Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 94.15
Bible en Swahili de l’est


Jugement des méchants

1 Ee Bwana, Mungu wa kisasi, Mungu wa kisasi, uangaze,
Nahum 1.2 Romains 12.19 Deutéronome 32.35 Esaïe 35.4 Psaumes 80.1
2 Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze, Uwape wenye kiburi stahili zao.
Psaumes 31.23 Genèse 18.25 Psaumes 7.6 Psaumes 74.22 Apocalypse 18.6-18.8
3 Bwana, hata lini wasio haki, Hata lini wasio haki watashangilia?
Job 20.5 Apocalypse 6.10 Psaumes 80.4 Esther 7.6 Psaumes 79.5
4 Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?
Psaumes 31.18 Psaumes 52.1 Esaïe 37.24-37.25 Job 21.14-21.15 Jérémie 18.18
5 Ee Bwana, wanawaseta watu wako; Wanautesa urithi wako;
Esaïe 3.15 Michée 3.2-3.3 Psaumes 79.2-79.3 Jérémie 51.20-51.23 Jérémie 51.34
6 Wanamwua mjane na mgeni; Wanawafisha yatima.
Esaïe 10.2 Ezéchiel 22.7 Jérémie 22.3 Malachie 3.5 Esaïe 13.15-13.18
7 Nao husema, Bwana haoni; Mungu wa Yakobo hafikiri.
Ezéchiel 8.12 Esaïe 29.15 Sophonie 1.12 Psaumes 10.11-10.13 Job 22.12-22.13
8 Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?
Psaumes 92.6 Psaumes 49.10 Deutéronome 32.29 Proverbes 12.1 Proverbes 8.5
9 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione?
Proverbes 20.12 Exode 4.11 Psaumes 139.1-139.12 Proverbes 20.1 Psaumes 17.3
10 Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue?
Job 35.11 Esaïe 28.26 Psaumes 44.2 Ezéchiel 39.21 Psaumes 135.8-135.12
11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.
1 Corinthiens 3.20 Job 11.11-11.12 1 Corinthiens 1.25 1 Corinthiens 1.19 Romains 1.21-1.22
12 Ee Bwana, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;
Proverbes 3.11-3.12 Job 5.17 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.5-12.11 Psaumes 119.71
13 Upate kumstarehesha siku za mabaya, Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo.
Psaumes 55.23 Psaumes 9.15 Habakuk 3.16 Apocalypse 14.13 2 Pierre 2.9
14 Kwa kuwa Bwana hatawatupa watu wake, Wala hutauacha urithi wake,
1 Samuel 12.22 Romains 11.1-11.2 Psaumes 37.28 Deutéronome 32.9 Jérémie 32.39-32.40
15 Maana hukumu itairejea haki, Na wote walio wanyofu wa moyo wataifuata.
Michée 7.9 Job 35.14 Psaumes 9.16 2 Pierre 3.8-3.10 Malachie 3.18
16 Ni nani atakayesimama Kwa ajili yangu juu ya wabaya? Ni nani atakayenisaidia Juu yao wafanyao maovu?
Esaïe 59.16 Matthieu 12.30 Nombres 25.6-25.13 2 Rois 10.15 1 Rois 18.39-18.40
17 Kama Bwana asingalikuwa msaada wangu, Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya.
Psaumes 124.1-124.2 Psaumes 31.17 Psaumes 118.13 Psaumes 13.3 Psaumes 142.4-142.5
18 Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee Bwana, fadhili zako zilinitegemeza.
Psaumes 38.16 Psaumes 121.3 Psaumes 37.23-37.24 Esaïe 41.10 Psaumes 119.116-119.117
19 Katika wingi wa mawazo ya moyoni mwangu, Faraja zako zaifurahisha roho yangu.
Habakuk 3.16-3.18 Psaumes 77.2-77.10 Psaumes 61.2 Psaumes 73.12-73.16 Jérémie 20.7-20.11
20 Je! Kiti cha udhalimu kishirikiane nawe, Kitungacho madhara kwa njia ya sheria?
Psaumes 58.2 Amos 6.3 Esaïe 10.1 Jérémie 7.4-7.11 Apocalypse 13.15-13.17
21 Huishambulia nafsi yake mwenye haki, Na kuihukumu damu isiyo na hatia.
Proverbes 17.15 Exode 23.7 Psaumes 59.3 Matthieu 27.1 Apocalypse 17.6
22 Lakini Bwana amekuwa ngome kwangu, Na Mungu wangu mwamba wangu wa kukimbilia.
Psaumes 18.2 Psaumes 59.9 Psaumes 62.2 Esaïe 33.16 Psaumes 27.1-27.3
23 Naye atawarudishia uovu wao, Atawaangamiza katika ubaya wao, Naam, Bwana, Mungu wetu, atawaangamiza.
Psaumes 7.16 Proverbes 2.22 Psaumes 64.8 Daniel 7.24 Proverbes 14.32

Cette Bible est dans le domaine public.