Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 29.13
Bible en Swahili de l’est


Jacob à Charan

1 Kisha Yakobo akashika njia yake, akafika nchi ya wana wa mashariki.
Juges 6.3 Juges 6.33 Nombres 23.7 Genèse 28.5-28.7 Genèse 25.20
2 Naye akaangalia, na tazama, kiko kisima kondeni, na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu nacho, kwa sababu katika kisima kile hunywesha makundi; na palikuwa na jiwe kubwa juu ya kinywa cha kisima.
Exode 2.15-2.16 Genèse 24.11 Apocalypse 7.17 Genèse 24.13 Jean 4.14
3 Makundi yote hukusanyika huko, watu wakafingirisha hilo jiwe katika kinywa cha kisima wakawanywesha kondoo, na kulirudisha jiwe juu ya kinywa cha kisima mahali pake.
4 Yakobo akawauliza, Ndugu zangu, watu wa wapi ninyi? Wakasema, Tu wa Harani sisi.
Genèse 28.10 Genèse 27.43 Genèse 11.31 Genèse 24.10 Actes 7.2
5 Akawauliza, Je! Mnamjua Labani, mwana wa Nahori? Wakasema, Tunamjua.
Genèse 24.24 Genèse 24.29 Genèse 31.53
6 Akawauliza, Je! Hajambo? Wakasema, Hajambo; tazama, Raheli binti yake anakuja na kondoo.
Exode 18.7 1 Samuel 17.22 Genèse 37.14 1 Samuel 25.5 2 Samuel 20.9
7 Akasema, Tazama, ukali mchana bado, wala sio wakati wa kukusanya wanyama; wanywesheni kondoo, mwende kuwalisha.
Ephésiens 5.16 Galates 6.9-6.10
8 Wakasema, Hatuwezi, hata yakusanyike makundi yote, watu wakafingirishe jiwe katika kinywa cha kisima, ndipo tunapowanywesha kondoo.
Genèse 34.14 Marc 16.3 Genèse 29.3 Genèse 43.32 Luc 24.2
9 Hata alipokuwa akisema nao, Raheli akaja na kondoo za baba yake, maana aliwachunga.
Genèse 24.15 Exode 2.15-2.16 Cantique 1.7-1.8 Exode 2.21
10 Ikawa Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mamaye, na kondoo za Labani, ndugu wa mamaye, Yakobo akakaribia, na kulifingirisha lile jiwe litoke katika kinywa cha kisima, akawanywesha kondoo za Labani, ndugu wa mamaye.
Exode 2.17
11 Yakobo akambusu Raheli, akainua sauti yake akalia.
Genèse 33.4 Genèse 45.2 Genèse 43.30 Genèse 45.14-45.15 Genèse 29.13
12 Yakobo akamwarifu Raheli ya kuwa yeye ni ndugu wa babaye, na ya kuwa ni mwana wa Rebeka. Basi akapiga mbio akampasha babaye habari.
Genèse 24.28 Genèse 13.8 Genèse 14.14-14.16
13 Ikawa Labani aliposikia habari za Yakobo, mwana wa nduguye, akaenda mbio amlaki, akamkumbatia, akambusu, akamleta nyumbani kwake. Naye akamwambia Labani maneno hayo yote.
Genèse 24.29 Genèse 45.15 Exode 18.7 Exode 4.27 Actes 20.37
14 Labani akamwambia, Ndiwe kweli mfupa wangu na nyama yangu. Naye akakaa kwake muda wa mwezi mmoja.
2 Samuel 19.12-19.13 Genèse 2.23 Juges 9.2 2 Samuel 5.1 Genèse 13.8

