Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 10.13
Bible en Swahili de l’est


Règne de David

Mort de Saül

1 Basi Wafilisti wakapigana juu ya Israeli; nao watu wa Israeli wakakimbia mbele ya Wafilisti, wakaanguka wameuawa katika mlima Gilboa.
1 Samuel 31.1-31.13 1 Chroniques 10.8 1 Samuel 28.4 2 Samuel 1.6 1 Samuel 28.1
2 Nao Wafilisti wakamfuatia sana Sauli na wanawe; Wafilisti wakawaua Yonathani, na Abinadabu, na Malkishua, wana wa Sauli.
1 Chroniques 8.33 Esaïe 57.1-57.2 1 Chroniques 9.39 2 Rois 25.7 1 Samuel 14.49
3 Tena vita vilikuwa vikali sana juu ya Sauli, na wapiga upinde wakampata; hata akafadhaika sana kwa sababu ya wapiga upinde.
Amos 2.14 Genèse 49.23-49.24 1 Samuel 31.3-31.6 2 Samuel 1.4-1.10
4 Ndipo Sauli akamwambia yule mchukua silaha zake, Futa upanga wako, unichome nao, wasije watu hawa wasiotahiriwa wakanisimanga. Lakini huyo mchukua silaha zake akakataa; kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akautwaa upanga wake, akauangukia.
1 Samuel 31.4 Juges 9.54 1 Chroniques 10.5 2 Samuel 17.23 1 Samuel 17.26
5 Na mchukua silaha zake alipoona ya kuwa Sauli amekufa, yeye naye akauangukia upanga wake, akafa.
6 Hivyo Sauli akafa, na wanawe watatu; na nyumba yake yote wakafa pamoja.
1 Samuel 4.18 1 Samuel 4.10-4.11 Ecclésiaste 9.1-9.2 Osée 13.10-13.11 1 Samuel 12.25
7 Kisha watu wote wa Israeli, waliokuwa huko bondeni, walipoona ya kuwa wamekimbia, na ya kuwa Sauli na wanawe wamekufa, wakaiacha miji yao, wakakimbia; nao Wafilisti wakaenda wakakaa humo.
Deutéronome 28.33 Juges 6.2 Deutéronome 28.43 1 Samuel 13.6 Lévitique 26.31
8 Hata ikawa siku ya pili yake Wafilisti walipokwenda kuwateka nyara hao waliouawa, walimwona Sauli na wanawe wameanguka juu ya mlima Gilboa.
1 Samuel 31.8 2 Chroniques 20.25 2 Rois 3.23
9 Wakamvua mavazi, wakamtwalia kichwa, na silaha zake, kisha wakapeleka wajumbe kwenda nchi ya Wafilisti pande zote, ili kutangaza habari kwa sanamu zao, na kwa watu.
Daniel 5.23 1 Samuel 31.9-31.10 Daniel 5.2-5.4 2 Samuel 1.20 Juges 16.23-16.24
10 Wakaziweka silaha zake nyumbani mwa miungu yao, wakakikaza kichwa chake nyumbani mwa Dagoni.
1 Samuel 5.2-5.7 1 Samuel 31.10
11 Na watu wote wa Yabesh-gileadi waliposikia hayo yote Wafilisti waliyomtenda Sauli,
2 Samuel 2.4-2.7 1 Samuel 31.11-31.13 1 Samuel 11.1-11.11
12 wakainuka mashujaa wote, wakautwaa mwili wake Sauli, na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi, wakaizika mifupa yao chini ya mwaloni huko Yabeshi, nao wakafunga muda wa siku saba.
Genèse 50.10 2 Samuel 3.35 Genèse 35.8 2 Samuel 21.12-21.14
13 Basi Sauli alikufa kwa sababu ya kosa lake alilomkosa Bwana, kwa sababu ya neno la Bwana, asilolishika; na tena kwa kutaka shauri kwa mwenye pepo wa utambuzi, aulize kwake,
Lévitique 20.6 1 Samuel 15.23 Lévitique 19.31 Esaïe 8.19 Deutéronome 18.10-18.14
14 asiulize kwa Bwana; kwa hiyo akamwua, na ufalme akamgeuzia Daudi, mwana wa Yese.
1 Samuel 15.28 1 Samuel 13.14 2 Samuel 3.9-3.10 1 Chroniques 12.23 1 Samuel 28.17

Cette Bible est dans le domaine public.