Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 3.9
Bible en Swahili de l’est


Christ supérieur à Moïse et Josué

1 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu,
Hébreux 4.14-4.15 Philippiens 3.14 Hébreux 2.17 2 Timothée 1.9 Hébreux 10.21
2 aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama Musa naye alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu.
Nombres 12.7 Jean 15.10 1 Timothée 3.15 1 Timothée 1.12 Ephésiens 2.22
3 Kwa maana huyo amehesabiwa kuwa amestahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile yeye aitengenezaye nyumba alivyo na heshima zaidi ya hiyo nyumba.
Hébreux 2.9 1 Pierre 2.5-2.7 Zacharie 6.12-6.13 Colossiens 1.18 1 Corinthiens 3.9
4 Maana kila nyumba imetengenezwa na mtu; ila yeye aliyevitengeneza vitu vyote ni Mungu.
Hébreux 1.2 Hébreux 3.3 Esther 2.10 Esther 3.9
5 Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye;
Nombres 12.7 Hébreux 3.2 Exode 14.31 Hébreux 8.5 1 Timothée 1.12
6 bali Kristo, kama mwana, juu ya nyumba ya Mungu; ambaye nyumba yake ni sisi, kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho.
Hébreux 1.2 1 Corinthiens 3.16 Hébreux 6.11 Hébreux 3.14 1 Timothée 3.15
7 Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake,
Psaumes 95.7-95.11 Hébreux 3.15 Esaïe 55.3 Hébreux 4.7 Psaumes 81.13
8 Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,
Exode 17.7 Proverbes 28.14 Romains 2.5-2.6 Psaumes 106.14 Hébreux 3.12-3.13
9 Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini.
Actes 7.36 Exode 19.4 Actes 13.8 Deutéronome 4.9 Deutéronome 4.3
10 Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu;
Psaumes 95.10 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Psaumes 147.20 Ephésiens 4.30 Psaumes 78.40
11 Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu.
Hébreux 4.3 Hébreux 4.5 Nombres 14.20-14.23 Deutéronome 1.34-1.35 Hébreux 3.18-3.19
12 Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai.
Jérémie 17.9 Jérémie 7.24 Jérémie 17.5 Jérémie 18.12 Hébreux 12.25
13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
Hébreux 10.24-10.25 1 Thessaloniciens 5.11 Ephésiens 4.22 2 Timothée 4.2 Proverbes 28.26
14 Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;
Hébreux 3.6 Romains 11.17 1 Pierre 4.13 Hébreux 6.4 Ephésiens 3.6
15 hapo inenwapo, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha.
Hébreux 3.7-3.8 Psaumes 95.7 Hébreux 10.38 Hébreux 10.29
16 Maana ni akina nani waliokasirisha, waliposikia? Si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Musa?
Nombres 14.2 Nombres 14.30 Deutéronome 1.38 Nombres 14.24 Nombres 14.38
17 Tena ni akina nani aliochukizwa nao miaka arobaini? Si wale waliokosa, ambao mizoga yao ilianguka katika jangwa?
Nombres 14.29 Jude 1.5 Nombres 26.64-26.65 Deutéronome 2.15-2.16 Nombres 14.32-14.33
18 Tena ni akina nani aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake, ila wale walioasi?
Deutéronome 1.34-1.35 Deutéronome 9.23 Psaumes 106.24-106.26 Hébreux 4.6 Hébreux 3.11
19 Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Jean 3.36 Jean 3.18 Marc 16.16 Jude 1.5 1 Jean 5.10

Cette Bible est dans le domaine public.