1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.
Psaumes 66.1  Psaumes 8.1  Jérémie 31.7  Psaumes 28.7  Psaumes 33.1-33.3  
 2 Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Psaumes 92.3  Exode 15.20  Psaumes 149.1-149.3  Marc 14.26  Psaumes 95.1-95.2  
 3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
2 Chroniques 8.13  Nahum 1.15  2 Chroniques 2.4  Lamentations 2.6  2 Chroniques 5.12  
 4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo. 
5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Psaumes 114.1  Deutéronome 28.49  Jérémie 5.15  Exode 11.4  Psaumes 77.15  
 6 Nimelitenga bega lake na mzigo, Mikono yake ikaachana na kikapu.
Esaïe 9.4  Esaïe 10.27  Exode 6.6  Exode 1.14  Psaumes 68.13  
 7 Katika shida uliniita nikakuokoa; Nalikuitikia katika sitara ya radi; Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Exode 19.19  Psaumes 50.15  Nombres 20.13  Exode 2.23  Exode 14.10  
 8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;Psaumes 50.7  Deutéronome 5.27  Actes 20.21  Esaïe 55.3-55.4  1 Jean 5.9  
 9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine.
Esaïe 43.12  Deutéronome 32.12  Malachie 2.11  Exode 20.3-20.5  1 Corinthiens 8.5-8.6  
 10 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Exode 20.2  Psaumes 37.3-37.4  Jérémie 31.31-31.33  Ephésiens 3.19-3.20  Jean 15.7  
 11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.
Exode 32.1  Deutéronome 32.15  Proverbes 1.30  Jérémie 7.23-7.24  Deutéronome 32.18  
 12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
Romains 1.24  Jérémie 7.24  Actes 7.42  Romains 1.26-1.27  Esaïe 30.1  
 13 Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Deutéronome 5.29  Esaïe 48.18  Matthieu 23.37  Luc 19.41-19.42  Deutéronome 10.12-10.13  
 14 Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
Amos 1.8  Zacharie 13.7  Nombres 14.45  Josué 23.13  Juges 2.20-2.23  
 15 Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake, Bali wakati wao ungedumu milele.
Romains 1.30  Deutéronome 7.10  Exode 20.5  Joël 3.20  Psaumes 18.44-18.45  
 16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.
Psaumes 147.14  Deutéronome 32.13-32.14  Job 29.6  Juges 14.18  1 Samuel 14.25-14.26