Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 24.1
Bible en Swahili de l’est


Les bouleversements à venir

Jugement universel

1 Tazama, Bwana ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa, aipindua, na kuwatawanya wakaao ndani yake.
Esaïe 42.15 Nahum 2.10 Ezéchiel 6.6 Esaïe 1.7-1.9 Néhémie 1.8
2 Na itakuwa kama ilivyo hali ya watu, ndivyo itakavyokuwa hali ya kuhani; kama ilivyo hali ya mtumwa, ndivyo itakavyokuwa hali ya bwana wake; kama ilivyo hali ya mjakazi, ndivyo itakavyokuwa hali ya bibi yake; kama ilivyo hali yake anunuaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake auzaye; kama ilivyo hali yake akopeshaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake akopaye; kama ilivyo hali yake atwaaye faida, ndivyo itakavyokuwa hali yake ampaye faida.
Osée 4.9 Ezéchiel 7.12-7.13 Jérémie 5.3-5.6 Ezéchiel 14.8-14.10 Lamentations 4.13
3 Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.
Esaïe 24.1 Esaïe 6.11 Lévitique 26.30-26.35 Ezéchiel 36.4 Esaïe 22.25
4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.
Esaïe 33.9 Osée 4.3 Esaïe 28.1 Jérémie 4.28 Esaïe 64.6
5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.
Romains 8.20-8.21 Nombres 35.33-35.34 Daniel 7.25 Deutéronome 32.20 Jérémie 3.1-3.2
6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu.
Zacharie 5.3-5.4 Malachie 4.1 Deutéronome 30.18-30.19 2 Pierre 3.10 Lévitique 26.22
7 Divai mpya inaomboleza, mzabibu umedhoofika, watu wote waliochangamka moyo wanaugua.
Esaïe 16.10 Esaïe 16.8 Joël 1.10-1.12 Osée 9.1-9.2 Esaïe 32.9-32.13
8 Sauti ya furaha ya matoazi inakoma; kelele yao wafurahio imekwisha; furaha ya kinubi inakoma.
Osée 2.11 Ezéchiel 26.13 Apocalypse 18.22 Jérémie 7.34 Jérémie 16.9
9 Hawatakunywa divai pamoja na nyimbo; kileo kitakuwa uchungu kwao wakinywao.
Ecclésiaste 9.7 Esaïe 5.22 Psaumes 69.12 Amos 8.3 Esaïe 5.11-5.12
10 Mji wa machafuko umebomolewa; kila nyumba imefungwa, asipate kuingia mtu awaye yote.
Jérémie 39.4 Esaïe 32.14 Jérémie 9.25-9.26 Michée 2.13 Matthieu 23.34-23.35
11 Pana kilio katika njia kuu kwa sababu ya divai; furaha yote imetiwa giza, na changamko la nchi limetoweka.
Esaïe 8.22 Jérémie 48.33 Esaïe 32.13 Luc 16.25 Esaïe 16.10
12 Ndani ya mji umebaki ukiwa, na lango lake limepigwa kwa uharibifu.
Lamentations 2.9 Lamentations 1.1 Esaïe 32.14 Michée 1.9 Lamentations 1.4
13 Maana katikati ya dunia, katikati ya mataifa, itakuwa hivi; kama wakati utikiswapo mzeituni, kama wakati waokotapo zabibu baada ya mavuno yake.
Esaïe 1.9 Esaïe 17.5-17.6 Ezéchiel 11.16-11.20 Romains 11.2-11.6 Ezéchiel 7.16
14 Hawa watainua sauti zao, watapiga kelele; kwa sababu ya utukufu wa Bwana watapiga kelele toka baharini.
Esaïe 54.1 Esaïe 12.1-12.6 Esaïe 35.2 Esaïe 51.11 Esaïe 25.1
15 Basi, mtukuzeni Bwana katika mashariki, litukuzeni jina la Bwana, Mungu wa Israeli, katika visiwa vya bahari.
Malachie 1.11 Esaïe 42.4 Esaïe 49.1 Esaïe 60.9 Esaïe 51.5
16 Toka pande za mwisho wa dunia tumesikia nyimbo, Atukuzwe mwenye haki. Ndipo niliposema, Kukonda kwangu! Kukonda kwangu! Ole wangu! Watenda hila wametenda hila, naam, watendao hila wametenda hila sana.
Esaïe 21.2 Jérémie 5.11 Esaïe 33.1 Jérémie 3.20 Marc 13.27
17 Hofu, na shimo, na mtego, vi juu yako, Ee mwenye kukaa duniani.
Jérémie 48.43-48.44 Lévitique 26.21-26.22 1 Rois 19.17 Amos 5.19 Jérémie 8.3
18 Itakuwa kila akimbiaye sauti ya hofu ataanguka katika shimo; na kila apandaye na kutoka shimoni atanaswa na mtego; kwa maana madirisha yaliyo juu yamewekwa wazi, na misingi ya dunia inatikisika.
Psaumes 18.7 Genèse 7.11 Psaumes 46.2-46.3 Job 18.8-18.16 Genèse 19.24
19 Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana.
Apocalypse 20.11 Nahum 1.5 Habakuk 3.6 Matthieu 24.3 Deutéronome 11.6
20 Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka, wala haitainuka tena.
Esaïe 19.14 Esaïe 29.9 Amos 8.14 Daniel 11.19 Esaïe 43.27
21 Tena itakuwa katika siku hiyo, Bwana ataliadhibu jeshi la mahali palipo juu katika mahali palipo juu, na wafalme wa dunia katika dunia;
Psaumes 76.12 Esaïe 10.12 Apocalypse 19.18-19.21 Esaïe 25.10-25.12 Joël 3.19
22 nao watakusanywa pamoja kama vile wakusanywavyo wafungwa katika shimo nao watafungwa katika gereza; na baada ya muda wa siku nyingi watajiliwa.
Zacharie 9.11 Esaïe 42.22 Jérémie 38.6-38.13 Esaïe 2.19 Esaïe 24.17
23 Ndipo mwezi utatahayari, na jua litaona haya; kwa kuwa Bwana wa majeshi atatawala katika mlima wa Sayuni, na katika Yerusalemu, na mbele ya wazee wake kwa utukufu.
Esaïe 13.10 Hébreux 12.22 Esaïe 60.19 Michée 4.7 Apocalypse 21.23

Cette Bible est dans le domaine public.