Léa et Rachel

15 Labani akamwambia Yakobo, Kwa sababu wewe ni ndugu yangu, basi, je! Unitumikie bure? Niambie mshahara wako utakuwa nini?
Genèse 31.7 Genèse 30.28
16 Labani alikuwa na binti wawili, jina la mkubwa ni Lea, na jina la mdogo ni Raheli.
Genèse 49.31 Ruth 4.11 Genèse 33.2 Genèse 30.19 Genèse 29.25-29.32
17 Naye Lea macho yake yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo, na mzuri uso.
Genèse 12.11 Genèse 30.1-30.2 Proverbes 31.30 Genèse 24.16 Genèse 35.19-35.20
18 Yakobo akampenda Raheli akasema, Nitakutumikia miaka saba kwa kumpata Raheli, binti yako mdogo.
Osée 12.12 Exode 22.16-22.17 Genèse 31.41 Genèse 29.20 Genèse 34.12
19 Labani akasema, Afadhali nikupe wewe kuliko mtu mwingine; kaa kwangu.
Psaumes 12.2 Esaïe 6.11 Esaïe 6.5
20 Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli. Ikawa machoni pake kama siku chache tu kwa vile alivyompenda.
Osée 12.12 1 Corinthiens 13.7 Genèse 30.26 Genèse 24.67 Cantique 8.6-8.7
21 Yakobo akamwambia Labani, Nipe mke wangu, maana siku zangu zimetimia; niingie kwake.
Juges 15.1 Genèse 29.20 Genèse 38.16 Genèse 4.1 Genèse 31.41
22 Labani akakusanya watu wote wa mahali pale, akafanya karamu.
Matthieu 22.2-22.10 Jean 2.1-2.10 Matthieu 25.1-25.10 Juges 14.10-14.18 Ruth 4.10-4.13
23 Ikawa wakati wa jioni akamtwaa Lea, binti yake, akamletea Yakobo, naye akaingia kwake.
Michée 7.5 Genèse 24.65 Genèse 38.14-38.15
24 Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake.
Genèse 30.9-30.12 Genèse 16.1 Genèse 24.59 Genèse 46.18
25 Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda?
Matthieu 7.2 1 Corinthiens 3.13 Matthieu 7.12 Genèse 27.35-27.36 Apocalypse 3.19
26 Sikukutumikia kwa Raheli? Mbona umenidanganya? Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa;
27 timiza siku zake saba, nasi tutakupa huyu naye kwa utumishi utakaonitumikia, miaka saba mingine.
Juges 14.12 Lévitique 18.18 Genèse 2.2-2.3 Juges 14.10 Malachie 2.15
28 Yakobo akafanya hivi, akatimiza siku zake saba. Naye akampa Raheli binti yake kuwa mkewe.
29 Labani akampa binti yake Raheli mjakazi wake Bilha, awe mjakazi wake.
Genèse 35.22 Genèse 29.24 Genèse 35.25 Genèse 30.3-30.8 Genèse 37.2
30 Akaingia kwa Raheli naye, akampenda Raheli kuliko Lea, akatumika kwa ajili yake miaka saba mingine.
Genèse 31.41 Genèse 29.18 Genèse 29.20 Genèse 29.31 Matthieu 6.24

Les enfants de Jacob

31 Bwana akaona ya kwamba Lea hakupendwa, naye akafungua tumbo lake; bali Raheli alikuwa hazai.
Deutéronome 21.15 Psaumes 127.3 Genèse 30.22 Genèse 25.21 1 Samuel 1.20
32 Lea akapata mimba akazaa mwana, akampa jina lake, Reubeni, maana alisema, Kwa kuwa Bwana ameona teso langu; sasa mume wangu atanipenda.
Exode 4.31 Deutéronome 26.7 Exode 3.7 Psaumes 25.18 Genèse 31.42
33 Akapata mimba tena akazaa mwana, akasema, Kwa kuwa Bwana amesikia ya kwamba mimi sikupendwa, amenipa na huyu; akamwita jina lake Simeoni.
Genèse 34.25 Genèse 49.5-49.6 Genèse 42.24 Genèse 34.30 Genèse 35.23
34 Akapata mimba tena, akazaa mwana, akasema, Basi wakati huu mume wangu ataungana nami, kwa sababu nimemzalia wana watatu. Kwa hiyo akamwita jina lake Lawi.
Genèse 49.5-49.7 Exode 32.26-32.29 Genèse 34.25 Nombres 18.2-18.4 Deutéronome 33.8-33.10
35 Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu Bwana; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa.
Matthieu 1.2 Genèse 44.18-44.34 Genèse 43.8-43.9 Genèse 49.8-49.12 1 Chroniques 5.2

Cette Bible est dans le domaine public.