Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 33.16
Bible en Swahili de l’est


Délivrance de Jérusalem

1 Ole wako uharibuye ila hukuharibiwa, utendaye hila wala hukutendwa hila! Utakapokwisha kuharibu, utaharibiwa wewe; na utakapokwisha kutenda kwa hila, wao watakutenda hila wewe.
Esaïe 21.2 Matthieu 7.2 Esaïe 10.12 Esaïe 17.14 Jérémie 25.12-25.14
2 Ee Bwana, uturehemu; tumekungoja wewe; uwe wewe mkono wetu kila asubuhi,na wokovu wetu pia wakati wa taabu.
Esaïe 25.9 Esaïe 26.8 Esaïe 30.18-30.19 Psaumes 130.4-130.8 2 Corinthiens 1.3-1.4
3 Kabila za watu wamekimbia wakisikia kelele za fujo; mataifa wametawanyika ulipojiinua nafsi yako.
Esaïe 59.16-59.18 Esaïe 10.32-10.34 Esaïe 37.11-37.18 Psaumes 46.6 Esaïe 10.13-10.14
4 Na mateka yako yatakumbwa kama wadudu wakumbavyo, wataruka juu yake kama arukavyo nzige.
Esaïe 33.23 2 Chroniques 20.25 Joël 2.25 2 Chroniques 14.13 2 Rois 7.15-7.16
5 Bwana ametukuka; kwa maana anakaa juu; amejaza Sayuni hukumu na haki.
Esaïe 2.17 Romains 3.26 Exode 15.6 Esaïe 37.20 Psaumes 123.1
6 Nyakati zako zitakuwa nyakati za kukaa imara; za wokovu tele na hekima na maarifa; kumcha Bwana ni hazina yake ya akiba.
Matthieu 6.33 Psaumes 112.1-112.3 Proverbes 24.3-24.7 Ecclésiaste 9.14-9.18 2 Corinthiens 6.10
7 Angalia, mashujaa wao wanalia nje, wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.
2 Rois 18.18 Esaïe 36.22 Esaïe 36.3 2 Rois 18.37-19.3
8 Njia kuu zimeachwa, msafiri amekoma; ameyavunja maagano, ameidharau miji, hamjali mtu.
Juges 5.6 1 Samuel 17.10 Luc 18.2-18.4 Esaïe 36.1 Esaïe 10.13-10.14
9 Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani.
Esaïe 35.2 Nahum 1.4 Esaïe 65.10 Esaïe 24.1 Esaïe 14.8
10 Basi, sasa nitasimama; asema Bwana; sasa nitajiinua, sasa nitajitukuza.
Psaumes 12.5 Exode 15.9-15.12 Amos 6.1 Exode 14.18 Psaumes 46.10
11 Ninyi mtachukua mimba ya makapi, mtazaa majani makavu; pumzi yenu ni moto utakaowateketeza wenyewe.
Esaïe 59.4 Psaumes 7.14 Jacques 1.15 Esaïe 26.18 Esaïe 8.9-8.10
12 Nao mataifa watakuwa kama kuchoma chokaa, kama miiba iliyokatika, iteketezwayo motoni.
Esaïe 27.4 2 Samuel 23.6-23.7 Amos 2.1 Esaïe 10.17 Esaïe 37.36
13 Sikieni, ninyi mlio mbali, niliyoyatenda; na ninyi mlio karibu, kirini uweza wangu.
Psaumes 48.10 Esaïe 49.1 Ephésiens 2.11-2.18 Psaumes 98.1-98.2 Exode 15.14
14 Wenye dhambi walio katika Sayuni wanaogopa; tetemeko limewashika wasiomcha Mungu; Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
Hébreux 12.29 Matthieu 25.41 Apocalypse 14.10 Matthieu 25.46 Esaïe 66.24
15 Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Psaumes 119.37 2 Pierre 2.14-2.16 Luc 1.6 Malachie 2.6 Jérémie 5.26-5.28
16 Huyu ndiye atakayekaa juu; majabali ni ngome yake; atapewa chakula chake; maji yake hayatakoma.
Esaïe 32.18 Luc 12.29-12.31 Psaumes 90.1 Esaïe 25.4 Esaïe 26.1-26.5
17 Macho yako yatamwona mfalme katika uzuri wake, yataona nchi iliyoenea sana.
Esaïe 6.5 Esaïe 32.1-32.2 Esaïe 26.15 Cantique 5.10 Esaïe 37.1
18 Moyo wako utatafakari hofu ile; Yuko wapi yeye aliyehesabu? Yuko wapi yeye aliyeupima ushuru? Yuko wapi yeye aliyeihesabu minara?
1 Corinthiens 1.20 2 Rois 18.14 2 Rois 15.19 2 Timothée 3.11 2 Corinthiens 1.8-1.10
19 Hutawaona watu wale wakali; watu wa maneno magumu usiyoweza kuyafahamu; wenye lugha ya kigeni usiyoweza kuelewa nayo.
Esaïe 28.11 Deutéronome 28.49-28.50 Jérémie 5.15 2 Rois 19.32 Ezéchiel 3.5-3.6
20 Angalia Sayuni, mji wa sikukuu zetu; macho yako yatauona Yerusalemu umekuwa kao la raha; hema isiyotanga-tanga; vigingi vyake havitang’olewa, wala kamba zake hazitakatika.
Psaumes 46.5 Esaïe 32.18 Esaïe 54.2 Psaumes 125.1-125.2 Esaïe 37.33
21 Bali huko Bwana atakuwa pamoja nasi, mwenye adhama; mahali penye mito mipana na vijito, pasipopita mashua na makasia yake; wala hapana merikebu ya vita itakayopita hapo.
Psaumes 46.4-46.5 Esaïe 66.12 Psaumes 29.3 Actes 7.2 Esaïe 41.18
22 Kwa maana Bwana ndiye mwamuzi wetu; Bwana ndiye mfanya sheria wetu; Bwana ndiye mfalme wetu; ndiye atakayetuokoa.
Jacques 4.12 Psaumes 89.18 Esaïe 25.9 Esaïe 12.2 Zacharie 9.9
23 Kamba zako zimelegea; hawakuweza kukaza sana shina la mlingoti wao; hawakuweza kulikunjua tanga; ndipo mapato ya mateka yaligawanywa, hata wachechemeao walipata mateka.
2 Rois 7.8 1 Corinthiens 1.27 Psaumes 68.12 1 Samuel 30.10 2 Rois 7.16
24 Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.
Jérémie 50.20 1 Jean 1.7-1.9 Michée 7.18-7.19 Esaïe 44.22 Esaïe 58.8

Cette Bible est dans le domaine public.