Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 4.9
Bible en Swahili de l’est


L’oppression et la solitude

1 Kisha nikarudi na kuona madhalimu yote yanayotendeka chini ya jua; na tazama, machozi yao waliodhulumiwa, ambao walikuwa hawana mfariji; na upande wa wale waliowadhulumu kulikuwa na uwezo, walakini wale walikuwa hawana mfariji.
Ecclésiaste 3.16 Ecclésiaste 5.8 Lamentations 1.2 Lamentations 1.9 Esaïe 5.7
2 Kwa hiyo nikawasifu wafu waliokwisha kufa kuliko wenye uhai walio hai bado;
Ecclésiaste 2.17 Job 3.11-3.26 Ecclésiaste 9.4-9.6
3 naam, zaidi ya hao wote nikamwita heri yeye asiyekuwako bado, ambaye hakuyaona mabaya yanayotendeka chini ya jua.
Luc 23.29 Ecclésiaste 1.14 Jérémie 20.17-20.18 Jérémie 9.2-9.3 Matthieu 24.19
4 Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo.
Ecclésiaste 1.14 Ecclésiaste 2.21 Ecclésiaste 6.9 Ecclésiaste 6.11 1 Samuel 18.8-18.9
5 Mpumbavu huikunja mikono yake, Naye hula chakula chake mwenyewe;
Esaïe 9.20 Proverbes 6.10-6.11 Proverbes 11.17 Proverbes 13.4 Proverbes 12.27
6 Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo.
Proverbes 16.8 Proverbes 15.16-15.17 Psaumes 37.16 Proverbes 17.1
7 Kisha nikarudi tena, na kuona ubatili chini ya jua.
Ecclésiaste 4.1 Zacharie 1.6 Psaumes 78.33
8 Kuna mtu aliye peke yake, wala hana wa pili wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema? Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa.
Proverbes 27.20 Ecclésiaste 1.8 Ecclésiaste 1.13 Genèse 2.18 Psaumes 39.6
9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
Genèse 2.18 1 Corinthiens 12.18-12.21 Proverbes 27.17 Nombres 11.14 Actes 15.39-15.40
10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
1 Thessaloniciens 5.11 Galates 6.1 1 Thessaloniciens 4.18 Exode 32.2-32.4 1 Samuel 23.16
11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?
1 Rois 1.1-1.4
12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.
Ephésiens 4.3 Daniel 3.16-3.17
13 Heri kijana maskini mwenye hekima Kuliko mfalme mzee mpumbavu.
Ecclésiaste 9.15-9.16 1 Rois 22.8 2 Chroniques 16.9-16.10 Proverbes 28.6 Proverbes 19.1
14 Kwa maana kutoka gerezani alikuja kumiliki; naam, hata katika ufalme wake alizaliwa hali ya umaskini.
Genèse 41.14 2 Rois 23.31-23.34 Daniel 4.31 2 Rois 24.1-24.2 2 Rois 24.12
15 Nikawaona wote walio hai waendao chini ya jua, ya kwamba walishikamana na huyo kijana, huyo wa pili aliyesimama badala ya yule.
2 Samuel 15.6
16 Hawakuwa na kikomo hao watu wote, hao wote ambao alikuwa juu yao; lakini hata hivyo wale wafuatao baada yake hawatamfurahia. Hakika hayo pia ni ubatili, na kujilisha upepo.
Ecclésiaste 1.14 Ecclésiaste 2.26 2 Samuel 15.12-15.13 1 Rois 1.40 2 Samuel 18.7-18.8

Cette Bible est dans le domaine public.