1 Ee Bwana, Mungu wa kisasi, Mungu wa kisasi, uangaze,
Nahum 1.2 Romains 12.19 Deutéronome 32.35 Esaïe 35.4 Psaumes 80.1
2 Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze, Uwape wenye kiburi stahili zao.
Psaumes 31.23 Genèse 18.25 Psaumes 7.6 Apocalypse 18.6-18.8 Psaumes 74.22
3 Bwana, hata lini wasio haki, Hata lini wasio haki watashangilia?
Job 20.5 Apocalypse 6.10 Psaumes 80.4 Esther 7.6 Psaumes 79.5
4 Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?
Psaumes 31.18 Psaumes 52.1 Job 21.14-21.15 Esaïe 37.24-37.25 Psaumes 140.3
5 Ee Bwana, wanawaseta watu wako; Wanautesa urithi wako;
Esaïe 3.15 Michée 3.2-3.3 Psaumes 79.2-79.3 Jérémie 51.20-51.23 Jérémie 51.34
6 Wanamwua mjane na mgeni; Wanawafisha yatima.
Esaïe 10.2 Ezéchiel 22.7 Jérémie 22.3 Malachie 3.5 Esaïe 13.15-13.18
7 Nao husema, Bwana haoni; Mungu wa Yakobo hafikiri.
Ezéchiel 8.12 Esaïe 29.15 Sophonie 1.12 Psaumes 10.11-10.13 Job 22.12-22.13
8 Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?
Psaumes 92.6 Psaumes 49.10 Deutéronome 32.29 Proverbes 12.1 Proverbes 8.5
9 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione?
Proverbes 20.12 Exode 4.11 Psaumes 139.1-139.12 Proverbes 20.1 Psaumes 17.3
10 Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue?Job 35.11 Esaïe 28.26 Psaumes 44.2 Ezéchiel 39.21 Habakuk 1.12
11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.
1 Corinthiens 3.20 Job 11.11-11.12 1 Corinthiens 1.25 1 Corinthiens 1.19 Romains 1.21-1.22
12 Ee Bwana, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;
Proverbes 3.11-3.12 Job 5.17 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.5-12.11 Psaumes 119.71
13 Upate kumstarehesha siku za mabaya, Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo.
Psaumes 55.23 Psaumes 9.15 Habakuk 3.16 Apocalypse 14.13 2 Pierre 2.9
14 Kwa kuwa Bwana hatawatupa watu wake, Wala hutauacha urithi wake,
1 Samuel 12.22 Romains 11.1-11.2 Psaumes 37.28 Deutéronome 32.9 Jérémie 32.39-32.40
15 Maana hukumu itairejea haki, Na wote walio wanyofu wa moyo wataifuata.
Michée 7.9 Psaumes 9.16 Job 35.14 2 Pierre 3.8-3.10 Malachie 3.18
16 Ni nani atakayesimama Kwa ajili yangu juu ya wabaya? Ni nani atakayenisaidia Juu yao wafanyao maovu?
Esaïe 59.16 Matthieu 12.30 Nombres 25.6-25.13 2 Rois 10.15 1 Rois 18.39-18.40
17 Kama Bwana asingalikuwa msaada wangu, Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya.
Psaumes 124.1-124.2 Psaumes 31.17 Psaumes 118.13 Psaumes 13.3 Psaumes 142.4-142.5
18 Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee Bwana, fadhili zako zilinitegemeza.
Psaumes 38.16 Psaumes 121.3 Psaumes 37.23-37.24 Esaïe 41.10 Psaumes 119.116-119.117
19 Katika wingi wa mawazo ya moyoni mwangu, Faraja zako zaifurahisha roho yangu.
Habakuk 3.16-3.18 Psaumes 77.2-77.10 Psaumes 61.2 Psaumes 73.12-73.16 Jérémie 20.7-20.11
20 Je! Kiti cha udhalimu kishirikiane nawe, Kitungacho madhara kwa njia ya sheria?
Psaumes 58.2 Amos 6.3 Esaïe 10.1 Apocalypse 13.15-13.17 Jérémie 7.4-7.11
21 Huishambulia nafsi yake mwenye haki, Na kuihukumu damu isiyo na hatia.
Proverbes 17.15 Exode 23.7 Psaumes 59.3 Matthieu 27.1 1 Rois 21.19
22 Lakini Bwana amekuwa ngome kwangu, Na Mungu wangu mwamba wangu wa kukimbilia.
Psaumes 18.2 Psaumes 59.9 Psaumes 62.2 Esaïe 33.16 Psaumes 27.1-27.3
23 Naye atawarudishia uovu wao, Atawaangamiza katika ubaya wao, Naam, Bwana, Mungu wetu, atawaangamiza.
Psaumes 7.16 Proverbes 2.22 Psaumes 64.8 Daniel 7.24 Proverbes 14.32