Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 13.10
Bible en Swahili de l’est


Prophéties sur les nations étrangères

Prophétie sur Babylone

1 Ufunuo juu ya Babeli; maono aliyoyaona Isaya, mwana wa Amozi.
Esaïe 1.1 Esaïe 14.28 Esaïe 47.1-47.15 Esaïe 15.1 Ezéchiel 12.10
2 Haya! Juu ya mlima usio na miti inueni bendera, wapazieni sauti zenu, wapungieni mkono, kwamba waingie katika malango ya wakuu.
Esaïe 5.26 Jérémie 51.58 Jérémie 50.2 Esaïe 45.1-45.3 Jérémie 51.25
3 Mimi mwenyewe nimewaamuru watu wangu waliowekwa wakfu kwangu, naam, nimewaita watu wangu walio hodari kwa ajili ya hasira yangu, watu wangu wenye kutakabari.
Joël 3.11 Psaumes 149.2 Esaïe 44.27-44.28 Esaïe 23.11 Psaumes 149.5-149.9
4 Kelele milimani kama kelele za watu wengi sana; kelele za falme za mataifa waliokutana pamoja; Bwana wa majeshi anapanga jeshi kwa vita;
Joël 3.14 Joël 2.1-2.11 Apocalypse 18.8 Jérémie 50.14-50.15 Esaïe 22.1-22.9
5 watu waliotoka katika nchi iliyo mbali, tokea upande wa mwisho wa mbingu; naam, Bwana na silaha za ghadhabu yake, ili aiangamize nchi yote.
Jérémie 50.3 Jérémie 51.20-51.46 Jérémie 51.11 Jérémie 50.9 Esaïe 5.26
6 Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu.
Joël 1.15 Esaïe 2.12 Amos 5.18 Ezéchiel 30.2-30.3 Esaïe 34.8
7 Kwa sababu hiyo mikono yote italegea, na moyo wa kila mtu utayeyuka.
Ezéchiel 21.7 Nahum 2.10 Ezéchiel 7.17 Esaïe 19.1 Esaïe 51.20
8 Nao watafadhaika; watashikwa na utungu na maumivu; watakuwa na utungu kama mwanamke aliye karibu na kuzaa; watakodoleana macho; nyuso zao zitakuwa ni nyuso za moto.
Nahum 2.10 Esaïe 26.17 Esaïe 21.3-21.4 Joël 2.6 Jérémie 4.31
9 Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.
Esaïe 13.15-13.18 Psaumes 104.35 Jérémie 6.22-6.23 Esaïe 13.6 Esaïe 47.10-47.15
10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.
Matthieu 24.29 Marc 13.24 Luc 21.25 Apocalypse 6.12-6.14 Esaïe 5.30
11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;
Daniel 5.22-5.23 Esaïe 2.11 Esaïe 14.12-14.16 Esaïe 26.21 Apocalypse 18.2-18.3
12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri.
Esaïe 4.1 Esaïe 24.6 Psaumes 137.9 Esaïe 13.15-13.18 Job 28.16
13 Kwa hiyo nitazitetemesha mbingu, na dunia itatikiswa itoke katika mahali pake, kwa sababu ya ghadhabu ya Bwana wa majeshi, na kwa sababu ya siku ya hasira yake kali.
Joël 3.16 Lamentations 1.12 Matthieu 24.35 Esaïe 34.4 Esaïe 51.6
14 Basi, itakuwa kama vile paa aliyetishwa, na kama kondoo wasio na mtu wa kuwakusanya; kila mtu atageukia watu wake; nao watakimbia, kila mtu aende nchi yake mwenyewe.
1 Rois 22.17 Jérémie 50.16 Jérémie 51.9 1 Rois 22.36 Esaïe 17.13
15 Kila mtu atakayeonekana atatumbuliwa, na kila mtu atakayepatikana ataanguka kwa upanga.
Esaïe 47.9-47.14 Jérémie 50.35-50.42 Esaïe 14.19-14.22 Jérémie 50.25 Jérémie 51.3-51.4
16 Na watoto wao wachanga watavunjwa-vunjwa mbele ya macho yao, nyumba zao zitatekwa nyara, na wake zao watatendwa jeuri.
Nahum 3.10 Osée 10.14 Psaumes 137.8-137.9 Esaïe 13.18 Lamentations 5.11
17 Tazama, nitawaamsha Wamedi juu yao, ambao hawaoni fedha kuwa kitu, wala hawafurahii dhahabu.
Proverbes 6.34-6.35 Jérémie 51.11 Esaïe 21.2 Esaïe 41.25 Jérémie 51.27-51.28
18 Na nyuta zao zitawaangusha vijana; wala hawatahurumia mazao ya tumbo; jicho lao halitawahurumia watoto.
2 Rois 8.12 Ezéchiel 9.10 2 Chroniques 36.17 Esaïe 13.16 Osée 13.16
19 Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.
Genèse 19.24 Daniel 4.30 Deutéronome 29.23 Jérémie 49.18 Jérémie 50.40
20 Hautakaliwa na watu tena kabisa, wala watu hawatakaa ndani yake tangu kizazi hata kizazi. Mwarabu hatapiga hema yake huko, wala wachungaji hawatalaza makundi yao huko.
Esaïe 14.23 Jérémie 51.43 Jérémie 51.62-51.64 Jérémie 51.29 Apocalypse 18.21-18.23
21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko.
Apocalypse 18.2 Esaïe 34.11-34.15
22 Na mbwa-mwitu watalia ndani ya ngome zake; na mbweha ndani ya majumba ya anasa; na wakati wake u karibu kufika, na siku zake hazitaongezeka.
Jérémie 51.33 Esaïe 35.7 Esaïe 25.2 2 Pierre 2.3 Habakuk 2.3

Cette Bible est dans le domaine public.