Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 5.9
Bible en Swahili de l’est


1 Maana kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi;
Hébreux 8.3 Hébreux 10.11 Hébreux 9.9 Hébreux 2.17 Hébreux 7.27
2 awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu;
Hébreux 7.28 Hébreux 2.18 Hébreux 4.15 Hébreux 12.13 Galates 4.13
3 na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi.
Hébreux 7.27 Hébreux 9.7 Lévitique 16.6 Lévitique 9.7 Lévitique 4.3-4.12
4 Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni.
Exode 28.1 Nombres 16.40 2 Chroniques 26.18 1 Chroniques 23.13 Nombres 16.5
5 Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.
Psaumes 2.7 Jean 8.54 Hébreux 1.5 Jean 7.18 Romains 8.3
6 kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani wa milele Kwa mfano wa Melkizedeki.
Psaumes 110.4 Hébreux 7.17 Hébreux 7.21 Hébreux 5.10 Hébreux 6.20
7 Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;
Matthieu 27.46 Matthieu 27.50 Marc 15.34 Marc 15.37 Hébreux 12.28
8 na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata;
Philippiens 2.8 Jean 4.34 Esaïe 50.5-50.6 Hébreux 10.5-10.9 Hébreux 1.5
9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;
Hébreux 2.10 Psaumes 68.18-68.20 Esaïe 45.22 Romains 2.8 Hébreux 12.2
10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
Hébreux 5.5-5.6 Hébreux 6.20
11 Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia.
2 Pierre 3.16 Matthieu 13.15 Actes 28.27 Marc 8.17-8.18 Luc 24.25
12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.
1 Pierre 2.2 Hébreux 6.1 Hébreux 5.13 1 Corinthiens 3.1-3.3 Esaïe 28.9-28.10
13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.
1 Pierre 2.2 1 Corinthiens 14.20 Esaïe 28.9 2 Timothée 3.16 Ephésiens 4.14
14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.
1 Corinthiens 2.6 Ephésiens 4.13 Esaïe 7.15 Ephésiens 1.18 Romains 14.1

Cette Bible est dans le domaine public.