Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 6.14
Bible en Swahili de l’est


Construction de l’arche de Noé

1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Esdras 9.12 Romains 9.7-9.8 Deutéronome 7.3-7.4 Malachie 2.11 Genèse 4.26
3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
1 Pierre 3.18-3.20 Néhémie 9.30 Psaumes 78.39 Esaïe 63.10 1 Thessaloniciens 5.19
4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Nombres 13.33 Deutéronome 2.20-2.21 Deutéronome 3.11 2 Samuel 21.15-21.22 1 Samuel 17.4
5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.
Matthieu 15.19 Genèse 8.21 Marc 7.21-7.23 Jérémie 17.9 Romains 1.28-1.31
6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.
1 Samuel 15.11 Ephésiens 4.30 Esaïe 63.10 2 Samuel 24.16 1 Samuel 15.29
7 Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.
Osée 4.3 Jérémie 4.22-4.27 Jérémie 12.3-12.4 Proverbes 10.27 Psaumes 37.20
8 Lakini Nuhu akapata neema machoni pa Bwana.
Genèse 19.19 Luc 1.30 2 Timothée 1.18 Actes 7.46 Psaumes 84.11
9 Hivi ndivyo vizazi vya Nuhu. Nuhu alikuwa mtu wa haki, mkamilifu katika vizazi vyake; Nuhu alikwenda pamoja na Mungu.
Luc 1.6 2 Pierre 2.5 Genèse 5.24 Ezéchiel 14.20 Ezéchiel 14.14
10 Nuhu akazaa wana watatu wa kiume, Shemu, na Hamu, na Yafethi.
Genèse 5.32
11 Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.
Ezéchiel 8.17 Esaïe 60.18 Habakuk 2.8 Genèse 7.1 Psaumes 11.5
12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.
Job 22.15-22.17 Psaumes 53.2-53.3 Job 33.27 Luc 3.6 Genèse 6.8
13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.
1 Pierre 4.7 Genèse 6.4 Osée 4.1-4.2 Genèse 6.11-6.12 Amos 8.2
14 Ujifanyie safina ya mti wa mvinje; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami.
1 Pierre 3.20 Luc 17.27 Matthieu 24.38 Exode 2.3
15 Hivi ndivyo utakavyoifanya; mikono mia tatu urefu wa safina, mikono hamsini upana wake, na mikono thelathini kwenda juu kwake.
Genèse 7.20 Deutéronome 3.11
16 Uifanyie safina mwangaza, ukaumalize juu kiasi cha mkono mmoja; ukautie mlango wa safina katika ubavu wake; ukaifanyie dari tatu, ya chini, ya pili, na ya tatu.
Ezéchiel 41.16 Ezéchiel 42.3 2 Samuel 6.16 2 Rois 9.30 Genèse 7.16
17 Na tazama, nitaleta gharika ya maji juu ya nchi, niharibu kila kitu chenye mwili na pumzi ya uhai, kisiwepo chini ya mbingu; kila kilichoko duniani kitakufa.
2 Pierre 2.5 Genèse 7.4 Genèse 7.21-7.23 Psaumes 29.10 1 Pierre 3.20
18 Lakini nitafanya agano langu nawe kuwa thabiti; nawe utaingia katika safina, wewe, na wanao, na mkeo, na wake za wanao, pamoja nawe.
Genèse 7.7 Genèse 7.1 Genèse 17.7 Genèse 7.13 Hébreux 11.7
19 Na katika kila kilicho hai chenye mwili, wawili wa kila namna utawaleta ndani ya safina, kuwahifadhi pamoja nawe; wawe mume na mke.
Psaumes 36.6 Genèse 8.17 Genèse 7.15-7.16 Genèse 7.8-7.9 Genèse 7.2-7.3
20 Katika vyote virukavyo kwa jinsi yake, na kila namna ya mnyama kwa jinsi yake, kila kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake, wawili wa kila namna watakuja kwako ili uwahifadhi.
Genèse 2.19 Genèse 1.28 Actes 10.11-10.12 Genèse 1.20-1.24 Jean 5.40
21 Ukajitwalie chakula cha kila namna kinacholika, ukakusanye, nacho kitakuwa ni chakula chenu na chao.
Genèse 1.29-1.30 Psaumes 145.16 Job 40.20 Matthieu 6.26 Psaumes 136.25
22 Ndivyo alivyofanya Nuhu, sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.
Genèse 7.5 Exode 40.16 Genèse 7.16 Hébreux 11.7-11.8 Matthieu 7.24-7.27

Cette Bible est dans le domaine public.