Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 4.1
Bible en Swahili de l’est


Mort d’Éli et de ses deux fils

1 [Ikawa siku zile Wafilisti walikusanyika ili kupigana na Israeli,] nao Waisraeli wakatoka juu ya Wafilisti kwenda vitani;wakatua karibu na Ebenezeri ,nao Wafilisti wakatua huko Afeki.
1 Samuel 29.1 1 Samuel 7.12 1 Samuel 5.1 Josué 19.30 Josué 15.53
2 Nao Wafilisti wakajipanga juu ya Israeli; na walipopigana, Israeli wakapigwa mbele ya Wafilisti; wakauawa watu wa jeshi lao lililokuwa uwandani wapata watu elfu nne.
Psaumes 79.7-79.8 Josué 7.5-7.8 Psaumes 44.9-44.10 Josué 7.12 Psaumes 106.40-106.41
3 Hata watu walipofika kambini, wazee wa Israeli wakasema, Mbona Bwana ametupiga leo mbele ya Wafilisti? Twende tukalilete sanduku la agano la Bwana toka Shilo hata huku, lije kati yetu, na kutuokoa katika mikono ya adui zetu.
Nombres 10.35 Esaïe 58.3 Deutéronome 31.26 1 Samuel 14.18 2 Timothée 3.5
4 Basi wakatuma watu kwenda Shilo, nao wakalileta toka huko sanduku la agano la Bwana wa majeshi, akaaye juu ya makerubi; na Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwako huko pamoja na sanduku la agano la Mungu.
2 Samuel 6.2 Psaumes 80.1 Psaumes 99.1 Nombres 7.89 1 Samuel 2.22
5 Na sanduku la agano la Bwana lilipoingia kambini, Israeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu, hata nchi ikavuma.
Josué 6.5 Job 20.5 Josué 6.20 Amos 6.3 Juges 15.14
6 Nao Wafilisti waliposikia mshindo wa zile kelele, walisema, Maana yake nini mshindo wa kelele hizi kubwa katika kambi ya Waebrania? Wakatambua ya kuwa sanduku la Bwana limefika kambini.
Exode 32.17-32.18
7 Wafilisti wakaogopa, maana walisema, Mungu ameingia kambini. Wakasema, Ole wetu! Kwani halijawa jambo kama hili tangu hapo.
Exode 14.25 Deutéronome 32.30 Exode 15.14-15.16
8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa na mkono wa miungu hawa walio hodari? Hawa ndio miungu waliowapiga Wamisri kwa mapigo ya kila namna jangwani.
Exode 9.14 Exode 7.5 Psaumes 78.43-78.51
9 Iweni hodari, na kufanya kiume enyi Wafilisti, msije mkawa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa watumwa wenu; fanyeni kiume, mkapigane nao.
Juges 13.1 1 Corinthiens 16.13 Ephésiens 6.10-6.11 2 Samuel 10.12 Juges 10.7
10 Wafilisti wakapigana nao, Israeli wakapigwa, wakakimbia kila mtu hemani kwake; wakauawa watu wengi sana; maana katika Israeli walianguka watu thelathini elfu wenye kwenda vitani kwa miguu.
1 Samuel 4.2 2 Rois 14.12 Deutéronome 28.25 2 Samuel 18.17 Lévitique 26.17
11 Hilo sanduku la Mungu Likatwaliwa; na Hofni na Finehasi, wale wana wawili wa Eli, wakauawa.
1 Samuel 2.34 Psaumes 78.64 1 Samuel 2.32 Psaumes 78.60-78.61 Esaïe 3.11
12 Basi, mtu mmoja wa Benyamini akapiga mbio kutoka mle jeshini akafika Shilo siku ile ile, hali nguo zake zimeraruliwa, na mavumbi kichwani mwake.
Josué 7.6 Job 2.12 Néhémie 9.1 2 Samuel 1.2 2 Samuel 15.32
13 Alipofika, tazama, Eli alikuwa ameketi kitini pake kando ya njia, akingojea; maana moyo wake ulitetemeka kwa ajili ya sanduku la Mungu. Na yule mtu alipoingia mjini, akatoa habari, mji wote ukalia.
1 Samuel 1.9 1 Samuel 4.18 Psaumes 26.8 Josué 7.9 Psaumes 137.4-137.6
14 Naye Eli aliposikia kelele za kile kilio, akasema, Maana yake nini kelele za kishindo hiki? Yule mtu akafanya haraka, akaenda, akamwambia Eli.
15 Basi Eli umri wake umepata miaka tisini na minane; na macho yake yamepofuka hata asiweze kuona.
1 Samuel 3.2 Psaumes 90.10 1 Rois 14.4 Genèse 27.1
16 Yule mtu akamwambia Eli, Mimi ndimi niliyetoka jeshini, nami leo hivi nimekimbia toka jeshini. Naye akasema, Yalikwendaje, mwanangu?
2 Samuel 1.4 1 Samuel 3.6 Josué 7.19
17 Yeye aliyeleta habari akajibu, akasema, Israeli wamekimbia mbele ya Wafilisti, tena watu wengi sana wameuawa, hata na wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa pia, na sanduku la Mungu limetwaliwa.
1 Samuel 3.11 1 Samuel 4.10-4.11
18 Ikawa alipolitaja sanduku la Mungu, Eli akaanguka kitini pake kwa nyuma, kando ya mlango, shingo yake ikavunjika, akafa; maana alikuwa mzee, tena mzito. Naye alikuwa amewaamua Israeli miaka arobaini.
1 Samuel 4.21-4.22 1 Pierre 4.17-4.18 1 Samuel 4.13 Psaumes 42.3 Psaumes 69.9
19 Tena mkwewe, mkewe huyo Finehasi, alikuwa mja-mzito, karibu na kuzaa; basi, aliposikia habari ya kutwaliwa sanduku la Mungu, na ya kwamba mkwewe na mumewe wamekufa, akajiinamisha, akazaa; maana utungu wake ulimfikilia.
20 Hata alipokuwa katika kufa, wale wanawake waliohudhuria karibu naye wakamwambia, Usiogope; kwa maana umezaa mtoto mwanamume. Walakini hakujibu, wala hakumtazama.
Genèse 35.17-35.18 Psaumes 77.2 Jean 16.21
21 Akamwita mtoto, Ikabodi, akisema, Huo utukufu umeondoka katika Israeli; kwa sababu sanduku la Mungu lilikuwa limetwaliwa, na kwa sababu ya mkwewe na mumewe.
Psaumes 26.8 Jérémie 2.11 Psaumes 78.61 1 Samuel 4.11 Psaumes 78.64
22 Naam, akasema, Huo utukufu umeondoka katika Israeli; maana sanduku la Mungu limetwaliwa.
Psaumes 137.5-137.6 Jean 2.17

Cette Bible est dans le domaine public.