Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 104.27
Bible en Swahili de l’est


Louange au Dieu de la création

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.
Psaumes 103.22 Psaumes 93.1 Esaïe 59.17 Psaumes 103.1-103.2 Psaumes 96.6
2 Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;
Esaïe 40.22 Daniel 7.9 Matthieu 17.2 Hébreux 1.10-1.12 Zacharie 12.1
3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,
Amos 9.6 Esaïe 19.1 2 Samuel 22.11 Psaumes 18.10-18.11 Apocalypse 1.7
4 Huwafanya malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa moto wa miali.
Hébreux 1.7 2 Rois 2.11 2 Rois 6.17 Psaumes 148.8 Actes 23.8
5 Uliiweka nchi juu ya misingi yake, Isitikisike milele.
Psaumes 24.2 Job 26.7 Psaumes 96.10 Apocalypse 6.14 Ecclésiaste 1.4
6 Uliifunika kwa vilindi kama kwa vazi, Maji yalikuwa yakisimama juu ya milima.
Genèse 7.19 Genèse 1.2-1.10 2 Pierre 3.5
7 Kwa kukemea kwako yakakimbia, Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi,
Psaumes 18.15 Genèse 8.1 Psaumes 77.18 Psaumes 106.9 Psaumes 114.3-114.7
8 Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni, Mpaka mahali ulipoyatengenezea.
Genèse 8.5 Psaumes 33.7
9 Umeweka mpaka yasiupite, Wala yasirudi kuifunikiza nchi.
Genèse 9.11-9.15 Jérémie 5.22 Job 26.10 Job 38.10-38.11 Esaïe 54.9
10 Hupeleka chemchemi katika mabonde; Zapita kati ya milima;
Esaïe 41.18 Psaumes 107.35 Deutéronome 8.7 Esaïe 35.7
11 Zamnywesha kila mnyama wa kondeni; Punda mwitu huzima kiu yao.
Job 39.5-39.8 Psaumes 104.13 Psaumes 145.16
12 Kandokando hukaa ndege wa angani; Kati ya matawi hutoa sauti zao.
Psaumes 148.10 Matthieu 6.26 Psaumes 147.9 Psaumes 84.3 Matthieu 8.20
13 Huinywesha milima toka orofa zake; Nchi imeshiba mazao ya kazi zako.
Psaumes 147.8 Jérémie 10.13 Deutéronome 11.11 Jérémie 14.22 Matthieu 5.45
14 Huyameesha majani kwa makundi, Na maboga kwa matumizi ya mwanadamu; Ili atoe chakula katika nchi,
Job 28.5 Psaumes 147.8-147.9 Genèse 3.18 Genèse 9.3 Psaumes 136.25
15 Na divai imfurahishe mtu moyo wake. Aung’aze uso wake kwa mafuta, Na mkate umburudishe mtu moyo wake.
Psaumes 23.5 Juges 9.13 Ecclésiaste 10.19 Psaumes 92.10 Proverbes 31.6
16 Miti ya Bwana nayo imeshiba, Mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Nombres 24.6 Psaumes 92.2 Psaumes 29.5 Ezéchiel 17.23
17 Ndimo ndege wafanyamo vitundu vyao, Na korongo, misunobari ni nyumba yake.
Psaumes 104.12 Lévitique 11.19 Jérémie 22.23 Abdias 1.4 Jérémie 8.7
18 Milima mirefu ndiko waliko mbuzi wa mwitu, Na magenge ni kimbilio la wibari.
Proverbes 30.26 Job 39.1 1 Samuel 24.2 Deutéronome 14.7 Lévitique 11.5
19 Aliufanya mwezi kwa ajili ya nyakati, Jua latambua kuchwa kwake.
Job 38.12 Deutéronome 4.19 Psaumes 136.7-136.9 Job 31.26-31.28 Jérémie 31.35
20 Wewe hufanya giza, kukawa usiku, Ndipo atambaapo kila mnyama wa mwitu.
Esaïe 45.7 Psaumes 74.16 Psaumes 139.10-139.12 Amos 1.13 Genèse 8.22
21 Wana-simba hunguruma wakitaka mawindo, Ili kutafuta chakula chao kwa Mungu.
Job 38.39 Joël 1.20 Psaumes 147.9 Psaumes 145.15 Psaumes 34.10
22 Jua lachomoza, wanakwenda zao, Na kujilaza mapangoni mwao.
Job 37.8 Jean 3.20 Nahum 3.17 Job 24.13-24.17
23 Mwanadamu atoka kwenda zake kazini, Na kwenye utumishi wake mpaka jioni.
Genèse 3.19 Ephésiens 4.28 Ecclésiaste 5.12 Juges 19.16 2 Thessaloniciens 3.8-3.12
24 Ee Bwana, jinsi yalivyo mengi matendo yako! Kwa hekima umevifanya vyote pia. Dunia imejaa mali zako.
Jérémie 10.12 Psaumes 40.5 Genèse 1.31 Psaumes 50.10-50.12 Proverbes 8.22-8.36
25 Bahari iko kule, kubwa na upana, Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika, Viumbe hai vidogo kwa vikubwa.
Psaumes 69.34 Genèse 1.28 Deutéronome 33.19 Actes 28.5 Genèse 3.1
26 Ndimo zipitamo merikebu, Ndimo alimo lewiathani uliyemwumba acheze humo.
Esaïe 27.1 Psaumes 107.23 Psaumes 74.14 Job 3.8 Ezéchiel 27.9
27 Hao wote wanakungoja Wewe, Uwape chakula chao kwa wakati wake.
Psaumes 147.9 Psaumes 136.25 Job 36.31 Job 38.41 Luc 12.24-12.28
28 Wewe huwapa, Wao wanakiokota; Wewe waukunjua mkono wako, Wao wanashiba mema;
Psaumes 145.16
29 Wewe wauficha uso wako, Wao wanafadhaika; Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao,
Job 34.14-34.15 Genèse 3.19 Ecclésiaste 12.7 Psaumes 30.7 Deutéronome 31.17
30 Waipeleka roho yako, wanaumbwa, Nawe waufanya upya uso wa nchi.
Job 33.4 Apocalypse 21.5 Ezéchiel 37.9 Job 26.13 Tite 3.5
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele; Bwana na ayafurahie matendo yake.
Genèse 1.31 Romains 11.36 1 Pierre 5.11 Luc 15.5-15.6 Apocalypse 5.12-5.13
32 Aitazama nchi, inatetemeka; Aigusa milima, inatoka moshi.
Exode 19.18 Psaumes 144.5 Habakuk 3.10 Psaumes 97.4-97.5 Psaumes 114.7
33 Nitamwimbia Bwana maadamu ninaishi; Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai;
Psaumes 63.4 Psaumes 146.2 Psaumes 145.1-145.2
34 Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Mimi nitamfurahia Bwana.
Psaumes 1.2 Psaumes 77.12 Psaumes 139.17-139.18 Habakuk 3.17-3.18 Psaumes 119.127-119.128
35 Wenye dhambi waangamizwe katika nchi, Watendao ubaya wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Psaumes 37.38 Psaumes 106.48 Psaumes 59.13 Psaumes 105.45 Psaumes 103.22-104.1

Cette Bible est dans le domaine public.