Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 24.18
Bible en Swahili de l’est


Saül épargné par David à En-Guédi

1 Ikawa, Sauli aliporudi baada ya kuwafuatia Wafilisti, aliambiwa ya kwamba, Daudi yuko katika nyika ya Engedi.
1 Samuel 23.28-23.29 1 Samuel 23.19 Proverbes 25.5 Osée 7.3 Ezéchiel 22.9
2 Ndipo Sauli akatwaa watu elfu waliochaguliwa katika Israeli wote, akaenda kumtafuta Daudi na watu wake juu ya majabali ya mbuzi-mwitu.
1 Samuel 26.2 Psaumes 104.18 Psaumes 38.12 1 Samuel 13.2 Psaumes 141.6
3 Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, na huko kulikuwa na pango; Sauli akaingia ndani ili kuifunika miguu. Na Daudi na watu wake walikuwa wakikaa mle pangoni ndani sana.
Juges 3.24 Psaumes 142.1-142.7 Psaumes 57.1-57.11 Psaumes 141.6
4 Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia Bwana, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema. Basi Daudi akainuka, akaukata upindo wa vazi lake Sauli kwa siri.
1 Samuel 26.8-26.11 1 Samuel 25.28-25.30 1 Samuel 23.17 2 Samuel 4.8 Job 31.31
5 Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.
2 Samuel 24.10 1 Jean 3.20-3.21 2 Samuel 12.9 2 Rois 22.19
6 Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA,neon hili,kuunyosha mkono wangu juu yake,kwa maana yeye ni masihi wa BWANA.
1 Thessaloniciens 5.15 2 Samuel 1.14 Romains 12.14-13.2 1 Samuel 26.9-26.11 Matthieu 5.44
7 Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaache kumwondokea Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake.
Psaumes 7.4 Matthieu 5.44 1 Samuel 25.33 Romains 12.17-12.21
8 Daudi naye akainuka baadaye, akatoka pangoni, akamwita Sauli, akisema, Bwana wangu, mfalme. Na Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama uso wake hata nchi, akamsujudia.
1 Samuel 25.23-25.24 1 Samuel 20.41 1 Pierre 2.17 Romains 13.7 1 Samuel 26.17
9 Daudi akamwambia Sauli, Kwa nini unasikiliza maneno ya watu wasemao, Tazama, Daudi anataka kukudhuru?
Lévitique 19.16 Ecclésiaste 7.21-7.22 Proverbes 25.23 Psaumes 101.5 Proverbes 26.28
10 Tazama, leo hivi macho yako yameona jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu pangoni, na watu wengine wakaniambia nikuue; lakini nikakuacha; nikasema, Sitaki kuunyosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa maana yeye ni masihi wa BWANA.
1 Samuel 24.4 Psaumes 105.15 1 Samuel 26.8-26.9
11 Tena, baba yangu, tazama, tafadhali, tazama upindo wa vazi lako mkononi mwangu; maana ikiwa nimeukata upindo wa vazi lako, nisikuue, ujue, na kuona ya kuwa hakuna uovu wala kosa mkononi mwangu, wala sikukukosa neno; ingawa wewe unaniwinda roho yangu ili kuikamata.
1 Samuel 26.20 1 Samuel 23.23 1 Samuel 23.14 2 Rois 5.13 Proverbes 15.1
12 Bwana atuamue, mimi na wewe, na Bwana anilipizie kisasi changu kwako; lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.
Genèse 16.5 Juges 11.27 Psaumes 43.1 Romains 12.19 Job 5.8
13 Kama vile walivyosema watu wa kale katika mithali yao, Katika waovu hutoka uovu; ila mkono wangu hautakuwa juu yako.
Matthieu 7.16-7.18 Matthieu 7.20 Matthieu 12.33-12.34 Matthieu 15.19
14 Na mfalme wa Israeli ametoka ili kumfuatia nani? Unamwinda nani? Ni kuwinda mbwa mfu, au kiroboto.
1 Samuel 26.20 2 Samuel 9.8 1 Samuel 17.43 2 Samuel 6.20 Juges 8.1-8.3
15 Basi Bwana atuamue, akatuhukumu mimi na wewe, akaone, akanitetee neno langu, akaniokoe na mkono wako.
Psaumes 43.1 1 Samuel 24.12 Psaumes 35.1 Psaumes 119.154 Michée 7.9
16 Ikawa, Daudi alipokwisha kumwambia Sauli maneno hayo Sauli alisema, Hii ndiyo sauti yako, Daudi, mwanangu? Naye Sauli akapaza sauti yake, akalia.
1 Samuel 26.17 Proverbes 25.11 Job 6.25 Actes 6.10 Genèse 33.4
17 Akamwambia Daudi, Wewe u mwenye haki kuliko mimi; maana wewe umenitendea mema, nami nimekutenda mabaya.
1 Samuel 26.21 Matthieu 5.44 Genèse 38.26 Psaumes 37.6 Romains 12.20-12.21
18 Nawe umeonyesha leo jinsi ulivyonitendea mema, kwani Bwana aliponitia mikononi mwako, hukuniua.
1 Samuel 26.23 1 Samuel 23.7 Psaumes 31.8 1 Samuel 23.12 1 Samuel 26.8
19 Maana mtu akimwona adui yake, je! Atamwacha aende zake salama? Basi Bwana na akulipe mema kwa haya uliyonitendea leo.
Proverbes 25.21-25.22 Juges 17.2 1 Samuel 23.21 Psaumes 18.20 1 Samuel 26.25
20 Na sasa, angalia, najua ya kuwa hakika utakuwa mfalme, na ufalme wa Israeli utafanyika imara mkononi mwako.
1 Samuel 23.17 Matthieu 2.3-2.6 Matthieu 2.16 1 Samuel 20.30-20.31 1 Samuel 13.14
21 Basi sasa, uniapie kwa Bwana, ya kwamba hutawakatilia mbali wazao wangu baada yangu, wala hutaliharibu jina langu katika mbari ya baba yangu.
Genèse 21.23 2 Samuel 21.6-21.8 1 Samuel 20.14-20.17 Genèse 31.48 Hébreux 6.16
22 Naye Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akaenda zake kwao; lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.
1 Samuel 23.29 Proverbes 26.24-26.25 Jean 2.24 Matthieu 10.16-10.17

Cette Bible est dans le domaine public.