Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 33.4
Bible en Swahili de l’est


La joie de ceux qui se confient en Dieu

1 Mpigieni Bwana vigelegele, enyi wenye haki, Kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Psaumes 32.11 Psaumes 147.1 Philippiens 4.4 Romains 3.10 Psaumes 78.36-78.37
2 Mshukuruni Bwana kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.
Psaumes 150.3-150.6 Psaumes 144.9 Psaumes 98.4-98.5 2 Samuel 6.5 1 Chroniques 15.28
3 Mwimbieni wimbo mpya, Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.
Psaumes 96.1 Esaïe 42.10 Apocalypse 5.9 Psaumes 144.9 Psaumes 98.1
4 Kwa kuwa neno la Bwana lina adili, Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu.
Psaumes 19.8 Psaumes 119.75 Romains 15.8-15.9 Psaumes 119.128 Psaumes 85.10-85.11
5 Huzipenda haki na hukumu, Nchi imejaa fadhili za Bwana.
Psaumes 11.7 Psaumes 119.64 Psaumes 45.7 Matthieu 5.45 Psaumes 99.4
6 Kwa neno la Bwana mbingu zilifanyika, Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.
Hébreux 11.3 2 Pierre 3.5 Genèse 2.1 Jean 1.1-1.3 Job 26.13
7 Hukusanya maji ya bahari chungu chungu, Huviweka vilindi katika ghala.
Exode 15.8 Josué 3.16 Josué 3.13 Jérémie 5.22 Psaumes 104.6-104.9
8 Nchi yote na imwogope Bwana, Wote wakaao duniani na wamche.
Daniel 6.25-6.26 Hébreux 12.29 Psaumes 67.7 Apocalypse 14.6-14.7 Psaumes 22.27
9 Maana Yeye alisema, ikawa; Na Yeye aliamuru, ikasimama.
Genèse 1.3 Psaumes 148.5-148.6 Psaumes 33.6 Hébreux 1.3 Psaumes 119.90-119.91
10 Bwana huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huyatangua makusudi ya watu.
Psaumes 21.11 Esaïe 8.9-8.10 Esaïe 19.3 Psaumes 140.8 Psaumes 9.15
11 Shauri la Bwana lasimama milele, Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi.
Proverbes 19.21 Job 23.13 Esaïe 46.10 Esaïe 55.8-55.9 Jérémie 29.11
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, Watu aliowachagua kuwa urithi wake.
Psaumes 144.15 Psaumes 65.4 Deutéronome 33.29 1 Pierre 2.9 Tite 2.14
13 Toka mbinguni Bwana huchungulia, Huwatazama wanadamu wote pia.
Psaumes 11.4 Job 28.24 Psaumes 14.2 Jérémie 23.23-23.24 2 Chroniques 16.9
14 Toka mahali pake aketipo Huwaangalia wote wakaao duniani.
1 Rois 8.39 Esaïe 66.1 Luc 11.2 1 Rois 8.30 Esaïe 57.15
15 yeye aiumbaye mioyo yao wote Huzifikiri kazi zao zote.
Jérémie 32.19 Psaumes 44.21 Proverbes 27.19 Job 10.8 Esaïe 64.8
16 Hapana mfalme aokokaye kwa wingi wa uwezo, Wala shujaa haokoki kwa wingi wa nguvu.
2 Samuel 21.16-21.22 Psaumes 44.3 2 Chroniques 20.23 2 Chroniques 32.21 Juges 7.12-7.25
17 Farasi hafai kitu kwa wokovu, Wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake.
Proverbes 21.31 Psaumes 20.7 Psaumes 147.10 Ecclésiaste 9.11 Esaïe 30.16
18 Tazama, jicho la Bwana li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili zake.
Psaumes 147.11 Job 36.7 1 Pierre 3.12 Hébreux 6.18 Psaumes 13.5
19 Yeye huwaponya nafsi zao na mauti, Na kuwahuisha wakati wa njaa.
Psaumes 37.19 Matthieu 6.31-6.33 Proverbes 10.3 Job 5.19-5.22 Psaumes 91.3-91.7
20 Nafsi zetu zinamngoja Bwana; Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.
Psaumes 144.1-144.2 Psaumes 115.9-115.12 Esaïe 40.31 1 Chroniques 5.20 Psaumes 62.5-62.6
21 Maana mioyo yetu itamfurahia, Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu.
Zacharie 10.7 Jean 16.22 Psaumes 30.10-30.12 Psaumes 28.7 Psaumes 13.5
22 Ee Bwana, fadhili zako zikae nasi, Kama vile tulivyokungoja Wewe.
Matthieu 9.29 Psaumes 32.10 Psaumes 119.49 Psaumes 13.5 Psaumes 5.11-5.12

Cette Bible est dans le domaine public.