Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 83.9
Bible en Swahili de l’est


Prière contre les ennemis d’Israël

1 Ee Mungu, usistarehe, Ee Mungu, usinyamae, wala usitulie.
Psaumes 28.1 Psaumes 35.22 Psaumes 50.3 Esaïe 42.14 Psaumes 109.1-109.2
2 Maana adui zako wanafanya ghasia, Nao wakuchukiao wameviinua vichwa vyao.
Psaumes 81.15 Juges 8.28 Psaumes 74.23 Actes 22.22 Matthieu 27.24
3 Juu ya watu wako wanafanya hila, Na kushauriana juu yao uliowaficha.
Psaumes 27.5 Psaumes 64.2 Psaumes 31.20 Psaumes 10.9 1 Samuel 13.19
4 Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, Na jina la Israeli halitakumbukwa tena.
Jérémie 11.19 Actes 4.17 Jérémie 48.2 Esther 3.6-3.9 Exode 1.10
5 Maana wanashauriana kwa moyo mmoja, Juu yako wanafanyana agano.
Psaumes 2.2 Esaïe 7.5-7.7 Jean 11.47-11.53 Actes 23.12-23.13 Apocalypse 17.13
6 Hema za Edomu, na Waishmaeli, Na Moabu, na Wahagari,
1 Chroniques 5.10 2 Chroniques 20.1 Psaumes 137.7 1 Chroniques 5.19-5.20 2 Chroniques 20.10-20.11
7 Gebali, na Amoni, na Amaleki, Na Filisti, nao wanaokaa Tiro,
Josué 13.5 Ezéchiel 27.9 Ezéchiel 27.3 1 Samuel 15.2 Amos 1.9
8 Ashuri naye amepatana nao, Wamewasaidia wana wa Lutu.
Deutéronome 2.9 Esaïe 33.2 Genèse 19.37-19.38 2 Rois 15.19 Genèse 25.3
9 Uwatende kama Midiani, kama Sisera, Kama Yabini, penye kijito Kishoni.
Juges 5.21 Esaïe 9.4 Nombres 31.7-31.8 Esaïe 10.26 Juges 4.15-4.24
10 Ambao waliangamizwa Endori; Wakawa samadi juu ya nchi.
Sophonie 1.17 1 Samuel 28.7 Josué 17.11 Jérémie 16.4 Jérémie 8.2
11 Uwafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu, Na masheki yao wote kama Zeba na Zalmuna.
Juges 7.25 Juges 8.12-8.21
12 Ambao Walisema, Na tutamalaki makao ya Mungu.
2 Chroniques 20.11 Psaumes 83.4 Psaumes 74.7-74.8
13 Ee Mungu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, Mithili ya makapi mbele ya upepo,
Job 21.18 Psaumes 35.5 Esaïe 40.24 Jérémie 13.24 Job 13.25
14 Kama moto uteketezao msitu, Kama miali ya moto iiwashayo milima,
Deutéronome 32.22 Esaïe 9.18 Malachie 4.1 Esaïe 33.11-33.12 Esaïe 30.33
15 Ndivyo utakavyowafuatia kwa tufani yako, Na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
Job 9.17 Psaumes 58.9 Ezéchiel 13.11-13.14 Psaumes 50.3 Hébreux 12.18
16 Uwajaze nyuso zao fedheha; Wakalitafute jina lako, Bwana.
Psaumes 132.18 Psaumes 9.19-9.20 Psaumes 109.29 Psaumes 6.10 Job 10.15
17 Waaibike, wafadhaike milele, Naam, watahayarike na kupotea.
Psaumes 35.4 Psaumes 109.29 Psaumes 40.14-40.15 Psaumes 35.26
18 Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.
Exode 6.3 Psaumes 59.13 Michée 4.13 Psaumes 9.16 Esaïe 42.8

Cette Bible est dans le domaine public.