Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 33.4
Bible en Swahili de l’est


Règne de Manassé

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka hamsini na mitano.
2 Rois 21.1-21.18 1 Chroniques 3.13 Matthieu 1.10 Esaïe 3.12 2 Chroniques 32.33
2 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, sawasawa na machukizo yote ya mataifa, aliowafukuza Bwana mbele ya wana wa Israeli.
2 Chroniques 28.3 Deutéronome 18.9 Esdras 9.14 Psaumes 106.35-106.40 Jérémie 15.4
3 Kwa maana akapajenga tena mahali pa juu alipopabomoa Hezekia babaye; akazisimamisha madhabahu za mabaali, akafanya na sanamu za maashera, akaabudu jeshi lote la mbinguni, na kulitumikia.
Deutéronome 16.21 2 Chroniques 31.1 Deutéronome 17.3 2 Rois 18.4 2 Rois 23.5-23.6
4 Akajenga madhabahu katika nyumba ya Bwana, napo ndipo alipopanena Bwana, Katika Yerusalemu litakuwako jina langu milele.
2 Chroniques 7.16 2 Chroniques 6.6 2 Chroniques 34.3-34.4 2 Chroniques 32.19 2 Chroniques 33.15
5 Akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni katika nyua mbili za nyumba ya Bwana.
2 Chroniques 4.9 Ezéchiel 8.7-8.18 Jérémie 32.34-32.35
6 Tena akawapitisha wanawe motoni katika bonde la mwana wa Hinomu; akatazama bao, akabashiri, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.
2 Chroniques 28.3 2 Rois 21.6 Lévitique 20.6 1 Chroniques 10.13 Lévitique 19.31
7 Akaiweka sanamu ya kuchonga aliyoifanya, katika nyumba ya Mungu ambayo Mungu alimwambia Daudi, na Sulemani mwanawe, Katika nyumba hii, na katika Yerusalemu, niliouchagua miongoni mwa kabila zote za Israeli, nitaliweka jina langu milele;
2 Chroniques 33.4 2 Chroniques 6.6 2 Chroniques 33.15 2 Rois 21.7-21.8 Psaumes 132.13-132.14
8 wala sitawaondoshea miguu tena Israeli katika nchi niliyowaagizia baba zenu; wakiangalia tu kutenda yote niliyowaamuru, yaani, torati yote, na sheria, na maagizo, niliyowaamuru kwa mkono wa Musa.
2 Samuel 7.10 Lévitique 8.36 Esaïe 1.19-1.20 Deutéronome 30.15-30.20 Lévitique 10.11
9 Basi Manase akawakosesha Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, hata wakazidi kufanya mabaya kuliko mataifa, aliowaharibu Bwana mbele ya wana wa Israeli.
2 Rois 17.8-17.11 2 Rois 24.3-24.4 Michée 6.16 1 Rois 14.16 Proverbes 29.12
10 Naye Bwana akasema na Manase, na watu wake; wala wasiangalie.
2 Chroniques 36.15-36.16 Zacharie 1.4 Actes 7.51-7.52 Jérémie 25.4-25.7 Jérémie 44.4-44.5
11 Kwa hiyo Bwana akaleta juu yao maakida wa jeshi la mfalme wa Ashuru, waliomkamata Manase kwa minyororo, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli.
Deutéronome 28.36 2 Rois 25.6 Job 36.8-36.11 Esaïe 36.9 Esaïe 5.26-5.30
12 Hata alipokuwa katika taabu, akamsihi Bwana, Mungu wake, akajinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.
2 Chroniques 32.26 2 Chroniques 28.22 2 Chroniques 33.23 Luc 18.14-18.15 Luc 15.16-15.18
13 Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba Bwana ndiye Mungu.
Esdras 8.23 1 Chroniques 5.20 Daniel 4.25 Jean 4.10 Esaïe 55.6-55.9
14 Hata baada ya hayo akaujengea mji wa Daudi ukuta wa nje, upande wa magharibi wa Gihoni, bondeni, hata kufika maingilio ya lango la samaki; akauzungusha Ofeli, akauinua juu sana; akaweka maakida mashujaa katika miji yote ya Yuda yenye maboma.
2 Chroniques 27.3 Néhémie 3.3 1 Rois 1.33 Néhémie 12.39 Sophonie 1.10
15 Akaiondoa miungu migeni, na hiyo sanamu nyumbani mwa Bwana, na madhabahu zote alizozijenga katika mlima wa nyumba ya Bwana, na Yerusalemu, akazitupa nje ya mji.
2 Chroniques 33.3-33.7 Ezéchiel 18.20-18.22 Esaïe 2.17-2.21 Osée 14.1-14.3 2 Rois 21.7
16 Akaijenga madhabahu ya Bwana, akatoa juu yake dhabihu za sadaka za amani, na za shukrani, akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli.
Lévitique 3.1-3.17 2 Chroniques 33.9 Luc 22.32 Genèse 18.19 Lévitique 7.11-7.18
17 Lakini watu wakaendelea kutoa dhabihu katika mahali pa juu, ila wakamtolea Bwana, Mungu wao tu.
2 Chroniques 32.12 1 Rois 22.43 2 Rois 15.4 2 Chroniques 15.17
18 Basi mambo yote ya Manase yaliyosalia, na maombi yake kwa Mungu wake, na maneno ya waonaji walionena naye kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, tazama, yameandikwa kati ya mambo ya wafalme wa Israeli.
2 Chroniques 33.19 Amos 7.12 Esaïe 30.10 Michée 3.7 1 Rois 14.19
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.
Proverbes 15.8 2 Chroniques 30.11 1 Jean 1.9 2 Chroniques 36.12 Psaumes 119.67
20 Basi Manase akalala na babaze, wakamzika nyumbani mwake; na Amoni mwanawe akatawala mahali pake.
2 Rois 21.18-21.25 Matthieu 1.10 2 Chroniques 32.33 1 Chroniques 3.14

Règne d’Amon

21 Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka miwili.
Jacques 4.13-4.15 Luc 12.19-12.20 2 Rois 21.19-21.24 2 Chroniques 33.1
22 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Manase babaye; Amoni akazitolea dhabihu sanamu zote alizozifanya Manase babaye, akazitumikia.
2 Rois 21.1-21.11 Ezéchiel 20.18 2 Chroniques 33.1-33.10 2 Rois 21.20 Esaïe 44.13-44.20
23 Wala hakujinyenyekeza mbele za Bwana, kama Manase babaye alivyojinyenyekeza; lakini huyo Amoni akaongeza makosa juu ya makosa.
2 Chroniques 33.12 2 Chroniques 33.19 2 Chroniques 28.22 Jérémie 7.26 2 Timothée 3.13
24 Wakamfanyia fitina watumishi wake, wakamwua katika nyumba yake mwenyewe.
Romains 11.22 2 Chroniques 24.25-24.26 2 Rois 21.23-21.26 2 Chroniques 25.27-25.28 2 Samuel 4.5-4.12
25 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliomfanyia fitina mfalme Amoni; watu wa nchi wakamfanya Yosia mwanawe awe mfalme badala yake.
2 Chroniques 34.1 Nombres 35.31 Genèse 9.5-9.6 2 Chroniques 36.1 2 Chroniques 26.1

Cette Bible est dans le domaine public.