Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Thessaloniciens 3.8
Bible en Swahili de l’est


1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu;
1 Thessaloniciens 5.25 1 Thessaloniciens 1.8 Ephésiens 6.19-6.20 Colossiens 4.3 Romains 15.30
2 tukaokolewe na watu wasio haki, wabaya; maana si wote walio na imani.
Romains 15.31 2 Corinthiens 4.3-4.4 Deutéronome 32.20 Luc 18.8 Matthieu 23.23
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu.
1 Corinthiens 1.9 2 Timothée 4.18 1 Corinthiens 10.13 1 Thessaloniciens 5.24 Jean 17.15
4 Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba mnayafanya tulivyowaagiza, tena kwamba mtayafanya.
2 Corinthiens 2.3 1 Thessaloniciens 4.10 2 Thessaloniciens 3.6 2 Thessaloniciens 3.12 Philippiens 2.12
5 Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na saburi ya Kristo.
1 Chroniques 29.18 1 Thessaloniciens 1.3 1 Thessaloniciens 3.11 Jérémie 31.33 Hébreux 9.28
6 Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.
1 Corinthiens 5.4 1 Thessaloniciens 5.14 2 Thessaloniciens 2.15 Romains 16.17 2 Thessaloniciens 3.7
7 Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata; kwa sababu hatukuenda bila utaratibu kwenu;
1 Corinthiens 11.1 1 Corinthiens 4.16 2 Thessaloniciens 3.9 1 Thessaloniciens 1.6-1.7 2 Thessaloniciens 3.6
8 wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote.
1 Thessaloniciens 2.9 Actes 18.3 Ephésiens 4.28 1 Thessaloniciens 4.11 Matthieu 6.11
9 Si kwamba hatuna amri, lakini makusudi tufanye nafsi zetu kuwa kielelezo kwenu, mtufuate.
1 Corinthiens 9.4-9.14 2 Thessaloniciens 3.7 1 Thessaloniciens 2.6 Galates 6.6 Jean 13.15
10 Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.
Proverbes 20.4 Genèse 3.19 Proverbes 13.4 1 Thessaloniciens 4.11 Proverbes 24.30-24.34
11 Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.
1 Timothée 5.13 1 Pierre 4.15 2 Thessaloniciens 3.6 1 Thessaloniciens 4.11
12 Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.
1 Thessaloniciens 4.11 Ephésiens 4.28 2 Thessaloniciens 3.8 Proverbes 17.1 1 Timothée 2.2
13 Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.
Galates 6.9-6.10 1 Thessaloniciens 4.1 Luc 18.1 2 Corinthiens 4.1 Psaumes 27.13
14 Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari;
2 Thessaloniciens 3.6 1 Corinthiens 5.11 Tite 3.10 Psaumes 83.16 Hébreux 13.17
15 lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
Galates 6.1 1 Thessaloniciens 5.14 Matthieu 18.15 Tite 3.10 1 Corinthiens 4.14

Bénédiction et salutation

16 Sasa, Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote.
Romains 15.33 Nombres 6.26 Ruth 2.4 Esaïe 26.12 Matthieu 1.23
17 Salamu zangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndiyo alama katika kila waraka, ndio mwandiko wangu.
1 Corinthiens 16.21 1 Samuel 17.18 2 Thessaloniciens 1.5 Colossiens 4.18 Josué 2.12
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi nyote.
Romains 16.20 Romains 16.23

Cette Bible est dans le domaine public.