Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 30.5
Bible en Swahili de l’est


Victoire de David sur les Amalécites

1 Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, hao Waamaleki walikuwa wameshambulia Negebu, na Siklagi, nao wameupiga Siklagi, na kuuchoma moto;
1 Samuel 15.7 1 Samuel 29.11 1 Samuel 27.8-27.10 1 Samuel 29.4 Josué 11.6
2 nao wamewachukua mateka wanawake waliokuwamo wakubwa kwa wadogo; hawakuwaua wo wote, ila wakawachukua, wakaenda zao.
1 Samuel 27.11 Job 38.11 Esaïe 27.8-27.9 Psaumes 76.10 1 Samuel 30.19
3 Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka.
1 Pierre 1.6-1.7 Apocalypse 3.9 Hébreux 12.6 Psaumes 34.19
4 Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakainua sauti zao na kulia, hata walipokuwa hawana nguvu za kulia tena.
Nombres 14.1 Juges 2.4 Nombres 14.39 1 Samuel 4.13 Esdras 10.1
5 Na hao wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, aliyekuwa mkewe Nabali, wa Karmeli.
2 Samuel 2.2 1 Samuel 25.42-25.43 1 Samuel 27.3 2 Samuel 3.2-3.3 1 Samuel 1.2
6 Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
Psaumes 56.3-56.4 Psaumes 56.11 Psaumes 25.17 Psaumes 18.6 Psaumes 27.1-27.3
7 Kisha Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, Tafadhali niletee hapa hiyo naivera. Naye Abiathari akamletea Daudi naivera huko.
1 Samuel 22.20-22.21 1 Rois 2.26 Marc 2.26 1 Samuel 23.2-23.9
8 Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote.
1 Samuel 30.18 1 Samuel 23.2 2 Samuel 5.19 2 Samuel 5.23 1 Samuel 28.6
9 Basi Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye, nao wakakifikilia kijito Besori, ambapo wale walioachwa nyuma walikaa.
1 Samuel 27.2
10 Lakini Daudi akakaza kufuata, yeye na watu mia nne; kwa maana watu mia mbili walikaa nyuma, ambao walitaka kuzimia hata hawakuweza kukivuka hicho kijito Besori.
1 Samuel 30.21 1 Samuel 30.9 1 Samuel 14.31 Juges 8.4-8.5 1 Samuel 14.20
11 Nao wakamkuta Mmisri mavueni, wakamleta kwa Daudi, na kumpa chakula, naye akala; nao wakampa maji ya kunywa;
Romains 12.20-12.21 Luc 10.36-10.37 Deutéronome 15.7-15.11 Deutéronome 23.7 Proverbes 25.21
12 kisha wakampa kipande cha mkate wa tini, na vishada viwili vya zabibu; naye akiisha kula roho yake ikamrudia; kwa maana alikuwa hakula chakula wala kunywa maji, siku tatu mchana na usiku.
Juges 15.19 1 Samuel 14.27 Esther 4.16 Matthieu 27.63 Jonas 1.17
13 Ndipo Daudi akamwuliza, Wewe u mtu wa nani; nawe umetoka wapi? Naye akasema, Mimi ni kijana wa Misri, mtumwa wa Mwamaleki mmoja; bwana wangu aliniacha, kwa sababu tangu siku hizi tatu nalishikwa na ugonjwa.
Proverbes 12.10 Job 31.13-31.15 Jacques 2.13
14 Sisi tulishambulia Negebu ya Wakerethi, na ya milki ya Yuda, na Negebu ya Kalebu; na huo mji wa Siklagi tukauchoma moto.
1 Rois 1.44 1 Rois 1.38 Sophonie 2.5 2 Samuel 8.18 Ezéchiel 25.16
15 Daudi akamwambia, Je! Wewe utaniongoza chini hata nilifikilie jeshi hilo? Naye akasema, Uniapie kwa Mungu, ya kwamba hutaniua, wala kunitia mikononi mwa huyo bwana wangu, nami nitakuongoza chini hata kulifikilia jeshi hilo.
Deutéronome 23.15-23.16 Ezéchiel 17.13 Ezéchiel 17.16 Ezéchiel 17.19 Josué 9.15
