Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 31.15
Bible en Swahili de l’est


Des artisans qualifiés par l’Esprit

1 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda;
Exode 36.1 Exode 35.30 1 Chroniques 2.19-2.20 Marc 3.16-3.19 Exode 37.1
3 nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
Exode 35.31 1 Rois 7.14 Esaïe 28.6 1 Corinthiens 12.4-12.11 Esaïe 28.26
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
Exode 26.1 2 Chroniques 2.7 1 Rois 7.14 Exode 25.32-25.35 2 Chroniques 2.13-2.14
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
Exode 28.9-28.21
6 Tena, tazama, nimemchagua, awe pamoja naye, huyo Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani; nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza;
Exode 35.10 Exode 28.3 Exode 35.34-36.1 Jacques 1.16-1.17 Ezéchiel 43.1-43.27
7 yaani, hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
Exode 36.8-37.9 Exode 27.9-27.19 Exode 25.10-25.22 Exode 26.1-26.37
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote, na madhabahu ya kufukizia uvumba;
Exode 37.10-37.28 Exode 30.1-30.10 Exode 25.23-25.40
9 na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake;
Exode 38.1-38.8 Exode 30.18-30.21 Exode 27.1-27.8 Exode 40.11
10 na mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani;
Lévitique 8.7-8.8 Exode 28.1-28.43 Lévitique 8.13 Exode 39.1-39.43 Nombres 4.5-4.14
11 na mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
Exode 37.29 Exode 30.23-30.38

Rappel du sabbat

12 Bwana akasema na Musa, na kumwambia,
13 Kisha, nena wewe na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi.
Ezéchiel 20.20 Ezéchiel 20.12 Lévitique 19.3 Exode 31.17 Lévitique 19.30
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
Exode 35.2-35.3 Nombres 15.32-15.36 Exode 20.8 Deutéronome 5.12-5.15 Néhémie 9.14
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa Bwana; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
Exode 16.23 Lévitique 23.3 Genèse 2.2 Exode 34.21 Ezéchiel 46.1
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato, kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
Genèse 17.11 Jérémie 50.5 Genèse 9.13
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Bwana alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
Genèse 1.31 Exode 31.13 Genèse 2.2-2.3 Hébreux 4.10 Ezéchiel 20.12
18 Hapo Bwana alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa chanda cha Mungu.
Deutéronome 4.13 Exode 24.12 Deutéronome 5.22 Exode 32.15-32.16 2 Corinthiens 3.3

Cette Bible est dans le domaine public.