Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 35.11
Bible en Swahili de l’est


Jacob à Béthel

1 Mungu akamwambia Yakobo, Ondoka, panda uende Betheli, ukakae huko; ukamfanyie Mungu madhabahu huko; yeye aliyekutokea ulipomkimbia Esau, ndugu yako.
Osée 12.4 Genèse 28.10-28.22 Psaumes 46.1 Genèse 12.8 Genèse 16.8
2 Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, Ondoeni miungu migeni iliyoko kwenu, mjisafishe mkabadili nguo zenu.
Genèse 18.19 Genèse 31.19 Josué 24.15 Exode 19.10 Exode 19.14
3 Tuondoke, tupande kwenda Betheli, nami nitamfanyia Mungu madhabahu huko; yeye aliyenisikia siku ya shida yangu, akawa pamoja nami katika njia yote niliyoiendea.
Genèse 31.3 Genèse 31.42 Genèse 32.7 Genèse 32.24 Psaumes 107.6
4 Nao wakampa Yakobo miungu migeni yote iliyokuwa mikononi mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu.
Josué 24.25-24.26 Juges 9.6 Deutéronome 7.25 Exode 32.2-32.4 Esaïe 2.20
5 Wakashika njia, hofu ya Mungu ikaishika miji iliyowazunguka, wala hawakuwafuata wana wa Yakobo.
Exode 23.27 Psaumes 14.5 2 Chroniques 17.10 Josué 5.1 Exode 15.15-15.16
6 Basi Yakobo akafika Luzu, ulio katika nchi ya Kanaani, ndio Betheli, yeye na watu wote waliokuwa pamoja naye.
Genèse 28.19 Genèse 48.3 Juges 1.22-1.26 Genèse 28.22 Genèse 12.8
7 Akajenga huko madhabahu, akapaita mahali pale, El-Betheli; kwa sababu huko Mungu alimtokea, hapo alipomkimbia ndugu yake.
Genèse 28.13 Genèse 35.3 Genèse 35.1 Juges 6.24 Ecclésiaste 5.4-5.5
8 Akafa Debora mlezi wa Rebeka, akazikwa chini ya Betheli, chini ya mwaloni; na jina lake likaitwa Alon-bakuthi.
Genèse 24.59 Juges 2.5 Juges 2.1 1 Samuel 31.13
9 Mungu akamtokea Yakobo tena, aliporudi kutoka Padan-aramu akambariki.
Genèse 26.2 Genèse 12.7 Genèse 18.1 Genèse 35.1 Genèse 28.13
10 Mungu akamwambia, Jina lako ni Yakobo; hutaitwa tena Yakobo, lakini Israeli litakuwa jina lako. Akamwita jina lake, Israeli.
Genèse 17.5 Genèse 17.15 1 Rois 18.31 2 Rois 17.34 Genèse 32.27-32.28
11 Mungu akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uzidi ukaongezeke. Taifa na kundi la mataifa watatoka kwako, na wafalme watatoka viunoni mwako.
Genèse 17.1 Genèse 17.16 Exode 6.3 Genèse 17.5-17.7 Genèse 22.17
12 Na nchi hii niliyowapa Ibrahimu na Isaka nitakupa wewe, na uzao wako baada yako nitawapa nchi hiyo.
Genèse 12.7 Genèse 28.13 Genèse 26.3-26.4 Genèse 15.18 Genèse 13.14-13.17
13 Mungu akakwea juu kutoka kwake mahali hapo aliposema naye.
Genèse 17.22 Genèse 18.33 Juges 6.21 Juges 13.20 Genèse 11.5
14 Yakobo akasimamisha nguzo mahali aliposema naye, nguzo ya mawe, akamimina juu yake sadaka ya kinywaji, akamimina mafuta juu yake.
Genèse 28.18-28.19 Genèse 31.45 Genèse 35.20 1 Samuel 7.12 Exode 17.15
15 Yakobo akapaita mahali pale, Mungu aliposema naye, Betheli.
Genèse 28.19

Naissance de Benjamin et mort de Rachel

16 Wakasafiri kutoka Betheli, hata ukabaki mwendo wa kitambo tu kufika Efrathi, Raheli akashikwa na utungu wa kuzaa, na utungu wake ulikuwa mzito.
Michée 5.2 Genèse 48.7 Matthieu 2.18 Matthieu 2.16 Psaumes 132.6
17 Ikawa alipokuwa anashikwa sana na utungu, mzalisha akamwambia, Usiogope, maana sasa utamzaa mwanamume mwingine.
Genèse 30.24 1 Samuel 4.19-4.21
18 Ikawa hapo katika kutoa roho yake, maana alikufa, akamwita jina lake Benoni, lakini babaye alimwita Benyamini.
Luc 12.20 Actes 7.59 Luc 23.46 1 Samuel 4.20-4.21 Lamentations 2.12
19 Akafa Raheli, akazikwa katika njia ya Efrathi, ndio Bethlehemu.
Michée 5.2 Genèse 48.7 Ruth 4.11 Ruth 1.2 Matthieu 2.6
20 Yakobo akasimamisha nguzo juu ya kaburi lake, ndiyo nguzo ya kaburi la Raheli hata leo.
1 Samuel 10.2 2 Samuel 18.17-18.18 Genèse 35.14 Genèse 35.9
21 Kisha akasafiri Israeli akapiga hema yake upande wa pili wa mnara wa Ederi.
Michée 4.8 Luc 2.8
22 Ikawa Israeli alipokuwa akikaa katika nchi ile, Reubeni akaenda akalala na Bilha, suria wa babaye; Israeli akasikia habari. Basi hao wana wa Yakobo walikuwa kumi na wawili.
1 Chroniques 5.1 1 Corinthiens 5.1 Lévitique 18.8 2 Samuel 20.3 Apocalypse 21.14
23 Wana wa Lea ni Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, na Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Zabuloni.
Genèse 46.8-46.15 Genèse 30.18-30.20 Genèse 29.32-29.35 Exode 1.2-1.4 Genèse 33.2
24 Wana wa Raheli, ni Yusufu na Benyamini.
Genèse 30.22-30.24 Genèse 46.19-46.22 Genèse 35.16-35.18
25 Wana wa Bilha, kijakazi wa Raheli, ni Dani na Naftali.
Genèse 46.23-46.25 Genèse 37.2 Genèse 30.4-30.8
26 Wana wa Zilpa, kijakazi wa Lea, ni Gadi na Asheri. Hawa ndio wana wa Yakobo aliozaliwa katika Padan-aramu.
Genèse 46.16-46.18 Genèse 31.18 Genèse 28.2 Genèse 25.20 Genèse 30.9-30.13
27 Yakobo akaja kwa Isaka, babaye, huko Mamre, mji wa Arba, ndio Hebroni, walipokaa ugenini Ibrahimu na Isaka.
Genèse 13.18 Genèse 18.1 Genèse 23.19 Josué 15.13 Genèse 23.2
28 Siku za Isaka zilikuwa miaka mia na themanini.
Genèse 25.7 Genèse 47.28 Genèse 50.26
29 Naye Isaka akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake, ni mzee, ameshiba siku. Esau na Yakobo, wanawe, wakamzika
Genèse 15.15 Genèse 49.33 Genèse 49.31 Genèse 25.7-25.9 Ecclésiaste 12.5-12.7

Cette Bible est dans le domaine public.