Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 81.5
Bible en Swahili de l’est


Invitation à écouter le Seigneur

1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.
Psaumes 66.1 Psaumes 8.1 Jérémie 31.7 Psaumes 46.11 Philippiens 4.13
2 Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Psaumes 92.3 Exode 15.20 Psaumes 149.1-149.3 Marc 14.26 Psaumes 95.1-95.2
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
2 Chroniques 8.13 Deutéronome 16.15 Nombres 10.1-10.10 1 Chroniques 16.42 1 Chroniques 15.24
4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Psaumes 114.1 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15 Psaumes 77.15 1 Corinthiens 14.21-14.22
6 Nimelitenga bega lake na mzigo, Mikono yake ikaachana na kikapu.
Esaïe 9.4 Esaïe 10.27 Exode 6.6 Exode 1.14 Psaumes 68.13
7 Katika shida uliniita nikakuokoa; Nalikuitikia katika sitara ya radi; Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Nombres 20.13 Exode 19.19 Psaumes 50.15 Exode 2.23 Exode 14.10
8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;
Psaumes 50.7 Jean 3.11 Deutéronome 32.46 Deutéronome 5.27 Actes 20.21
9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine.
Esaïe 43.12 Deutéronome 32.12 Malachie 2.11 Exode 20.3-20.5 1 Corinthiens 8.5-8.6
10 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Exode 20.2 Psaumes 37.3-37.4 Jean 16.23 Apocalypse 21.6 Jérémie 31.31-31.33
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.
Exode 32.1 Deutéronome 32.15 Proverbes 1.30 Jérémie 7.23-7.24 Deutéronome 32.18
12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
Romains 1.24 Jérémie 7.24 Actes 7.42 Romains 1.26-1.27 Esaïe 30.1
13 Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Deutéronome 5.29 Esaïe 48.18 Matthieu 23.37 Luc 19.41-19.42 Deutéronome 10.12-10.13
14 Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
Amos 1.8 Zacharie 13.7 Nombres 14.45 Josué 23.13 Juges 2.20-2.23
15 Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake, Bali wakati wao ungedumu milele.
Romains 1.30 Psaumes 63.3 Deutéronome 7.10 Exode 20.5 Joël 3.20
16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.
Psaumes 147.14 Deutéronome 32.13-32.14 Job 29.6 Juges 14.18 1 Samuel 14.25-14.26

Cette Bible est dans le domaine public.