Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 94
Bible en Swahili de l’est


Jugement des méchants

1 Ee Bwana, Mungu wa kisasi, Mungu wa kisasi, uangaze,
Nahum 1.2 Deutéronome 32.35 Esaïe 35.4 Romains 12.19 Psaumes 80.1
2 Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze, Uwape wenye kiburi stahili zao.
Psaumes 7.6 Psaumes 31.23 Genèse 18.25 Esaïe 37.23 Esaïe 37.29
3 Bwana, hata lini wasio haki, Hata lini wasio haki watashangilia?
Job 20.5 Apocalypse 6.10 Esther 6.6-6.10 Psaumes 89.46 Psaumes 80.4
4 Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?
Psaumes 31.18 Psaumes 52.1 Daniel 7.8 Jude 1.14-1.15 Psaumes 64.3-64.4
5 Ee Bwana, wanawaseta watu wako; Wanautesa urithi wako;
Esaïe 3.15 Exode 2.23-2.24 Apocalypse 11.3 Psaumes 14.4 Psaumes 79.7
6 Wanamwua mjane na mgeni; Wanawafisha yatima.
Esaïe 10.2 Jérémie 7.6 Ezéchiel 22.7 Jérémie 22.3 Malachie 3.5
7 Nao husema, Bwana haoni; Mungu wa Yakobo hafikiri.
Ezéchiel 9.9 Luc 18.3-18.4 Ezéchiel 8.12 Esaïe 29.15 Sophonie 1.12
8 Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?
Psaumes 92.6 Psaumes 49.10 Jérémie 10.8 Psaumes 73.22 Deutéronome 32.29
9 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione?
Exode 4.11 Proverbes 20.12 Jérémie 23.23-23.24 Psaumes 139.1-139.12 Proverbes 20.1
10 Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue?
Job 35.11 Esaïe 28.26 Psaumes 44.2 Esaïe 10.5-10.6 Psaumes 119.66
11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.
1 Corinthiens 3.20 Psaumes 49.10-49.13 Job 11.11-11.12 1 Corinthiens 1.25 1 Corinthiens 1.19
12 Ee Bwana, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;
Proverbes 3.11-3.12 Job 5.17 Psaumes 119.71 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.5-12.11
13 Upate kumstarehesha siku za mabaya, Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo.
Psaumes 55.23 Psaumes 9.15 2 Pierre 2.9 Habakuk 3.16 Apocalypse 14.13
14 Kwa kuwa Bwana hatawatupa watu wake, Wala hutauacha urithi wake,
1 Samuel 12.22 Romains 11.1-11.2 Psaumes 37.28 Deutéronome 32.9 Ephésiens 1.18
15 Maana hukumu itairejea haki, Na wote walio wanyofu wa moyo wataifuata.
Michée 7.9 Psaumes 58.11 Psaumes 94.2-94.3 Deutéronome 32.35-32.36 Apocalypse 15.3-15.4
16 Ni nani atakayesimama Kwa ajili yangu juu ya wabaya? Ni nani atakayenisaidia Juu yao wafanyao maovu?
Néhémie 5.7 Psaumes 59.2 Exode 32.26-32.29 Jérémie 26.16-26.19 Ezéchiel 22.30
17 Kama Bwana asingalikuwa msaada wangu, Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya.
Psaumes 124.1-124.2 Psaumes 31.17 Psaumes 13.3 Psaumes 118.13 Psaumes 142.4-142.5
18 Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee Bwana, fadhili zako zilinitegemeza.
Psaumes 38.16 Psaumes 121.3 Psaumes 37.23-37.24 Psaumes 119.116-119.117 Esaïe 41.10
19 Katika wingi wa mawazo ya moyoni mwangu, Faraja zako zaifurahisha roho yangu.
Habakuk 3.16-3.18 Psaumes 77.2-77.10 Psaumes 61.2 Psaumes 43.2-43.5 2 Corinthiens 1.4-1.5
20 Je! Kiti cha udhalimu kishirikiane nawe, Kitungacho madhara kwa njia ya sheria?
Psaumes 58.2 Amos 6.3 Esaïe 10.1 Ecclésiaste 3.16 Esther 3.6-3.12
21 Huishambulia nafsi yake mwenye haki, Na kuihukumu damu isiyo na hatia.
Proverbes 17.15 Matthieu 27.1 Exode 23.7 Psaumes 59.3 Psaumes 56.6
22 Lakini Bwana amekuwa ngome kwangu, Na Mungu wangu mwamba wangu wa kukimbilia.
Psaumes 18.2 Psaumes 59.9 Psaumes 62.2 Esaïe 33.16 Psaumes 27.1-27.3
23 Naye atawarudishia uovu wao, Atawaangamiza katika ubaya wao, Naam, Bwana, Mungu wetu, atawaangamiza.
Psaumes 7.16 Proverbes 2.22 Psaumes 55.23 Psaumes 12.3 Psaumes 64.8

Cette Bible est dans le domaine public.