1 Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
Psaumes 113.2-113.4  Psaumes 8.9  Psaumes 57.5  Psaumes 148.13  Hébreux 7.26  
 2 Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.
Matthieu 21.16  1 Corinthiens 1.27  Matthieu 11.25  Psaumes 44.16  Exode 15.16  
 3 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha;Psaumes 111.2  Romains 1.20  Exode 31.18  Psaumes 104.19  Genèse 1.1  
 4 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie?
Psaumes 144.3  Job 7.17  Hébreux 2.6-2.9  Ezéchiel 8.15  Psaumes 4.2  
 5 Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima;
Hébreux 2.7  Hébreux 2.9  Genèse 1.26-1.27  Genèse 2.7  Psaumes 21.3-21.5  
 6 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
Genèse 1.28  Genèse 1.26  Hébreux 2.8  Ephésiens 1.22  Matthieu 28.18  
 7 Kondoo, na ng’ombe wote pia; Naam, na wanyama wa kondeni;
Genèse 2.20  
 8 Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini.
Genèse 1.20-1.25  Psaumes 148.10  Job 40.15-41.34  Job 38.39-39.30  
 9 Wewe, MUNGU, Bwana wetu, Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Psaumes 8.1  Deutéronome 33.26  Psaumes 104.24  Job 11.7