Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 23.9
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 8 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Hata leo mashitaka yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu.
Job 10.1 Job 11.6 Psaumes 32.4 Job 7.11 Job 6.2-6.3
3 Laiti ningejua mahali niwezapo kumwona, Nifike hata hapo anapokaa!
Job 16.21 Job 13.3 Esaïe 26.8 Hébreux 4.6 Job 31.35-31.37
4 Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja.
Job 13.18 Esaïe 43.26 Genèse 32.12 Exode 32.12-32.13 Josué 7.8-7.9
5 Ningeyajua maneno atakayonijibu, Na kuelewa na hayo atakayoniambia.
Job 13.22-13.23 Job 10.2 Job 42.2-42.6 1 Corinthiens 4.3-4.4
6 Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza.
Job 13.21 Job 9.33-9.34 2 Corinthiens 12.9-12.10 Esaïe 27.8 Psaumes 138.3
7 Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele.
Job 13.3 Jérémie 12.1 Jérémie 3.5 Romains 8.33-8.34 Romains 8.1
8 Tazama, naenda mbele, wala hayuko; Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona;
Job 9.11 Psaumes 10.1 1 Timothée 6.16 Job 35.14 Psaumes 13.1-13.3
9 Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone.
Esaïe 8.17 Psaumes 89.46
10 Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
1 Pierre 1.7 Psaumes 139.1-139.3 Jacques 1.12 Psaumes 66.10 Zacharie 13.9
11 Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.
Psaumes 44.18 Psaumes 17.5 Psaumes 125.5 Job 17.9 Romains 2.7
12 Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,
Jean 4.34 Jérémie 15.16 Psaumes 119.103 Job 22.22 Jean 6.66-6.69
13 Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza? Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo.
Psaumes 115.3 Proverbes 19.21 Daniel 4.35 Job 12.14 Nombres 23.19-23.20
14 Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa; Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye.
1 Thessaloniciens 3.3 Romains 11.33 Job 7.3 1 Pierre 2.8 1 Thessaloniciens 5.9
15 Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake; Nitakapofikiri, namwogopa.
Psaumes 119.120 Job 31.23 Job 10.15 Psaumes 77.3 Job 23.3
16 Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye Mwenyezi amenitaabisha;
Job 27.2 Psaumes 22.14 Deutéronome 20.3 Psaumes 88.16 Joël 1.15
17 Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso.
Job 19.8 Job 22.11 Job 15.22 Esaïe 57.1 Job 18.6

Cette Bible est dans le domaine public.