Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 33.2
Bible en Swahili de l’est


Délivrance de Jérusalem

1 Ole wako uharibuye ila hukuharibiwa, utendaye hila wala hukutendwa hila! Utakapokwisha kuharibu, utaharibiwa wewe; na utakapokwisha kutenda kwa hila, wao watakutenda hila wewe.
Matthieu 7.2 Esaïe 21.2 Jérémie 25.12-25.14 Esaïe 24.16 Esaïe 10.12
2 Ee Bwana, uturehemu; tumekungoja wewe; uwe wewe mkono wetu kila asubuhi,na wokovu wetu pia wakati wa taabu.
Esaïe 25.9 Esaïe 26.8 Esaïe 30.18-30.19 Psaumes 37.39 Lamentations 3.25-3.26
3 Kabila za watu wamekimbia wakisikia kelele za fujo; mataifa wametawanyika ulipojiinua nafsi yako.
Esaïe 17.12-17.14 Esaïe 59.16-59.18 Esaïe 10.32-10.34 Esaïe 37.11-37.18 Psaumes 46.6
4 Na mateka yako yatakumbwa kama wadudu wakumbavyo, wataruka juu yake kama arukavyo nzige.
Joël 2.9 Esaïe 33.23 2 Chroniques 20.25 Joël 2.25 2 Chroniques 14.13
5 Bwana ametukuka; kwa maana anakaa juu; amejaza Sayuni hukumu na haki.
Esaïe 2.17 Ephésiens 1.20-1.21 Job 40.9-40.14 Esaïe 66.1 Esaïe 60.21
6 Nyakati zako zitakuwa nyakati za kukaa imara; za wokovu tele na hekima na maarifa; kumcha Bwana ni hazina yake ya akiba.
Matthieu 6.33 Proverbes 24.3-24.7 Psaumes 112.1-112.3 1 Timothée 4.8 Esaïe 38.5-38.6
7 Angalia, mashujaa wao wanalia nje, wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.
Esaïe 36.22 2 Rois 18.18 Esaïe 36.3 2 Rois 18.37-19.3
8 Njia kuu zimeachwa, msafiri amekoma; ameyavunja maagano, ameidharau miji, hamjali mtu.
Juges 5.6 2 Rois 18.20-18.21 Lamentations 1.4 Psaumes 10.5 Esaïe 10.9-10.11
9 Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani.
Esaïe 35.2 Nahum 1.4 Esaïe 65.10 Deutéronome 3.4 Esaïe 37.24
10 Basi, sasa nitasimama; asema Bwana; sasa nitajiinua, sasa nitajitukuza.
Psaumes 12.5 Esaïe 30.17-30.18 Deutéronome 32.36-32.43 Psaumes 78.65 Sophonie 3.8
11 Ninyi mtachukua mimba ya makapi, mtazaa majani makavu; pumzi yenu ni moto utakaowateketeza wenyewe.
Psaumes 7.14 Esaïe 59.4 Jacques 1.15 Esaïe 37.23-37.29 Actes 5.4
12 Nao mataifa watakuwa kama kuchoma chokaa, kama miiba iliyokatika, iteketezwayo motoni.
Esaïe 27.4 2 Samuel 23.6-23.7 Esaïe 9.18 Amos 2.1 Esaïe 10.17
13 Sikieni, ninyi mlio mbali, niliyoyatenda; na ninyi mlio karibu, kirini uweza wangu.
Psaumes 48.10 Esaïe 49.1 Ephésiens 2.11-2.18 Josué 2.9-2.11 Psaumes 147.12-147.14
14 Wenye dhambi walio katika Sayuni wanaogopa; tetemeko limewashika wasiomcha Mungu; Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
Hébreux 12.29 Esaïe 66.24 Deutéronome 5.24-5.25 Matthieu 18.8 Matthieu 25.41
15 Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Psaumes 119.37 2 Pierre 2.14-2.16 Tite 2.11-2.12 1 Samuel 12.3 Exode 23.6-23.9
16 Huyu ndiye atakayekaa juu; majabali ni ngome yake; atapewa chakula chake; maji yake hayatakoma.
Luc 12.29-12.31 Esaïe 32.18 Psaumes 91.14 Psaumes 18.33 Psaumes 107.41
17 Macho yako yatamwona mfalme katika uzuri wake, yataona nchi iliyoenea sana.
Esaïe 6.5 Jean 17.24 Zacharie 9.17 Matthieu 17.2 Psaumes 31.8
18 Moyo wako utatafakari hofu ile; Yuko wapi yeye aliyehesabu? Yuko wapi yeye aliyeupima ushuru? Yuko wapi yeye aliyeihesabu minara?
2 Rois 18.14 1 Corinthiens 1.20 Esaïe 17.14 Genèse 23.16 Psaumes 31.22
19 Hutawaona watu wale wakali; watu wa maneno magumu usiyoweza kuyafahamu; wenye lugha ya kigeni usiyoweza kuelewa nayo.
Esaïe 28.11 Deutéronome 28.49-28.50 Jérémie 5.15 2 Rois 19.32 Ezéchiel 3.5-3.6
20 Angalia Sayuni, mji wa sikukuu zetu; macho yako yatauona Yerusalemu umekuwa kao la raha; hema isiyotanga-tanga; vigingi vyake havitang’olewa, wala kamba zake hazitakatika.
Psaumes 46.5 Esaïe 32.18 Esaïe 54.2 Psaumes 78.68-78.69 Psaumes 128.5
21 Bali huko Bwana atakuwa pamoja nasi, mwenye adhama; mahali penye mito mipana na vijito, pasipopita mashua na makasia yake; wala hapana merikebu ya vita itakayopita hapo.
Psaumes 46.4-46.5 2 Corinthiens 4.4-4.6 Esaïe 66.12 Psaumes 29.3 Actes 7.2
22 Kwa maana Bwana ndiye mwamuzi wetu; Bwana ndiye mfanya sheria wetu; Bwana ndiye mfalme wetu; ndiye atakayetuokoa.
Jacques 4.12 Esaïe 25.9 Psaumes 89.18 Zacharie 9.9 Esaïe 12.2
23 Kamba zako zimelegea; hawakuweza kukaza sana shina la mlingoti wao; hawakuweza kulikunjua tanga; ndipo mapato ya mateka yaligawanywa, hata wachechemeao walipata mateka.
2 Rois 7.8 Psaumes 68.12 1 Corinthiens 1.27 1 Samuel 30.22-30.24 2 Chroniques 20.25
24 Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.
Jérémie 50.20 Michée 7.18-7.19 1 Jean 1.7-1.9 Esaïe 58.8 Esaïe 44.22

Cette Bible est dans le domaine public.