Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 17.10
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur la Syrie

1 Ufunuo juu ya Dameski. Tazama, Dameski umeondolewa usiwe mji, nao utakuwa chungu ya magofu.
Zacharie 9.1 Amos 1.3-1.5 Esaïe 25.2 Jérémie 49.2 Genèse 14.15
2 Miji ya Aroeri imeachwa; itakuwa kwa makundi ya kondoo, nao watajilaza huko wala hapana atakayewatia hofu.
Ezéchiel 25.5 Michée 4.4 Nombres 32.34 Deutéronome 2.36 Jérémie 7.33
3 Na ngome ya Efraimu itakomeshwa, na ufalme wa Dameski, na mabaki ya Shamu; watakuwa kama utukufu wa wana wa Israeli, asema Bwana wa majeshi.
Esaïe 7.16 Esaïe 8.4 Osée 9.11 Esaïe 7.8 Esaïe 28.1-28.4
4 Tena itakuwa katika siku hiyo, utukufu wa Yakobo utapungua-pungua, na kunona kwa mwili wake kutakonda.
Esaïe 10.16 Esaïe 10.4 Sophonie 2.11 Ezéchiel 34.20 Esaïe 24.13
5 Tena itakuwa kama hapo avunaye ashikapo mabua ya ngano, na mkono wake ukatapo masuke; tena itakuwa kama hapo mtu aokotapo masuke katika bonde la Warefai.
Jérémie 51.33 Joël 3.13 2 Samuel 5.18 Matthieu 13.30 2 Samuel 5.22
6 Lakini kilichosazwa na mvunaji kitakuwa ndani yake, kama vile wakati wa kupiga mizeituni, matunda mawili matatu yaliyo juu sana; matunda manne matano katika matawi, matawi ya mti wa matunda, asema Bwana, Mungu wa Israeli.
Esaïe 24.13 Deutéronome 4.27 Abdias 1.5 Esaïe 27.12 Ezéchiel 39.29
7 Katika siku hiyo mwanadamu atamwangalia Muumba wake, na macho yake yatamtazama Mtakatifu wa Israeli.
Michée 7.7 Osée 6.1 Osée 3.5 Esaïe 10.20-10.21 Jérémie 3.12-3.14
8 Wala hataziangalia madhabahu, kazi ya mikono yake; wala hatavitazama vilivyofanyika kwa vidole vyake, maashera na sanamu za jua.
Esaïe 30.22 Esaïe 27.9 Michée 5.13-5.14 Esaïe 2.8 Esaïe 44.19-44.20
9 Katika siku hiyo miji yake yenye maboma itakuwa kama mahali palipoachwa ndani ya mwitu, na juu ya kilele cha mlima, palipoachwa mbele ya wana wa Israeli; napo patakuwa ganjo.
Esaïe 27.10 Amos 7.9 Esaïe 17.4-17.5 Michée 5.11 Osée 13.15-13.16
10 Maana umemsahau Mungu wa wokovu wako, wala hukuukumbuka mwamba wa ngome yako; kwa sababu hiyo ulipanda mashamba yapendezayo, na kutia ndani yake mizabibu migeni.
Esaïe 51.13 Esaïe 12.2 Esaïe 26.4 Deutéronome 32.4 Psaumes 106.21
11 Katika siku ile ulipopanda, ulifanya kitalu, na wakati wa asubuhi ulizimeesha mbegu zako, lakini mavuno yatatoweka siku ya huzuni, na ya sikitiko la moyo lifishalo.
Job 4.8 Osée 8.7 Romains 2.5 Matthieu 8.11-8.12 Joël 1.5-1.12
12 Aha! Uvumi wa watu wengi! Wanavuma kama uvumi wa bahari; Aha! Ngurumo ya mataifa! Wananguruma kama ngurumo ya maji mengi;
Psaumes 18.4 Jérémie 6.23 Luc 21.25 Ezéchiel 43.2 Psaumes 46.1-46.3
13 Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani.
Psaumes 9.5 Esaïe 41.15-41.16 Job 21.18 Psaumes 1.4 Esaïe 29.5
14 Wakati wa jioni, tazama, kuna hofu; Na kabla ya mapambazuko hawako; Hilo ndilo fungu lao watutekao, Na ajali yao wanaotunyang’anya mali zetu.
2 Rois 19.35 Job 20.29 Esaïe 10.28-10.32 Jérémie 13.25 Proverbes 22.23

Cette Bible est dans le domaine public.