Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 12.13
Bible en Swahili de l’est


L’appel d’Abram

1 Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
Hébreux 11.8 Néhémie 9.7 Actes 7.2-7.6 Luc 14.26-14.33 Esaïe 41.9
2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;
Genèse 18.18 Galates 3.14 Genèse 46.3 Genèse 17.4-17.6 Genèse 28.3-28.4
3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.
Genèse 22.18 Genèse 26.4 Genèse 27.29 Galates 3.8 Genèse 18.18
4 Basi Abramu akaenda, kama Bwana alivyomwamuru; Lutu akaenda pamoja naye. Naye Abramu alikuwa mtu wa miaka sabini na mitano alipotoka Harani.
Genèse 11.27 Genèse 11.31 Hébreux 11.8
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani.
Genèse 14.14 Genèse 11.31 Genèse 14.21 Genèse 10.19 Actes 7.4
6 Abramu akapita katikati ya nchi mpaka mahali patakatifu pa Shekemu; mpaka mwaloni wa More. Na Wakanaani siku zile walikaa katika nchi hiyo.
Deutéronome 11.30 Genèse 35.4 Hébreux 11.9 Juges 7.1 Genèse 13.7
7 Bwana akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu Bwana aliyemtokea.
Genèse 17.8 Genèse 13.15 Genèse 18.1 Genèse 17.1 Genèse 13.4
8 Kisha akaondoka huko akaenda mpaka mlima ulio upande wa mashariki wa Betheli, akaipiga hema yake; alikuwa na Betheli upande wa magharibi, na Ai upande wa mashariki, akamjengea Bwana madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana.
Genèse 4.26 Néhémie 11.31 Genèse 28.19 Genèse 21.33 Genèse 35.15-35.16
9 Naye Abramu akasafiri, akazidi kwenda pande za kusini.
Genèse 13.3 Genèse 24.62 Genèse 13.1 Hébreux 11.13-11.14 Psaumes 105.13

Abram en Égypte

10 Basi kulikuwa njaa katika nchi ile; Abramu akashuka Misri, akae huko kwa muda maana njaa ilikuwa nzito katika nchi.
Genèse 43.1 1 Rois 17.1-17.18 Genèse 46.3-46.4 2 Rois 7.1-7.8 2 Rois 4.38
11 Ikawa alipokuwa karibu kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, Tazama, najua ya kuwa u mwanamke mzuri wa uso;
Genèse 26.7 Genèse 29.17 Proverbes 21.30 2 Samuel 11.2 Genèse 12.14
12 basi itakuwa, Wamisri watakapokuona watasema, Huyu ni mkewe; kisha wataniua mimi na wewe watakuacha hai.
Genèse 20.11 Genèse 26.7 Proverbes 29.25 1 Jean 1.8-1.10 Matthieu 10.28
13 Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe heri kwangu kwa ajili yako, na nafsi yangu iishi kwa ajili yako.
Genèse 26.7 Genèse 20.2 Genèse 20.5 Genèse 20.12-20.13 Romains 6.23
14 Basi ikawa Abramu alipofika Misri, Wamisri wakamwona huyo mwanamke ya kwamba yeye ni mzuri sana.
Matthieu 5.28 Genèse 39.7 Genèse 3.6 Genèse 6.2
15 Wakuu wa Farao wakamwona, nao wakamsifu kwa Farao; basi yule mwanamke akachukuliwa nyumbani mwa Farao.
Genèse 20.2 Ezéchiel 32.2 Proverbes 29.12 Esther 2.2-2.16 Osée 7.4-7.5
16 Naye akamtendea Abramu mema kwa ajili yake; naye alikuwa na kondoo na ng’ombe, na punda waume, na watumwa, na wajakazi, na punda wake, na ngamia.
Genèse 20.14 Genèse 13.2 Job 42.12 Genèse 26.14 Genèse 32.13-32.15
17 Lakini Bwana akampiga Farao na nyumba yake mapigo makuu, kwa ajili ya Sarai, mkewe Abramu.
1 Chroniques 16.21 Genèse 20.18 Job 34.19 1 Chroniques 21.22 Psaumes 105.14-105.15
18 Ndipo Farao akamwita Abramu, akasema, N’nini hili ulilonitendea? Mbona hukuniambia ya kuwa huyo ni mkeo?
Genèse 20.9-20.10 Genèse 4.10 Genèse 31.26 1 Samuel 14.43 Genèse 44.15
19 Mbona ulisema, Huyo ni umbu langu, hata nikamtwaa kuwa mke wangu? Basi sasa, huyo mke wako umchukue, uende zako.
20 Farao akawaagiza watu kwa ajili yake, wakampeleka njiani, na mkewe, na kila alichokuwa nacho.
Psaumes 105.14-105.15 1 Samuel 29.6-29.11 Proverbes 21.1 Exode 18.27

Cette Bible est dans le domaine public.