Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 86.12
Bible en Swahili de l’est


Appel à la grâce de Dieu

1 Ee Bwana, utege sikio lako unijibu, Maana mimi ni maskini na mhitaji
Psaumes 31.2 Psaumes 40.17 Matthieu 5.3 Esaïe 37.17 Psaumes 119.22
2 Unihifadhi nafsi yangu, Maana mimi ni mcha Mungu. Wewe uliye Mungu wangu, Umwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
Ephésiens 1.12-1.13 Psaumes 4.3 Psaumes 119.124-119.125 Romains 15.12-15.13 Psaumes 143.12
3 Wewe, Bwana, unifadhili, Maana nakulilia Wewe mchana kutwa.
Psaumes 57.1 Psaumes 88.9 Ephésiens 6.18 Psaumes 25.5 Psaumes 56.1
4 Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako, Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana.
Psaumes 25.1 Psaumes 143.8 Esaïe 66.13-66.14 Esaïe 61.3 Esaïe 65.18
5 Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, Umekuwa tayari kusamehe, Na mwingi wa fadhili, Kwa watu wote wakuitao.
Joël 2.13 Psaumes 103.8 Exode 34.6 Néhémie 9.17 Psaumes 145.8-145.9
6 Ee Bwana, uyasikie maombi yangu; Uisikilize sauti ya dua zangu.
Psaumes 5.1-5.2 Psaumes 130.2 Psaumes 55.1 Psaumes 17.1
7 Siku ya mateso yangu nitakuita, Kwa maana utaniitikia.
Psaumes 50.15 Psaumes 34.4-34.6 Jonas 2.2 Psaumes 17.6 Lamentations 3.55-3.57
8 Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako.
Deutéronome 3.24 Exode 15.11 Psaumes 89.6 Jérémie 10.6-10.7 Jérémie 10.16
9 Mataifa yote uliowafanya watakuja; Watakusujudia Wewe, Bwana, Watalitukuza jina lako;
Psaumes 66.4 Apocalypse 15.4 Esaïe 66.23 Esaïe 43.7 Psaumes 102.18
10 Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, Wewe ndiwe mfanya miujiza, Ndiwe Mungu peke yako.
Psaumes 72.18 Marc 12.29 Esaïe 37.16 1 Corinthiens 8.4 Exode 15.11
11 Ee Bwana, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;
Jérémie 32.38-32.39 1 Corinthiens 10.21 Psaumes 5.8 Job 34.32 Psaumes 26.3
12 Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu, Kwa moyo wangu wote, Nitalitukuza jina lako milele.
Deutéronome 6.5 1 Corinthiens 10.31 Romains 15.6 Apocalypse 5.9-5.13 1 Corinthiens 6.20
13 Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana; Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu.
Luc 1.58 Psaumes 103.8-103.12 1 Thessaloniciens 1.10 Psaumes 88.6 Psaumes 30.3
14 Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia; Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho. Wala hawakukuweka Wewe Mbele ya macho yao.
Psaumes 54.3 Psaumes 140.5 Psaumes 119.51 Psaumes 10.11 Psaumes 119.85
15 Lakini Wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli.
Psaumes 103.8 Néhémie 9.17 Psaumes 111.4 Psaumes 86.5 Joël 2.13
16 Unielekee na kunifadhili mimi; Mpe mtumishi wako nguvu zako, Umwokoe mwana wa mjakazi wako.
Psaumes 25.16 Psaumes 116.16 Psaumes 119.132 Colossiens 1.11 Psaumes 28.7-28.8
17 Unifanyie ishara ya wema, Wanichukiao waione na kuaibishwa. Kwa kuwa Wewe, Bwana, Umenisaidia na kunifariji.
Psaumes 41.10-41.11 1 Corinthiens 5.5 Psaumes 40.1 Psaumes 71.20-71.21 Juges 6.17

Cette Bible est dans le domaine public.