Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 1.19
Bible en Swahili de l’est


Règne de David sur Juda

Annonce de la mort de Saül

1 Ikawa baada ya kufa kwake Sauli, hapo Daudi aliporudi katika kuwaua Waamaleki, naye Daudi amekaa siku mbili katika Siklagi;
2 hata siku ya tatu ikawa, tazama! Akaja mtu kutoka kambi ya Sauli, nguo zake zimeraruliwa, tena ana mavumbi kichwani mwake; basi, ikawa alipomfikia Daudi, akaanguka chini, akamsujudia.
1 Samuel 4.12 2 Samuel 4.10 1 Samuel 25.23 Josué 7.6 Genèse 37.29
3 Daudi akamwambia, Umetoka wapi? Akamwambia, Nimeokoka katika kambi ya Israeli.
2 Rois 5.25 Job 1.15-1.19
4 Daudi akamwambia, Yalikwendaje? Tafadhali uniambie. Akajibu, Watu wamekimbia vitani, tena watu wengi wameanguka wamekufa; hata Sauli naye na Yonathani, mwanawe, wamekufa.
1 Samuel 4.16 1 Chroniques 10.1-10.6 1 Samuel 31.1-31.6
5 Daudi akamwambia yule kijana aliyempa habari, Umejuaje ya kuwa Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?
Proverbes 25.2 Proverbes 14.15
6 Yule kijana aliyempa habari akasema, Nalikuwapo kwa nasibu juu ya kilima cha Gilboa, na tazama, Sauli alikuwa ameegemea fumo lake; na tazama, magari na wapanda farasi wanamfuatia kwa kasi.
1 Samuel 28.4 1 Chroniques 10.4-10.6 Ruth 2.3 Luc 10.31 2 Samuel 1.21
7 Naye alipotazama nyuma, akaniona, akaniita. Nikajibu, Mimi hapa.
Esaïe 65.1 2 Samuel 9.6 1 Samuel 22.12 Juges 9.54 Esaïe 6.8
8 Akaniambia, U nani wewe? Nikamjibu, Mimi ni Mwamaleki.
1 Samuel 30.13 1 Samuel 30.17 1 Samuel 15.3 1 Samuel 30.1 Genèse 14.7
9 Akaniambia, Tafadhali simama karibu nami, ukaniue, maana shida imenipata; kwa sababu roho yangu ingali hai ndani yangu.
10 Basi, nikasimama karibu naye, nikamwua, kwa sababu nalijua hakika ya kuwa hawezi kupona baada ya kuanguka; kisha nikaitwaa ile taji iliyokuwa kichwani mwake, na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.
Juges 9.54 2 Rois 11.12 1 Samuel 31.4-31.5 1 Samuel 22.18 Lamentations 5.16
11 Ndipo Daudi akashika nguo zake akazirarua na kadhalika watu wote waliokuwa pamoja naye;
2 Samuel 3.31 Genèse 37.29 2 Samuel 13.31 Genèse 37.34 Actes 14.14
12 wakaomboleza, wakalia, wakafunga hata jioni, kwa ajili ya Sauli, na kwa ajili ya Yonathani mwanawe, na kwa ajili ya watu wa Bwana na kwa ajili ya nyumba ya Israeli; kwa sababu wameanguka kwa upanga.
2 Samuel 3.35 Matthieu 5.44 2 Corinthiens 11.29 Jérémie 9.1 Amos 6.6
13 Naye Daudi akamwambia yule kijana aliyempa habari, Watoka wapi wewe? Akajibu, Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.
2 Samuel 1.8
14 Daudi akamwambia, Jinsi gani hukuogopa kuunyosha mkono wako umwangamize masihi wa BWANA?
1 Samuel 24.6 1 Samuel 26.9 1 Samuel 31.4 Psaumes 105.15 Nombres 12.8
15 Ndipo Daudi akamwita mmoja wa vijana, akamwambia, Mwendee, ukamwangukie. Basi akampiga hata akafa.
2 Samuel 4.10-4.12 1 Samuel 22.17-22.18 Proverbes 11.18 1 Rois 2.25 1 Rois 2.46
16 Daudi akamwambia, Damu yako na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe; maana umejishuhudia nafsi yako ukisema, Nimemwua masihi wa Bwana.
Matthieu 27.25 1 Rois 2.37 1 Samuel 26.9 Luc 19.22 Lévitique 20.9

Oraison funèbre sur Saül et Jonathan

17 Basi Daudi akamwomboleza Sauli, na Yonathani, mwanawe, maombolezo haya;
2 Chroniques 35.25 Genèse 50.11 2 Samuel 1.19 Jérémie 9.17-9.21
18 (kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema, Wana wa Yuda na wafundishwe haya,
Josué 10.13 Deutéronome 4.10 Genèse 49.8
19 Walio fahari yako, Ee Israeli Juu ya mahali pako palipoinuka wameuawa; Jinsi mashujaa walivyoanguka!
2 Samuel 1.27 2 Samuel 1.25 1 Samuel 31.8 Deutéronome 4.7-4.8 Lamentations 2.1
20 Msiyahubiri mambo haya katika Gathi, Msiyatangaze katika njia za Ashkeloni; Wasije wakashangilia binti za Wafilisti, Binti za wasiotahiriwa wakasimanga.
Michée 1.10 1 Samuel 18.6 Exode 15.20-15.21 Juges 11.34 Juges 16.23-16.24
21 Enyi milima ya Gilboa, visiwepo juu yenu Umande wala mvua, wala mashamba ya matoleo; Maana ndipo ilipotupwa kwa aibu ngao ya shujaa, Ngao yake Sauli, pasipo kutiwa mafuta.
1 Samuel 31.1 Esaïe 21.5 1 Samuel 10.1 Esaïe 5.6 Ezéchiel 31.15
22 Kutoka kwa damu yao waliouawa, Kutoka kwa shahamu yao mashujaa, Upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, Wala upanga wa Sauli haukurudi bure.
1 Samuel 18.4 Esaïe 34.6-34.7 1 Samuel 14.6-14.14 Deutéronome 32.42
23 Sauli na Yonathani walipendwa na kupendeza Maishani wala mautini hawakutengwa; Walikuwa wepesi kuliko tai, Walikuwa hodari kuliko simba.
Juges 14.18 Jérémie 4.13 Deutéronome 28.49 Lamentations 4.19 1 Chroniques 12.8
24 Enyi binti za Israeli, mlilieni Huyo Sauli, ambaye aliwavika Mavazi mekundu kwa anasa, Akazipamba nguo zenu dhahabu.
1 Pierre 3.3-3.5 1 Timothée 2.9-2.10 Jérémie 2.32 Psaumes 68.12 Proverbes 31.21
25 Jinsi mashujaa walivyoanguka Katikati ya vita! Ee Yonathani, wewe umeuawa Juu ya mahali pako palipoinuka
2 Samuel 1.19 2 Samuel 1.27 1 Samuel 14.13-14.15 Juges 5.18 Lamentations 5.16
26 Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, Ulikuwa ukinipendeza sana; Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, Kupita upendo wa wanawake.
1 Samuel 18.1-18.4 1 Samuel 23.16 1 Samuel 20.41 1 Samuel 20.17 1 Samuel 19.2
27 Jinsi mashujaa walivyoanguka, Na silaha za vita zilivyoangamia!
2 Samuel 1.25 2 Samuel 1.19 2 Rois 2.12 Ezéchiel 39.9-39.10 2 Rois 13.14

Cette Bible est dans le domaine public.