Appel à la grâce de Dieu
 1  Ee Bwana, utege sikio lako unijibu, Maana mimi ni maskini na mhitaji 
Psaumes 31.2  Psaumes 40.17  Psaumes 119.22  Psaumes 17.6  Psaumes 34.6  
 2  Unihifadhi nafsi yangu, Maana mimi ni mcha Mungu. Wewe uliye Mungu wangu, Umwokoe mtumishi wako anayekutumaini. 
Psaumes 4.3  Ephésiens 1.12-1.13  Psaumes 143.12  Jean 12.26  Psaumes 119.94  
 3  Wewe, Bwana, unifadhili, Maana nakulilia Wewe mchana kutwa. 
Psaumes 57.1  Psaumes 88.9  Ephésiens 6.18  Psaumes 25.5  Psaumes 56.1  
 4  Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako, Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana. 
Psaumes 25.1  Psaumes 143.8  Esaïe 61.3  Esaïe 65.18  Psaumes 62.8  
 5  Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, Umekuwa tayari kusamehe, Na mwingi wa fadhili, Kwa watu wote wakuitao. 
Joël 2.13  Psaumes 103.8  Exode 34.6  Néhémie 9.17  Psaumes 25.8  
 6  Ee Bwana, uyasikie maombi yangu; Uisikilize sauti ya dua zangu. 
Psaumes 5.1-5.2  Psaumes 130.2  Psaumes 55.1  Psaumes 17.1  
 7  Siku ya mateso yangu nitakuita, Kwa maana utaniitikia. 
Psaumes 50.15  Psaumes 34.4-34.6  Jonas 2.2  Psaumes 17.6  Lamentations 3.55-3.57  
 8  Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako. 
Deutéronome 3.24  Exode 15.11  Psaumes 89.6  Esaïe 40.25  Daniel 3.29  
 9  Mataifa yote uliowafanya watakuja; Watakusujudia Wewe, Bwana, Watalitukuza jina lako; 
Psaumes 66.4  Apocalypse 15.4  Esaïe 66.23  Esaïe 2.2-2.4  Psaumes 102.15  
 10  Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, Wewe ndiwe mfanya miujiza, Ndiwe Mungu peke yako. 
Psaumes 72.18  Marc 12.29  Esaïe 37.16  1 Corinthiens 8.4  Exode 15.11  
 11  Ee Bwana, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako; 
Jérémie 32.38-32.39  Psaumes 5.8  Job 34.32  Psaumes 26.3  1 Corinthiens 6.17  
 12  Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu, Kwa moyo wangu wote, Nitalitukuza jina lako milele. 
Deutéronome 6.5  Romains 15.6  1 Corinthiens 10.31  1 Corinthiens 6.20  Psaumes 104.33  
 13  Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana; Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu. 
Psaumes 103.8-103.12  Luc 1.58  1 Thessaloniciens 1.10  Psaumes 88.6  Psaumes 30.3  
 14  Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia; Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho. Wala hawakukuweka Wewe Mbele ya macho yao. 
Psaumes 54.3  Psaumes 10.11  Psaumes 119.85  Psaumes 36.1  Psaumes 10.4  
 15  Lakini Wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli. 
Psaumes 103.8  Néhémie 9.17  Psaumes 111.4  Psaumes 86.5  Nombres 14.18  
 16  Unielekee na kunifadhili mimi; Mpe mtumishi wako nguvu zako, Umwokoe mwana wa mjakazi wako. 
Psaumes 116.16  Psaumes 25.16  Colossiens 1.11  Psaumes 28.7-28.8  Esaïe 40.29-40.31  
 17  Unifanyie ishara ya wema, Wanichukiao waione na kuaibishwa. Kwa kuwa Wewe, Bwana, Umenisaidia na kunifariji. 
Psaumes 41.10-41.11  Psaumes 40.1  Psaumes 71.20-71.21  Juges 6.17  1 Corinthiens 5.5