Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 13.17
Bible en Swahili de l’est


Dégradation de la situation

1 Siku hiyo walisoma katika kitabu cha Musa masikioni mwa watu; na ndani yake yalionekana maneno haya yameandikwa, ya kwamba Mwamoni na Mmoabi wasiingie katika kusanyiko la Mungu milele;
Deutéronome 23.3-23.5 Néhémie 9.3 Néhémie 13.23 Deutéronome 31.11-31.12 2 Rois 23.2
2 kwa sababu hawakuwalaki wana wa Israeli kwa chakula na maji, bali walimwajiri Balaamu juu yao ili awalaani; lakini Mungu aliigeuza ile laana kuwa baraka.
Deutéronome 23.5 Matthieu 25.40 Psaumes 109.28 Michée 6.5 Nombres 22.3-22.11
3 Ikawa walipoisikia torati, wakawatenga Israeli na umati wa watu waliochanganyika nao.
Néhémie 9.2 Exode 12.38 Nombres 11.4 Néhémie 10.28 Esdras 10.11
4 Na kabla ya hayo, Eliashibu, kuhani, aliyewekwa avisimamie vyumba vya nyumba ya Mungu wetu, kwa kuwa alikuwa karibu yake Tobia,
Néhémie 12.44 Néhémie 2.10 Néhémie 13.28 Néhémie 6.17-6.18 Néhémie 12.10
5 alikuwa amemtengenezea chumba kikubwa, hapo walipoweka zamani sadaka za unga, na ubani, na vyombo, na zaka za nafaka, na divai, na mafuta, walivyoamriwa kuwapa Walawi, na waimbaji, na mabawabu; tena sadaka za kuinuliwa zilizokuwa za makuhani.
Néhémie 12.44 2 Chroniques 34.11 Nombres 18.21-18.24 Néhémie 10.38
6 Lakini wakati huo wote mimi sikuwako huko Yerusalemu; maana katika mwaka wa thelathini na mbili wa Artashasta, mfalme wa Babeli, nalimrudia mfalme; na baada ya siku kadha wa kadha nikaomba ruhusa tena kwa mfalme.
Néhémie 5.14 Néhémie 2.5-2.6 2 Chroniques 24.17-24.18 Esdras 6.22 Exode 32.1
7 Nami nikaja Yerusalemu, nikafahamu yale mabaya, ambayo Eliashibu ameyatenda kwa ajili ya Tobia, kwa kumtengenezea chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
Néhémie 13.5 Néhémie 13.1 Matthieu 21.12-21.13 Lamentations 1.10 1 Corinthiens 1.11
8 Nami nikasikitika sana; basi nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia vitoke humo chumbani.
Esdras 10.1 Psaumes 69.9 Esdras 9.3-9.4 Marc 11.15-11.17 Jean 2.13-2.17
9 Kisha nikatoa amri, nao wakavisafisha vyumba; nami nikavirudisha humo vyombo vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za unga na ubani.
2 Chroniques 29.5 Néhémie 12.45 2 Chroniques 29.15-29.19
10 Tena nikaona ya kwamba Walawi hawakupewa sehemu zao; basi wamekimbia Walawi na waimbaji, waliofanya kazi, kila mtu shambani kwake.
Néhémie 10.37 Malachie 3.8 Deutéronome 12.19 Néhémie 12.47 Néhémie 12.28-12.29
11 Ndipo nikagombana na mashehe, nikasema, Mbona nyumba ya Mungu imeachwa? Kisha nikawakusanya, nikawaweka mahali pao.
Néhémie 10.39 Néhémie 13.25 Néhémie 13.17 1 Samuel 2.17 Malachie 3.8-3.11
12 Ndipo Yuda wote walipoleta zaka za nafaka, na mvinyo, na mafuta, kwenye hazina.
Néhémie 12.44 Néhémie 10.37-10.39 Malachie 3.10 Nombres 18.20-18.26 Deutéronome 14.22
13 Nami nikawaweka watunza hazina juu ya hazina, yaani, Shelemia kuhani, na Sadoki mwandishi, na wa Walawi, Pedaya; na wa pili wao alikuwa Hanani, mwana wa Zakuri, mwana wa Matania; kwani walihesabiwa kuwa waaminifu, na ilikuwa juu yao kuwagawia ndugu zao.
Néhémie 7.2 1 Corinthiens 4.2 Néhémie 12.44 Actes 6.3 Actes 6.1
14 Unikumbukie hayo, Ee Mungu wangu, wala usifute fadhili zangu nilizozitenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu, na kwa taratibu zake.
Néhémie 5.19 Psaumes 122.6-122.9 Néhémie 13.31 Néhémie 13.22 1 Chroniques 29.3
15 Siku hizo naliona katika Yuda watu wengine waliokanyaga mashinikizo ya mvinyo siku ya sabato, na wengine waliochukua miganda, na kuwapakia punda zao; tena na mvinyo, na zabibu, na tini, na namna zote za mizigo, waliyoileta Yerusalemu, siku ya sabato; nami nikashuhudia juu yao siku ile waliyouza vyakula.
