Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 81.15
Bible en Swahili de l’est


Invitation à écouter le Seigneur

1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.
Psaumes 66.1 Jérémie 31.7 Psaumes 8.1 Psaumes 100.1-100.2 Psaumes 67.4
2 Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Psaumes 92.3 Psaumes 149.1-149.3 Exode 15.20 Ephésiens 5.19 Colossiens 3.16
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
2 Chroniques 8.13 Lévitique 23.24-23.25 1 Chroniques 16.6 Psaumes 98.6 Nombres 15.3
4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Psaumes 114.1 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15 Psaumes 77.15 1 Corinthiens 14.21-14.22
6 Nimelitenga bega lake na mzigo, Mikono yake ikaachana na kikapu.
Esaïe 9.4 Esaïe 10.27 Matthieu 11.29 Exode 6.6 Exode 1.14
7 Katika shida uliniita nikakuokoa; Nalikuitikia katika sitara ya radi; Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Exode 19.19 Psaumes 50.15 Nombres 20.13 Exode 2.23 Exode 14.10
8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;
Psaumes 50.7 Esaïe 1.19 Exode 15.26 Jean 3.32-3.33 Psaumes 81.13
9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine.
Esaïe 43.12 Deutéronome 32.12 1 Corinthiens 8.5-8.6 Psaumes 44.20 Deutéronome 6.14
10 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Exode 20.2 Psaumes 37.3-37.4 Psaumes 107.9 Apocalypse 22.17 Jérémie 11.4
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.
Exode 32.1 Deutéronome 32.15 Jérémie 7.23-7.24 Deutéronome 32.18 Jérémie 2.11-2.13
12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
Romains 1.24 Jérémie 7.24 Actes 7.42 Romains 1.26-1.27 Esaïe 30.1
13 Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Deutéronome 5.29 Esaïe 48.18 Matthieu 23.37 Luc 19.41-19.42 Deutéronome 10.12-10.13
14 Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
Amos 1.8 Josué 23.13 Juges 2.20-2.23 Nombres 14.9 Zacharie 13.7
15 Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake, Bali wakati wao ungedumu milele.
Romains 1.30 Psaumes 102.28 Esaïe 65.22 Romains 8.7 Psaumes 83.2-83.18
16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.
Psaumes 147.14 Deutéronome 32.13-32.14 Job 29.6 Juges 14.8-14.9 Joël 2.24

Cette Bible est dans le domaine public.