Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 33.10
Bible en Swahili de l’est


La joie de ceux qui se confient en Dieu

1 Mpigieni Bwana vigelegele, enyi wenye haki, Kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Psaumes 32.11 Psaumes 147.1 Philippiens 4.4 Psaumes 50.14-50.16 Romains 5.19
2 Mshukuruni Bwana kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.
Psaumes 150.3-150.6 Psaumes 144.9 Psaumes 98.4-98.5 Psaumes 92.3 Apocalypse 14.2
3 Mwimbieni wimbo mpya, Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.
Psaumes 96.1 Esaïe 42.10 Psaumes 144.9 Psaumes 98.1 Apocalypse 5.9
4 Kwa kuwa neno la Bwana lina adili, Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu.
Psaumes 19.8 Psaumes 119.75 Deutéronome 32.4 Genèse 24.27 Psaumes 96.13
5 Huzipenda haki na hukumu, Nchi imejaa fadhili za Bwana.
Psaumes 11.7 Psaumes 119.64 Psaumes 45.7 Psaumes 145.15-145.16 Apocalypse 15.3-15.4
6 Kwa neno la Bwana mbingu zilifanyika, Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.
Hébreux 11.3 Genèse 2.1 2 Pierre 3.5 Jean 1.1-1.3 Job 26.13
7 Hukusanya maji ya bahari chungu chungu, Huviweka vilindi katika ghala.
Exode 15.8 Josué 3.16 Josué 3.13 Job 38.8-38.11 Habakuk 3.15
8 Nchi yote na imwogope Bwana, Wote wakaao duniani na wamche.
Psaumes 76.7 Apocalypse 15.4 Psaumes 96.9-96.10 Jérémie 10.7-10.12 Daniel 6.25-6.26
9 Maana Yeye alisema, ikawa; Na Yeye aliamuru, ikasimama.
Genèse 1.3 Psaumes 33.6 Psaumes 148.5-148.6 Psaumes 119.90-119.91 Hébreux 1.3
10 Bwana huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huyatangua makusudi ya watu.
Psaumes 21.11 Esaïe 8.9-8.10 Esaïe 19.3 Esaïe 44.23 Proverbes 21.30
11 Shauri la Bwana lasimama milele, Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi.
Proverbes 19.21 Esaïe 46.10 Job 23.13 Esaïe 55.8-55.9 Jérémie 29.11
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, Watu aliowachagua kuwa urithi wake.
Psaumes 144.15 Psaumes 65.4 Deutéronome 33.29 1 Pierre 2.9 Tite 2.14
13 Toka mbinguni Bwana huchungulia, Huwatazama wanadamu wote pia.
Psaumes 11.4 Job 28.24 Psaumes 14.2 Psaumes 102.19 Genèse 6.12
14 Toka mahali pake aketipo Huwaangalia wote wakaao duniani.
1 Rois 8.39 1 Rois 8.27 1 Rois 8.43 Psaumes 123.1 Esaïe 66.1
15 yeye aiumbaye mioyo yao wote Huzifikiri kazi zao zote.
Jérémie 32.19 Psaumes 44.21 Job 34.21-34.22 Proverbes 22.2 Ecclésiaste 7.29
16 Hapana mfalme aokokaye kwa wingi wa uwezo, Wala shujaa haokoki kwa wingi wa nguvu.
1 Samuel 17.45-17.49 2 Chroniques 20.12 Exode 14.17-14.18 Juges 7.2 1 Rois 20.10
17 Farasi hafai kitu kwa wokovu, Wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake.
Psaumes 20.7 Proverbes 21.31 Psaumes 147.10 2 Rois 7.6-7.7 Osée 14.3
18 Tazama, jicho la Bwana li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili zake.
Job 36.7 Psaumes 147.11 1 Pierre 3.12 Psaumes 34.15-34.20 Psaumes 52.8
19 Yeye huwaponya nafsi zao na mauti, Na kuwahuisha wakati wa njaa.
Psaumes 37.19 Proverbes 10.3 Matthieu 6.31-6.33 Esaïe 33.16 Jean 10.28
20 Nafsi zetu zinamngoja Bwana; Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.
Psaumes 144.1-144.2 Esaïe 8.17 Psaumes 62.1-62.2 Psaumes 27.14 Psaumes 130.5-130.6
21 Maana mioyo yetu itamfurahia, Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu.
Zacharie 10.7 Jean 16.22 Psaumes 30.10-30.12 Psaumes 28.7 Psaumes 13.5
22 Ee Bwana, fadhili zako zikae nasi, Kama vile tulivyokungoja Wewe.
Matthieu 9.29 Psaumes 119.49 Psaumes 13.5 Psaumes 5.11-5.12 Psaumes 119.76

Cette Bible est dans le domaine public.