La gloire de Dieu dans la création
 1  Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; 
Psaumes 113.2-113.4  Psaumes 8.9  Psaumes 57.5  Psaumes 148.13  Hébreux 7.26  
 2  Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi. 
Matthieu 21.16  1 Corinthiens 1.27  Matthieu 11.25  Psaumes 44.16  Esaïe 37.20-37.29  
 3  Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha; 
Psaumes 111.2  Job 25.3  Psaumes 148.3  Romains 1.20  Exode 31.18  
 4  Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? 
Psaumes 144.3  Job 7.17  Hébreux 2.6-2.9  Job 25.6  Ezéchiel 8.15  
 5  Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima; 
Hébreux 2.9  Hébreux 2.7  Genèse 1.26-1.27  Genèse 2.7  Psaumes 103.20  
 6  Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. 
Genèse 1.28  Genèse 1.26  Ephésiens 1.22  Matthieu 28.18  Hébreux 2.8  
 7  Kondoo, na ng’ombe wote pia; Naam, na wanyama wa kondeni; 
Genèse 2.20  
 8  Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini. 
Genèse 1.20-1.25  Psaumes 148.10  Job 40.15-41.34  Job 38.39-39.30  
 9  Wewe, MUNGU, Bwana wetu, Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! 
Psaumes 8.1  Deutéronome 33.26  Psaumes 104.24  Job 11.7