mashua na makasia yake; wala hapana merikebu ya vita itakayopita hapo.
Psaumes 46.4-46.5 2 Corinthiens 4.4-4.6 Esaïe 66.12 Psaumes 29.3 Actes 7.2
22 Kwa maana Bwana ndiye mwamuzi wetu; Bwana ndiye mfanya sheria wetu; Bwana ndiye mfalme wetu; ndiye atakayetuokoa.
Jacques 4.12 Psaumes 89.18 Esaïe 25.9 Zacharie 9.9 Esaïe 12.2
23 Kamba zako zimelegea; hawakuweza kukaza sana shina la mlingoti wao; hawakuweza kulikunjua tanga; ndipo mapato ya mateka yaligawanywa, hata wachechemeao walipata mateka.
2 Rois 7.8 Psaumes 68.12 1 Corinthiens 1.27 Actes 27.30-27.32 Esaïe 33.1
24 Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.
Jérémie 50.20 Michée 7.18-7.19 1 Jean 1.7-1.9 Esaïe 58.8 Esaïe 44.22

Cette Bible est dans le domaine public.