Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 81.16
Bible en Swahili de l’est


Invitation à écouter le Seigneur

1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.
Psaumes 66.1 Psaumes 8.1 Jérémie 31.7 Psaumes 28.7 Psaumes 33.1-33.3
2 Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Psaumes 92.3 Exode 15.20 Psaumes 149.1-149.3 Marc 14.26 Psaumes 95.1-95.2
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
2 Chroniques 8.13 2 Chroniques 13.14 Nahum 1.15 2 Chroniques 2.4 Lamentations 2.6
4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Psaumes 114.1 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15 Exode 11.4 Psaumes 77.15
6 Nimelitenga bega lake na mzigo, Mikono yake ikaachana na kikapu.
Esaïe 9.4 Esaïe 10.27 Exode 6.6 Exode 1.14 Psaumes 68.13
7 Katika shida uliniita nikakuokoa; Nalikuitikia katika sitara ya radi; Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Exode 19.19 Psaumes 50.15 Nombres 20.13 Exode 2.23 Exode 14.10
8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;
Psaumes 50.7 Deutéronome 5.27 Actes 20.21 Esaïe 55.3-55.4 1 Jean 5.9
9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine.
Esaïe 43.12 Deutéronome 32.12 Malachie 2.11 Exode 20.3-20.5 1 Corinthiens 8.5-8.6
10 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Exode 20.2 Psaumes 37.3-37.4 Jérémie 31.31-31.33 Ephésiens 3.19-3.20 Jean 15.7
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.
Exode 32.1 Deutéronome 32.15 Proverbes 1.30 Jérémie 7.23-7.24 Deutéronome 32.18
12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
Romains 1.24 Jérémie 7.24 Actes 7.42 Romains 1.26-1.27 Esaïe 30.1
13 Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Deutéronome 5.29 Esaïe 48.18 Matthieu 23.37 Luc 19.41-19.42 Deutéronome 10.12-10.13
14 Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
Amos 1.8 Zacharie 13.7 Nombres 14.45 Josué 23.13 Juges 2.20-2.23
15 Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake, Bali wakati wao ungedumu milele.
Romains 1.30 Deutéronome 7.10 Exode 20.5 Joël 3.20 Psaumes 18.44-18.45
16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.
Psaumes 147.14 Deutéronome 32.13-32.14 Job 29.6 Juges 14.18 1 Samuel 14.25-14.26

Cette Bible est dans le domaine public.