16 Na hapo alipokuwa amewaongoza chini, tazama, hao walikuwa wametawanyika juu ya nchi yote, wakila na kunywa, na kufanya karamu, kwa sababu ya hizo nyara kubwa walizochukua katika nchi ya Wafilisti, na katika nchi ya Yuda.
1 Samuel 30.14 Luc 21.34-21.35 1 Samuel 25.36-25.38 1 Thessaloniciens 5.3 Luc 12.19-12.20
17 Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia.
1 Samuel 11.11 Psaumes 18.42 Juges 4.16 1 Samuel 15.3 1 Rois 20.29-20.30
18 Daudi akawapokonya wote waliokuwa wamechukuliwa na Waamaleki; naye Daudi akawaokoa wakeze wawili.
Genèse 14.16
19 Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote.
1 Samuel 30.8 Genèse 14.14-14.16 Psaumes 34.9-34.10 Psaumes 91.9-91.10 Matthieu 6.33
20 Naye Daudi akatwaa makundi yote ya kondoo na ng’ombe, ambao waliwatanguliza mbele ya wanyama wale wengine, wakasema, Hao ndio nyara za Daudi.
1 Samuel 30.26 Nombres 31.9-31.12 Romains 8.37 Esaïe 53.12 2 Chroniques 20.25
21 Kisha Daudi aliwafikilia wale watu mia mbili, waliokuwa wametaka kuzimia, hata wasiweze kumfuata Daudi, wale waliowaacha wakae karibu na kijito cha Besori; nao wakatoka nje ili kumlaki Daudi, na kuwalaki hao watu waliokuwa pamoja naye, naye Daudi alipowakaribia hao watu, aliwasalimu.
Hébreux 13.1 1 Samuel 30.10 Juges 8.15 1 Pierre 3.8
22 Ndipo watu waovu wote na wale wasiofaa, miongoni mwa hao waliokwenda pamoja na Daudi, wakasema, Kwa kuwa watu hawa hawakuenda pamoja na sisi, hatutawapa kitu cho chote katika hizo nyara tulizozitwaa tena, isipokuwa kila mtu atapewa mkewe na watoto wake, wawachukue na kwenda zao.
Deutéronome 13.13 Matthieu 7.12 1 Rois 21.13 1 Samuel 25.17 1 Samuel 25.25
23 Ndipo Daudi akasema, La, ndugu zangu, msitende hivyo katika hizo nyara alizotupa Bwana, ambaye ndiye aliyetuhifadhi, akalitia mikononi mwetu lile jeshi lililokuja kinyume chetu.
Nombres 31.49-31.54 1 Samuel 2.7 Psaumes 121.7-121.8 Psaumes 44.2-44.7 Deutéronome 8.18
24 Tena ni nani atakayewasikiliza ninyi katika jambo hili? Kwa kuwa kama lilivyo fungu lake yeye ashukaye vitani, ndivyo litakavyokuwa na fungu lake huyo akaaye karibu na vyombo; watagawiwa sawasawa.
Nombres 31.27 Josué 22.8 1 Samuel 25.13 Psaumes 68.12
25 Basi ikawa hivyo tangu siku ile na baadaye; akaiweka iwe amri na agizo la Israeli hata leo.
1 Samuel 16.13
26 Basi Daudi alipofika Siklagi, aliwapelekea wazee wa Yuda, rafiki zake, sehemu ya nyara, akasema, Angalieni, zawadi yenu katika nyara za adui za Bwana;
1 Samuel 25.27 Esaïe 32.8 1 Chroniques 12.1-12.15 Proverbes 18.16-18.24 2 Corinthiens 9.5
27 yaani, kwa hao wa Betheli, na kwa hao wa Ramoth-Negebu, na kwa hao wa Yatiri;
Josué 15.48 Josué 19.8 Josué 21.14 Juges 1.22-1.23 Genèse 28.19
28 na kwa hao wa Aroeri, na kwa hao wa Sifmothi, na kwa hao wa Eshtemoa;
Josué 13.16 Josué 15.50 Josué 21.14
29 na kwa hao wa Rakali, na kwa hao wa miji ya Wayerameeli, na kwa hao wa miji ya Wakeni;
1 Samuel 27.10 Juges 1.16 1 Samuel 23.19 1 Samuel 15.6
30 na kwa hao wa Horma, na kwa hao wa Korashani, na kwa hao wa Athaki;
Juges 1.17 Josué 19.4 Nombres 14.45 Josué 15.42
31 na kwa hao wa Hebroni, na kwa hao wa kila mahali alipozoelea Daudi mwenyewe na watu wake.
2 Samuel 2.1 2 Samuel 2.4 Josué 14.13-14.15 2 Samuel 15.10 2 Samuel 4.1

Cette Bible est dans le domaine public.