Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 6.9
Bible en Swahili de l’est


Achèvement de la muraille

1 Basi ikawa, walipoarifiwa Sanbalati, na Tobia, na Geshemu, Mwarabu na adui zetu hao wengine, kwamba nimeujenga ukuta, wala hayakusalia mavunjiko ndani yake; (ijapokuwa hata wakati ule sijaisimamisha milango katika malango);
Néhémie 2.10 Néhémie 2.19 Néhémie 3.3 Néhémie 3.1 Néhémie 4.1
2 Sanbalati na Geshemu wakatuma wajumbe kwangu, wakasema, Njoo, tukutane huko vijijini katika nchi tambarare ya Ono. Walakini wakakusudi kunifanyia mabaya.
1 Chroniques 8.12 Psaumes 37.12 Psaumes 37.32 Psaumes 12.2 2 Samuel 20.9
3 Na mimi nikatuma wajumbe kwao, nikasema, Hii ni kazi kubwa ninayoifanya mimi, hata nisiweze kushuka; mbona kazi ikome, hapo ninapoiacha, niwashukie?
1 Timothée 4.15-4.16 Jean 9.4 Luc 14.30 Proverbes 14.15 Matthieu 10.16
4 Nao wakaniletea maneno kama hayo mara nne; nikawajibu maneno kama yale.
Juges 16.10 Galates 2.5 Juges 16.15-16.20 Luc 18.5 Proverbes 14.15
5 Ndipo Sanbalati akamtuma kwangu mtumwa wake vile vile mara ya tano, na barua wazi mkononi mwake;
Ephésiens 6.11 2 Corinthiens 11.13-11.15 2 Corinthiens 2.11 2 Thessaloniciens 2.10 2 Rois 18.26-18.28
6 nayo yakaandikwa humo, Habari imeenea katika mataifa, naye Geshemu asema neno lilo hilo, ya kwamba wewe na Wayahudi mwakusudi kuasi; ndiyo sababu waujenga huo ukuta; nawe wataka kuwamiliki, ndivyo wasemavyo.
Néhémie 2.19 Jérémie 20.10 2 Corinthiens 6.8 Jean 19.13 Jérémie 9.3-9.6
7 Nawe umewaweka manabii ili wakuhubirie huko Yerusalemu, kusema, Yuko mfalme katika Yuda; basi sasa ataarifiwa mfalme sawasawa na maneno haya. Njoo sasa basi, na tufanye shauri pamoja.
1 Rois 1.25 1 Rois 1.7 1 Rois 1.34 Actes 23.15 2 Samuel 15.10-15.12
8 Ndipo mimi nikatuma kwake wajumbe, kusema, Hakukufanyika mambo kama hayo uyasemayo, lakini kwa moyo wako wewe mwenyewe umeyabuni.
Psaumes 52.2 Job 13.4 Esaïe 59.4 Matthieu 12.34 Daniel 11.27
9 Kwani hao wote walitaka kutuogofisha, wakisema, Italegea mikono yao katika kazi, isifanyike. Lakini sasa nitaitia mikono yangu nguvu.
Psaumes 138.3 Philippiens 4.13 1 Pierre 5.10 Ephésiens 3.16 Esdras 4.1-4.24
10 Nikaingia nyumbani kwa Shemaya, mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, aliyekuwa amefungwa; naye akasema, Tukutane nyumbani mwa Mungu, ndani ya hekalu, tukaifunge milango ya hekalu; kwa maana watakuja kukuua; naam, wakati wa usiku watakuja kukuua.
Jérémie 36.5 2 Rois 11.3 Job 24.13-24.17 Proverbes 11.9 2 Chroniques 29.3
11 Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia.
Proverbes 28.1 Actes 21.13 Psaumes 112.6 Psaumes 112.8 Luc 13.31-13.33
12 Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri.
Ezéchiel 13.22 Ezéchiel 13.7 Jérémie 23.16 1 Jean 4.1 Apocalypse 18.13
13 Kwa sababu hii aliajiriwa, ili mimi niogope, nikafanye hivyo na kutenda dhambi, kisha wao wawe nazo habari mbaya, ili wanishutumie.
Jacques 4.17 Jérémie 20.10 Jérémie 18.18 Néhémie 6.6 Proverbes 29.5
14 Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, Tobia na Sanbalati sawasawa na hayo matendo yao, na yule nabii mke Noadia, na hao manabii waliosalia, waliotaka kuniogofya.
Néhémie 13.29 2 Timothée 4.14-4.15 Jérémie 11.20-11.23 Jérémie 28.1 Néhémie 5.19
15 Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku hamsini na mbili.
Néhémie 4.1-4.2 Esdras 6.15 Daniel 9.25 Psaumes 1.3
16 Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo makafiri wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu.
Psaumes 126.2 Néhémie 4.7 Néhémie 4.1 Néhémie 2.10 Josué 5.1
17 Tena siku zile wakuu wa Yuda walimletea Tobia nyaraka nyingi, nazo nyaraka za Tobia zikawafikilia.
Néhémie 13.28 Néhémie 3.5 Michée 7.1-7.6 Néhémie 5.7 Matthieu 24.10-24.12
18 Kwa maana walikuwa watu wengi katika Yuda waliomwapia, kwa sababu alikuwa mkwewe Shekania, mwana wa Ara; naye Yehohanani mwanawe amemwoa binti Meshulamu, mwana wa Berekia.
Esdras 2.5 Néhémie 3.4 Néhémie 7.10 Néhémie 3.30
19 Tena waliyanena mema yake mbele yangu, nayo maneno yangu humwambia yeye. Tobia naye akaniletea mimi nyaraka za kuniogofisha.
Néhémie 6.13 Néhémie 6.9 Proverbes 28.4 Esaïe 37.10-37.14 Actes 4.18-4.21

Cette Bible est dans le domaine public.