Règne de David
Mort de Saül
 1 Basi Wafilisti wakapigana juu ya Israeli; nao watu wa Israeli wakakimbia mbele ya Wafilisti, wakaanguka wameuawa katika mlima Gilboa.
1 Samuel 31.1-31.13  1 Chroniques 10.8  1 Samuel 28.4  2 Samuel 1.6  1 Samuel 28.1  
 2 Nao Wafilisti wakamfuatia sana Sauli na wanawe; Wafilisti wakawaua Yonathani, na Abinadabu, na Malkishua, wana wa Sauli.
1 Chroniques 8.33  Esaïe 57.1-57.2  1 Chroniques 9.39  2 Rois 25.7  1 Samuel 14.49  
 3 Tena vita vilikuwa vikali sana juu ya Sauli, na wapiga upinde wakampata; hata akafadhaika sana kwa sababu ya wapiga upinde.
Amos 2.14  Genèse 49.23-49.24  1 Samuel 31.3-31.6  2 Samuel 1.4-1.10  
 4 Ndipo Sauli akamwambia yule mchukua silaha zake, Futa upanga wako, unichome nao, wasije watu hawa wasiotahiriwa wakanisimanga. Lakini huyo mchukua silaha zake akakataa; kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akautwaa upanga wake, akauangukia.
1 Samuel 31.4  Juges 15.18  Juges 16.23-16.25  Juges 9.54  1 Chroniques 10.5  
 5 Na mchukua silaha zake alipoona ya kuwa Sauli amekufa, yeye naye akauangukia upanga wake, akafa. 
6 Hivyo Sauli akafa, na wanawe watatu; na nyumba yake yote wakafa pamoja.
1 Samuel 4.18  1 Samuel 4.10-4.11  Ecclésiaste 9.1-9.2  Osée 13.10-13.11  1 Samuel 12.25  
 7 Kisha watu wote wa Israeli, waliokuwa huko bondeni, walipoona ya kuwa wamekimbia, na ya kuwa Sauli na wanawe wamekufa, wakaiacha miji yao, wakakimbia; nao Wafilisti wakaenda wakakaa humo.
Deutéronome 28.33  Juges 6.2  Deutéronome 28.43  1 Samuel 13.6  Lévitique 26.31  
 8 Hata ikawa siku ya pili yake Wafilisti walipokwenda kuwateka nyara hao waliouawa, walimwona Sauli na wanawe wameanguka juu ya mlima Gilboa.
1 Samuel 31.8  2 Chroniques 20.25  2 Rois 3.23  
 9 Wakamvua mavazi, wakamtwalia kichwa, na silaha zake, kisha wakapeleka wajumbe kwenda nchi ya Wafilisti pande zote, ili kutangaza habari kwa sanamu zao, na kwa watu.
Daniel 5.23  1 Samuel 31.9-31.10  Daniel 5.2-5.4  2 Samuel 1.20  Juges 16.23-16.24  
 10 Wakaziweka silaha zake nyumbani mwa miungu yao, wakakikaza kichwa chake nyumbani mwa Dagoni.
1 Samuel 5.2-5.7  1 Samuel 31.10  
 11 Na watu wote wa Yabesh-gileadi waliposikia hayo yote Wafilisti waliyomtenda Sauli,
2 Samuel 2.4-2.7  1 Samuel 31.11-31.13  1 Samuel 11.1-11.11  
 12 wakainuka mashujaa wote, wakautwaa mwili wake Sauli, na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi, wakaizika mifupa yao chini ya mwaloni huko Yabeshi, nao wakafunga muda wa siku saba.Genèse 50.10  2 Samuel 3.35  Genèse 35.8  2 Samuel 21.12-21.14  
 13 Basi Sauli alikufa kwa sababu ya kosa lake alilomkosa Bwana, kwa sababu ya neno la Bwana, asilolishika; na tena kwa kutaka shauri kwa mwenye pepo wa utambuzi, aulize kwake,
Lévitique 20.6  1 Samuel 15.23  Lévitique 19.31  Esaïe 8.19  Deutéronome 18.10-18.14  
 14 asiulize kwa Bwana; kwa hiyo akamwua, na ufalme akamgeuzia Daudi, mwana wa Yese.
1 Samuel 15.28  1 Samuel 13.14  1 Samuel 16.11-16.13  1 Samuel 28.6  2 Samuel 3.9-3.10