Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 27.8
Bible en Swahili de l’est


Conclusion de Job

1 Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema,
Job 29.1 Nombres 24.15 Nombres 23.7 Proverbes 26.7 Psaumes 49.4
2 Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu; Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu;
Job 34.5 Nombres 14.21 2 Rois 4.27 Job 9.18 Ruth 1.20-1.21
3 (Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani yangu, Na roho ya Mungu i katika pua yangu;)
Job 33.4 Genèse 2.7 Esaïe 2.22 Actes 17.25 Job 32.8
4 Hakika midomo yangu haitanena yasiyo haki, Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
Job 13.7 Job 6.28 Jean 8.55 2 Corinthiens 11.10 Job 34.6
5 Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki; Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu.
Job 2.9 Job 13.15 Deutéronome 25.1 Job 29.14 Job 32.3
6 Haki yangu naishika sana, wala sitaiacha; Moyo wangu hautanisuta wakati nikiwapo hai.
Job 2.3 Actes 24.16 Psaumes 18.20-18.23 Proverbes 4.13 2 Corinthiens 12.11
7 Adui yangu na awe kama huyo mwovu, Na mwenye kuondoka kinyume changu na awe kama asiye haki.
2 Samuel 18.32 1 Samuel 25.26 Daniel 4.19
8 Kwani tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida, Hapo Mungu amwondoleapo roho yake?
Matthieu 16.26 Job 11.20 Luc 12.20-12.21 Job 8.13 Job 13.16
9 Je! Mungu atakisikia kilio chake, Taabu zitakapomfikilia?
Esaïe 1.15 Jérémie 14.12 Michée 3.4 Proverbes 1.28 Psaumes 18.41
10 Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi, Na kumlingana Mungu nyakati zote?
Psaumes 37.4 Job 22.26-22.27 Matthieu 13.21 1 Thessaloniciens 5.17 Ephésiens 6.18
11 Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu; Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.
Job 6.10 Esaïe 8.11 Job 32.8-32.10 Actes 20.20 Psaumes 71.17
12 Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe; Mbona basi mmebatilika kabisa?
Job 21.3 Job 17.2 Job 26.2-26.4 Ecclésiaste 8.14 Job 21.28-21.30
13 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu, Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi.
Job 20.19-20.29 2 Pierre 2.9 Proverbes 22.22-22.23 Esaïe 3.11 Psaumes 11.6
14 Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga; Na wazao wake hawatashiba chakula.
Deutéronome 28.41 Job 20.10 Luc 23.29 Job 15.22 Esther 9.5-9.10
15 Hao watakaosalia kwake watazikwa katika kufa, Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza.
Psaumes 78.64 1 Rois 21.21-21.24 1 Rois 16.3-16.4 Jérémie 22.18 1 Rois 14.10-14.11
16 Ajapokusanya fedha kama mavumbi, Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi;
Zacharie 9.3 1 Rois 10.27 Jacques 5.2 Matthieu 6.19 Habakuk 2.6
17 Yumkini kuyatengeza, lakini wenye haki watayavaa, Nao wasio na hatia watazigawanya hizo fedha.
Proverbes 13.22 Ecclésiaste 2.26 Proverbes 28.8
18 Yeye hujenga nyumba yake kama mdudu, Na kama kibanda afanyacho mlinzi.
Esaïe 1.8 Job 8.14-8.15 Esaïe 38.12 Lamentations 2.6 Esaïe 51.8
19 Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho; Hufunua macho yake, naye hayuko.
Job 24.24 Jérémie 8.2 Job 7.8 Job 30.23 Genèse 49.10
20 Vitisho vyampata kama maji mengi; Dhoruba humwiba usiku.
Job 15.21 Job 18.11 Exode 12.29 Job 22.16 Jonas 2.3
21 Upepo wa mashariki humchukua, naye huondoka; Na kumkumba atoke mahali pake.
Psaumes 58.9 Nahum 1.3-1.8 Osée 13.15 Job 7.10 Jérémie 18.17
22 Kwani Mungu atamtupia asimhurumie; Angependa kuukimbia mkono wake.
Exode 14.25-14.28 Amos 2.14 Exode 9.14 Juges 4.17-4.21 Jérémie 13.14
23 Watu watampigia makofi, Na kumzomea atoke mahali pake.
Lamentations 2.15 Sophonie 2.15 Jérémie 19.8 1 Rois 9.8 Proverbes 11.10

Cette Bible est dans le domaine public.