Néhémie 10.31 Exode 34.21 Néhémie 13.21 Jérémie 17.21-17.22 Exode 20.8-20.11
16 Tena wakakaa humo watu wa Tiro, walioleta samaki, na biashara za kila namna, wakawauzia wana wa Yuda siku ya sabato, na mumo humo Yerusalemu.
Exode 23.12 Deutéronome 5.14
17 Ndipo nikagombana na wakuu wa Yuda, nikawaambia, Ni neno baya gani hili mnalofanya ninyi, na kuinajisi siku ya sabato?
Néhémie 13.11 Néhémie 13.25 Jérémie 13.18 Jérémie 5.5 Esaïe 1.10
18 Je! Sivyo hivyo walivyofanya baba zenu; na Mungu wetu, je! Hakuyaleta mabaya haya yote juu yetu, na juu ya mji huu? Nanyi hata hivyo mwazidi kuleta ghadhabu juu ya Israeli kwa kuinajisi sabato!
Jérémie 17.21-17.23 Ezéchiel 23.8 Josué 22.17-22.18 Lévitique 26.18 Esdras 9.13-9.15
19 Ikawa malango ya Yerusalemu yalipoanza kuwa na giza kabla ya sabato, naliamuru milango ifungwe, nikaamuru isifunguliwe hata sabato iishe; na baadhi ya watumishi wangu nikawaweka juu ya malango, ili usiingizwe mzigo wo wote siku ya sabato.
Lévitique 23.32 Jérémie 17.19-17.22 Exode 31.14-31.17 Lévitique 23.22 Néhémie 7.3
20 Basi wenye biashara na wachuuzi wa bidhaa za kila namna wakalala nje ya Yerusalemu mara mbili tatu.
21 Ndipo nikawashuhudia, nikawaambia, Mbona mwalala mbele ya ukuta? Mkitenda hivi tena, nitawakamata. Tangu wakati ule hawakuja tena siku ya sabato.
Romains 13.3-13.4 Esdras 7.26 1 Pierre 2.14 Néhémie 13.15
22 Kisha nikawaamuru Walawi wajitakase, nao waje kuyalinda malango, ili kuitakasa siku ya sabato. Unikumbukie hayo nayo, Ee Mungu wangu, ukaniachilie sawasawa na wingi wa rehema zako.
Néhémie 12.30 Néhémie 13.14 Néhémie 13.31 Psaumes 130.3-130.4 Esaïe 55.7
23 Tena siku zizo hizo nikawaona wale Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake wa Ashdodi, na Amoni, na Moabu;
Néhémie 10.30 Esdras 9.1-9.2 Néhémie 13.1 Esdras 10.10 Esdras 10.44
24 na watoto wao wakanena nusu kwa lugha ya Ashdodi, wala hawakuweza kunena kwa Kiyahudi, bali kwa lugha ya watu hao mojawapo.
Sophonie 3.9
25 Nikagombana nao, nikawalaani, nikawapiga baadhi yao, na kuwang’oa nywele zao; nikawaapisha kwa Mungu, nikasema, Msiwaoze wana wao binti zenu, wala msiwatwae binti zao ili waolewe na wana wenu, wala na ninyi wenyewe.
Esdras 10.5 Néhémie 10.29-10.30 Néhémie 13.17 Néhémie 13.11 Exode 34.16
26 Je! Sulemani, mwana wa Daudi, hakufanya dhambi kwa kutenda hayo? Lakini katika mataifa mengi hapakuwa na mfalme mwingine mfano wake. Tena alipendwa na Mungu wake, naye Mungu akamfanya mfalme juu ya Israeli; walakini wanawake wageni walimkosesha hata yeye.
1 Rois 3.13 2 Chroniques 1.12 2 Samuel 12.24-12.25 1 Rois 11.1-11.8 2 Chroniques 9.22
27 Basi, na sisi, je! Tuwasikilize ninyi kutenda neno hili baya, hata kumhalifu Mungu wetu kwa kuwaoa wanawake wageni?
Esdras 10.2 1 Samuel 30.24
28 Na mwana mmoja wa Yoyada, mwana wa Eliashibu, kuhani mkuu, alikuwa mkwewe Sanbalati, Mhoroni, basi nikamfukuza kwangu.
Néhémie 2.19 Néhémie 3.1 Néhémie 12.10 Néhémie 2.10 Néhémie 12.22
29 Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, jinsi walivyounajisi ukuhani, na agano la ukuhani na la Walawi.
Néhémie 6.14 Lévitique 21.1-21.7 Nombres 16.9-16.10 Psaumes 59.5-59.13 1 Samuel 2.30
30 Hivyo nikawatakasa na kila kitu kigeni, nami nikawaagizia zamu makuhani na Walawi, kila mtu kazini mwake;
Néhémie 10.30 Néhémie 12.1-12.26 1 Chroniques 23.1-23.26
31 na matoleo ya kuni nyakati zilizoamriwa, na malimbuko. Nikumbuke, Ee Mungu wangu, ili unitendee mema.
Néhémie 13.22 Néhémie 10.34 Néhémie 13.14 Psaumes 106.4 Psaumes 26.8-26.9

Cette Bible est dans le domaine public.