Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jude 1.13
Bible en Swahili de l’est


Adresse et salutation

1 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, kwa hao walioitwa, waliopendwa katika Mungu Baba, na kuhifadhiwa kwa ajili ya Yesu Kristo.
Jean 14.22 1 Pierre 1.5 Romains 1.1 1 Thessaloniciens 5.23 Luc 6.16
2 Mwongezewe rehema na amani na upendano.
2 Pierre 1.2 1 Pierre 1.2 Apocalypse 1.4-1.6 Romains 1.7

Avertissements contre les prétendus enseignants

3 Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.
1 Timothée 6.12 Jude 1.20 Tite 1.4 Philippiens 1.27 Apocalypse 12.11
4 Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.
Galates 2.4 2 Pierre 2.1-2.3 1 Jean 2.22 1 Pierre 2.8 2 Pierre 2.10
5 Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasioamini.
Psaumes 106.26 Nombres 26.64-26.65 Hébreux 3.16-4.2 Nombres 14.22-14.37 2 Pierre 3.1
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
2 Pierre 2.4 Ephésiens 6.12 Matthieu 8.29 Matthieu 25.41 Jean 8.44
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
Deutéronome 29.23 2 Pierre 2.6 Romains 1.26-1.27 Matthieu 25.41 Osée 11.8
8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
Hébreux 13.17 1 Pierre 2.17 1 Corinthiens 3.17 Genèse 3.5 Actes 23.5
9 Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.
Apocalypse 12.7 1 Thessaloniciens 4.16 Daniel 10.13 Daniel 12.1 Zacharie 3.2
10 Lakini watu hawa huyatukana mambo wasiyoyajua, na mambo wayatambuayo kwa asili wajiharibu kwayo kama wanyama wasio na akili.
2 Pierre 2.12 Romains 1.21-1.22
11 Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora.
2 Pierre 2.15 1 Jean 3.12 Genèse 4.3-4.14 Nombres 26.9-26.10 Nombres 16.1-16.35
12 Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;
Matthieu 15.13 Proverbes 25.14 Ephésiens 4.14 Ezéchiel 34.8 2 Pierre 2.17-2.20
13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.
Philippiens 3.19 Esaïe 57.20 2 Pierre 2.17 Apocalypse 8.10-8.11 Psaumes 93.3-93.4
14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,
Deutéronome 33.2 1 Thessaloniciens 3.13 2 Thessaloniciens 1.7-1.8 Psaumes 50.3-50.5 Matthieu 25.31
15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake.
1 Samuel 2.3 Psaumes 94.4 Psaumes 37.6 Romains 2.16 Apocalypse 13.11
16 Watu hawa ni wenye kunung’unika, wenye kulalamika, waendao kwa tamaa zao, na vinywa vyao vyanena maneno makuu mno ya kiburi, wakipendelea watu wenye cheo kwa ajili ya faida.
2 Pierre 2.18 2 Pierre 2.10 Jude 1.18 1 Corinthiens 10.10 Nombres 16.11
17 Bali ninyi, wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo,
2 Pierre 3.2 Ephésiens 2.20 Ephésiens 4.11 Actes 20.35 1 Jean 4.6
18 ya kwamba waliwaambia ya kuwa, Wakati wa mwisho watakuwako watu wenye kudhihaki, wakizifuata tamaa zao wenyewe za upotevu.
2 Pierre 3.3 Actes 20.29 2 Timothée 4.3 Jude 1.16 2 Pierre 2.1
19 Watu hao ndio waletao matengano, watu wa dunia hii tu, wasio na Roho.
1 Corinthiens 2.14 Osée 9.10 Hébreux 10.25 Romains 8.9 Jacques 3.15

Recommandations aux chrétiens

20 Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu,
Ephésiens 6.18 Colossiens 2.7 Romains 8.26-8.27 1 Corinthiens 14.15 1 Thessaloniciens 5.11
21 jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele.
2 Pierre 3.12 Apocalypse 12.11 1 Jean 4.16 Hébreux 9.28 2 Timothée 1.16
22 Wahurumieni wengine walio na shaka,
1 Jean 5.16-5.18 Ezéchiel 34.17 Jacques 5.19-5.20 Galates 4.20 Galates 6.1
23 na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.
Apocalypse 3.4 Amos 4.11 1 Corinthiens 3.15 1 Timothée 4.16 Lévitique 13.47-13.59
24 Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu;
Ephésiens 3.20 Ephésiens 5.27 Colossiens 1.22 2 Corinthiens 4.14 Apocalypse 14.5
25 Yeye aliye Mungu pekee, Mwokozi wetu kwa Yesu Kristo Bwana wetu; utukufu una yeye, na ukuu, na uwezo, na nguvu, tangu milele, na sasa, na hata milele. Amina.
Jean 5.44 1 Timothée 1.17 Romains 11.36 Apocalypse 5.13-5.14 Tite 2.13

Cette Bible est dans le domaine public.