Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 11.10
Bible en Swahili de l’est


Victoire de Saül sur les Ammonites

1 Ikawa, kama baada ya mwezi mmoja, Nahashi, Mwamoni ,akakwea na kupanga marago juu ya Yabesh-gileadi;na watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, Fanya mapatano nasi,na sisi tutakutumikia.
Juges 21.8 1 Rois 20.34 Ezéchiel 17.13 1 Samuel 12.12 Genèse 26.28
2 Huyo Nahashi, Mwamoni, akawaambia, Kwa sharti hii mimi nitapatana nanyi, kila mtu ang’olewe jicho la kuume; na kwa jambo hilo nitawashutumu Waisraeli wote pia.
1 Samuel 17.26 Nombres 16.14 Genèse 34.14 Juges 16.21 Jérémie 39.7
3 Basi wazee wa Yabeshi wakamjibu, Tuachie siku saba, ili tutume wajumbe waende mipakani mwote mwa Israeli; kisha, ikiwa hakuna atakayetuokoa, tutakutokea.
4 Hivyo wajumbe wakafika Gibea ya Sauli, wakasema maneno hayo masikioni mwa watu; na watu wote wakainua sauti zao wakalia.
Juges 2.4 1 Samuel 10.26 1 Samuel 30.4 Juges 21.2 1 Samuel 15.34
5 Na tazama, Sauli akaja akifuata ng’ombe kutoka kondeni; naye Sauli akauliza, Watu hawa wana nini, hata wakalia? Wakamwambia maneno ya watu wale wa Yabeshi.
1 Rois 19.19 Esaïe 22.1 Psaumes 78.71 Genèse 21.17 1 Samuel 9.1
6 Na roho ya Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, hapo alipoyasikia maneno yale, na hasira yake ikawaka sana.
1 Samuel 10.10 Juges 6.34 1 Samuel 16.13 Juges 3.10 Juges 14.6
7 Naye akatwaa jozi ya ng’ombe, akawakata-kata vipande, kisha akavipeleka vile vipande mipakani mwote mwa Israeli kwa mikono ya wajumbe, kusema, Ye yote asiyetoka nyuma ya Sauli na Samweli, ng’ombe zake watatendwa vivi hivi. Basi utisho wa Bwana ukawaangukia wale watu, wakatoka kama mtu mmoja.
Juges 19.29 Juges 20.1 Juges 21.5-21.11 Genèse 35.5 2 Chroniques 17.10
8 Naye akawahesabu huko Bezeki; Waisraeli walikuwa mia tatu elfu, na Wayuda thelathini elfu.
Juges 1.4-1.5 2 Samuel 24.9 2 Chroniques 17.12-17.19 1 Samuel 13.15 1 Samuel 15.4
9 Nao wakawaambia hao wajumbe waliokuja, Waambieni watu wa Yabesh-gileadi, Kesho, wakati wa jua kali, mtapata wokovu. Basi wale wajumbe wakaenda, wakawaarifu watu wa Yabeshi; nao walifurahiwa.
Psaumes 18.17
10 Kwa hiyo watu wa Yabeshi walisema, Kesho tutawatokea, nanyi mtatufanyia yote myaonayo kuwa ni mema.
1 Samuel 11.2-11.3
11 Ikawa, kesho yake, Sauli akawapanga watu katika vikosi vitatu; nao wakaingia katikati ya marago kwenye zamu ya asubuhi, wakawapiga Waamoni hata wakati wa jua kali; kisha ikawa wale waliosalia wakatawanyika, hata wasiachwe wawili wao pamoja.
Juges 7.16 Juges 9.43 Psaumes 46.1 Juges 4.16 1 Samuel 30.17-30.18
12 Ndipo watu walipomwambia Samweli, Ni nani yule aliyesema, Je! Huyo Sauli atatutawala? Walete watu hao, ili tuwaue.
1 Samuel 10.27 Luc 19.27 Psaumes 21.8
13 Lakini Sauli akasema, Hakuna mtu atakayeuawa leo, maana leo Bwana amefanya wokovu katika Israeli.
2 Samuel 19.22 Exode 14.13 1 Samuel 19.5 Exode 14.30 Esaïe 59.16
14 Kisha Samweli akawaambia watu, Haya! Na twendeni mpaka Gilgali, ili tuuimarishe ufalme huko mara ya pili.
1 Samuel 10.8 1 Samuel 7.16 1 Samuel 10.24-10.25 1 Chroniques 12.38-12.39 1 Samuel 5.3
15 Nao watu wote wakaenda Gilgali; wakamtawaza Sauli mbele za Bwana huko Gilgali; wakachinja sadaka za amani mbele za Bwana; na huko Sauli na watu wote wa Israeli wakafurahi sana.
1 Samuel 10.8 1 Samuel 10.17 Osée 13.10-13.11 1 Samuel 12.13-12.15 Jacques 4.16

Cette Bible est dans le domaine public.