Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 81.10
Bible en Swahili de l’est


Invitation à écouter le Seigneur

1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.
Psaumes 66.1 Jérémie 31.7 Psaumes 8.1 Psaumes 52.7 Psaumes 46.1-46.7
2 Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Psaumes 92.3 Exode 15.20 Psaumes 149.1-149.3 Colossiens 3.16 Marc 14.26
3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
2 Chroniques 8.13 Psaumes 98.6 Nombres 15.3 Colossiens 2.16 Deutéronome 16.15
4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Psaumes 114.1 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15 Psaumes 77.15 1 Corinthiens 14.21-14.22
6 Nimelitenga bega lake na mzigo, Mikono yake ikaachana na kikapu.
Esaïe 9.4 Esaïe 10.27 Exode 6.6 Exode 1.14 Psaumes 68.13
7 Katika shida uliniita nikakuokoa; Nalikuitikia katika sitara ya radi; Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Psaumes 50.15 Nombres 20.13 Exode 19.19 Exode 14.10 Exode 2.23
8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;
Psaumes 50.7 Jean 3.32-3.33 Psaumes 81.13 Jean 3.11 Deutéronome 32.46
9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine.
Esaïe 43.12 Deutéronome 32.12 Deutéronome 6.14 Malachie 2.11 Exode 20.3-20.5
10 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Exode 20.2 Psaumes 37.3-37.4 Apocalypse 22.17 Jérémie 11.4 Jean 16.23
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka.
Exode 32.1 Deutéronome 32.15 Deutéronome 32.18 Jérémie 2.11-2.13 Proverbes 1.30
12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
Romains 1.24 Jérémie 7.24 Actes 7.42 Romains 1.26-1.27 Esaïe 30.1
13 Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Deutéronome 5.29 Esaïe 48.18 Matthieu 23.37 Luc 19.41-19.42 Deutéronome 10.12-10.13
14 Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
Amos 1.8 Nombres 14.9 Zacharie 13.7 Nombres 14.45 Josué 23.13
15 Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake, Bali wakati wao ungedumu milele.
Romains 1.30 Romains 8.7 Psaumes 83.2-83.18 Jean 15.22-15.23 Psaumes 63.3
16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.
Psaumes 147.14 Deutéronome 32.13-32.14 Job 29.6 Joël 2.24 Juges 14.18

Cette Bible est dans le domaine public.