Punition des méchants
 1 Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.
Psaumes 27.7  Psaumes 34.4  Lamentations 3.55-3.56  Psaumes 140.1  Psaumes 17.8-17.9  
 2 Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;
Jérémie 11.19  Psaumes 56.6  Matthieu 26.3-26.4  Psaumes 109.2-109.3  Psaumes 31.20  
 3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,
Psaumes 58.7  Psaumes 57.4  Psaumes 11.2  Proverbes 12.18  Jacques 3.6-3.8  
 4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.
Psaumes 55.19  Psaumes 11.2  1 Samuel 18.11  Psaumes 64.7  Psaumes 59.3-59.4  
 5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?
Psaumes 10.11  Psaumes 140.5  Psaumes 94.7  1 Samuel 23.19-23.23  Psaumes 59.7  
 6 Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa.
Psaumes 49.11  Daniel 6.4-6.5  Jean 19.7  1 Samuel 24.9  Esaïe 29.15  
 7 Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa.
Psaumes 7.12-7.13  Lamentations 3.12-3.13  1 Chroniques 10.3-10.7  Deutéronome 32.42  Proverbes 29.1  
 8 Ndivyo watakavyokwazwa, Ulimi wao wenyewe ukishindana nao. Wote wawaonao watatikisa kichwa.Proverbes 18.7  Proverbes 12.13  Luc 19.22  Jérémie 18.16  Psaumes 22.7  
 9 Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake.
Jérémie 51.10  Jérémie 50.28  Psaumes 40.3  Esaïe 5.12  Psaumes 107.42-107.43  
 10 Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu.
Job 22.19  Psaumes 25.20  Psaumes 112.2  Psaumes 97.11  Psaumes 11.1